Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Neno la Yehova Halikosi Kamwe Kutimia
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Novemba 1
    • Yehova Anawalinda Watu Wake

      7. Yehova aliwalinda jinsi gani Waisraeli kutokana na jeshi la Farao?

      7 Namna gani ahadi ya pili, ya kwamba Yehova angewalinda watu wake? Ahadi hiyo ilihusiana na ahadi ya Yehova ya kuwakomboa kutoka Misri na kuwaingiza katika Nchi ya Ahadi. Kumbuka kwamba Farao mwenye hasira aliwafuata Waisraeli akiwa na jeshi lake lenye nguvu, lenye mamia ya magari ya vita. Bila shaka, Farao mwenye kiburi alikuwa na uhakika sana, hasa ilipoonekana kana kwamba Waisraeli walikuwa wamenaswa kati ya milima na bahari! Sasa Mungu akachukua hatua ya kuwalinda watu wake kwa kuweka wingu kati ya kambi hizo mbili. Upande wa Wamisri ulikuwa na giza; na upande wa Waisraeli ulikuwa na nuru. Huku wingu likiwa limewazuia Wamisri kusonga, Musa aliinua fimbo yake na maji ya Bahari Nyekundu yakatengana. Waisraeli wakapata njia ya kuokokea lakini Wamisri wakanaswa. Yehova aliliharibu kabisa jeshi lenye nguvu la Farao na kuwalinda watu Wake walioonekana kana kwamba wangeshindwa.—Kutoka 14:19-28.

      8. Waisraeli walilindwa jinsi gani (a) jangwani na (b) walipoingia katika Nchi ya Ahadi?

      8 Baada ya kuvuka Bahari Nyekundu, Waisraeli walitangatanga katika nchi inayosemekana kuwa ‘jangwa kubwa na la kutisha, lenye nyoka wenye sumu na nge; nchi kame isiyokuwa na maji.’ (Kumbukumbu la Torati 8:15, Biblia Habari Njema) Yehova aliwalinda watu wake katika jangwa hilo pia. Namna gani walipoingia katika Nchi ya Ahadi? Majeshi yenye nguvu ya Wakanaani yaliwapinga. Lakini, Yehova alimwambia Yoshua hivi: “Simama sasa, vuka huu mto Yordani, wewe na watu hawa wote, mwingie katika nchi ambayo ninawapa wao, wana wa Israeli. Hakuna yeyote atakayesimama imara mbele yako siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe, kama vile nilivyokuwa pamoja na Musa. Sitakutupa wala kukuacha kabisa.” (Yoshua 1:2, 5) Maneno hayo ya Yehova hayakukosa kutimia. Katika muda wa miaka sita hivi, Yoshua aliwashinda Wafalme 31 na kuchukua sehemu kubwa ya Nchi ya Ahadi. (Yoshua 12:7-24) Hawangeshinda ikiwa Yehova hangewalinda.

  • Neno la Yehova Halikosi Kamwe Kutimia
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Novemba 1
    • Ulinzi wa Yehova Katika Siku Zetu

      15. Kwa nini ulinzi wa Yehova unahitajiwa katika nyakati za kisasa?

      15 Kama tulivyoona, Waisraeli wa siku za Yoshua walihitaji ulinzi wa Yehova. Je, watu wa Yehova wa nyakati za kisasa hawahitaji ulinzi? Bila shaka wanahitaji! Yesu aliwaonya hivi wafuasi wake: ‘Watu watawatia ninyi katika dhiki na kuwaua ninyi, nanyi mtachukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.’ (Mathayo 24:9) Kwa miaka mingi, Mashahidi wa Yehova katika nchi nyingi wamevumilia upinzani mkali na mateso ya kikatili. Hata hivyo, Yehova amekuwa akiwategemeza watu wake. (Waroma 8:31) Neno lake linatuhakikishia kwamba hakuna chochote, ndiyo, hakuna ‘silaha yoyote itakayofanywa juu yetu,’ itakayosimamisha kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha kuhusu Ufalme.—Isaya 54:17.

      16. Umeona ushuhuda gani ambao unaonyesha kwamba Yehova anawalinda watu wake?

      16 Watu wa Yehova wameendelea kuongezeka hata ingawa wanachukiwa na ulimwengu. Mashahidi wa Yehova wanasitawi katika nchi 236, na hilo linathibitisha kwa kweli kwamba Yehova anatutegemeza na kutulinda kutokana na wale ambao wanataka kutuangamiza au kutunyamazisha. Je, unaweza kukumbuka majina ya viongozi wa kisiasa au wa kidini wenye nguvu ambao waliwanyanyasa vikali watu wa Mungu? Walipatwa na nini? Wako wapi sasa? Wengi wao wameshindwa kabisa, kama Farao katika siku za Musa na Yoshua. Namna gani watumishi wa Mungu wa nyakati za kisasa ambao wamekufa wakiwa waaminifu? Wanalindwa katika kumbukumbu la Yehova. Wako mahali salama zaidi. Ni wazi kwamba ahadi ya Yehova ya kuwalinda imetimia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki