Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumwogopa Mungu Ni “Nidhamu ya Hekima”
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Agosti 1
    • Wakati Ambapo Mtu “Hushangilia Jibu”

      Maneno yanayosemwa kwa ufahamu yanaweza kuwa na matokeo gani mazuri? Mfalme wa Israeli anasema hivi: “Mtu hushangilia jibu la kinywa chake, nalo neno linalosemwa wakati unaofaa ni jema kama nini!” (Methali 15:23) Je, sisi hatushangilii wakati jibu au shauri letu linapofuatwa na matokeo yanakuwa mazuri? Hata hivyo, ili shauri letu liwe na matokeo mazuri, ni lazima litimize matakwa mawili.

      Kwanza, shauri hilo linapaswa kutegemea kabisa Neno la Mungu, Biblia. (Zaburi 119:105; 2 Timotheo 3:16, 17) Kisha, linapaswa kutolewa kwa wakati unaofaa. Hata maneno ambayo ni ya kweli yanaweza kuwa na madhara yanaposemwa kwa wakati usiofaa. Kwa mfano, kumshauri mtu kabla ya kumsikiliza kabisa si jambo la hekima wala halisaidii sana. Kwa hivyo, ni muhimu tuwe ‘wepesi kuhusu kusikia, si wepesi wa kusema.’—Yakobo 1:19.

  • Kumwogopa Mungu Ni “Nidhamu ya Hekima”
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Agosti 1
    • Akituonyesha jinsi ya kuepuka kosa moja ambalo watu wengi hufanya, mfalme wa Israeli anasema hivi: “Moyo wa mwadilifu hutafakari ili kujibu, lakini kinywa cha waovu hububujika mambo mabaya.” (Methali 15:28) Methali hiyo ina shauri zuri kama nini! Mara nyingi majibu ya kijinga na ya kipumbavu ambayo hububujika kutoka kinywani hayatokezi jambo lolote zuri. Tunapofikiria mambo fulani muhimu yanayohusika katika kisa fulani, kutia ndani hali na hisia za wengine, yaelekea hatutasema jambo lolote ambalo huenda tutajutia baadaye.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki