-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha MethaliMnara wa Mlinzi—2006 | Septemba 15
-
-
‘JIPATIE HEKIMA NA USHIKE NIDHAMU’
Sulemani anasema: “Hekima ya kweli huendelea kulia kwa sauti kubwa barabarani.” (Methali 1:20) Kwa nini tusikilize sauti yake kubwa na iliyo wazi? Sura ya pili inataja faida nyingi za kupata hekima. Sura ya tatu inazungumzia jinsi ya kuwa na urafiki wa karibu pamoja na Yehova. Kisha Sulemani anasema: “Hekima ndilo jambo kuu. Jipatie hekima; na pamoja na vyote unavyojipatia, jipatie uelewaji. Shika nidhamu; usiiache.”—Methali 4:7, 13.
Ni nini kitakachotusaidia kukataa njia zisizo za adili za ulimwengu? Sura ya tano ya Methali inajibu hivi: Tumia uwezo wa kufikiri na utambue njia zenye kushawishi za ulimwengu. Fikiria pia matokeo mabaya ya kuhusika katika ukosefu wa adili. Sura inayofuata inaonya juu ya mazoea na mitazamo inayohatarisha uhusiano wetu pamoja na Yehova. Sura ya saba inafafanua vizuri matendo ya mtu asiye na maadili. Sura ya nane inaeleza thamani na ubora wa hekima kwa njia yenye kuvutia. Sura ya tisa ambayo ni umalizio wenye kusisimua wa methali zilizotangulia, ina mfano unaotuchochea kuwa wenye hekima.
-
-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha MethaliMnara wa Mlinzi—2006 | Septemba 15
-
-
METHALI MOJA MOJA ZA KUTUONGOZA
Methali zilizobaki za Sulemani ni methali moja moja zinazoeleza mambo kwa ufupi. Zinaonyesha tofauti kati ya mambo na kuyalinganisha, nazo zina masomo muhimu kuhusu mwenendo, usemi, na mtazamo.
Sura ya 10 hadi ya 24 zinakazia umuhimu wa kumwogopa na kumheshimu Yehova. Methali zilizo katika sura ya 25 hadi ya 29 ziliandikwa na “watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.” (Methali 25:1) Methali hizo zinatufundisha kumtegemea Yehova na pia mambo mengine muhimu.
-
-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha MethaliMnara wa Mlinzi—2006 | Septemba 15
-
-
“UJUMBE MZITO”
Kitabu cha Biblia cha Methali kinamalizia kwa sura mbili zenye “ujumbe mzito.” (Methali 30:1; 31:1) Kwa kutumia ulinganifu unaotuchochea kufikiri, ujumbe wa Aguri unaonyesha jinsi ambavyo pupa haiwezi kutoshelezwa na jinsi njia za mwanamume anayemshawishi mwanamwali zisivyoweza kujulikana.b Pia, ujumbe huo unaonya dhidi ya kujiinua na kuongea kwa hasira.
Ujumbe mzito ambao Lemueli alipokea kutoka kwa mama yake una mashauri mazuri kuhusu kutumia divai na kileo na pia kuhukumu kwa uadilifu. Ufafanuzi wa mke mwema unamalizika kwa maneno haya: “Mpeni baadhi ya matunda ya mikono yake, nazo kazi zake na zimsifu malangoni.”—Methali 31:31.
-