-
Jiji la Kale la Yerusalemu Liliharibiwa Mwaka Gani?—Sehemu ya KwanzaMnara wa Mlinzi—2011 | Oktoba 1
-
-
Orodha ya Ptolemy
Orodha ya Majina ya Wafalme iliyoandikwa na mtaalamu wa nyota wa karne ya pili W.K. Claudius Ptolemy, inatumiwa pia kuunga mkono mwaka wa 587 K.W.K. Orodha ya wafalme ya Ptolemy inaonwa kuwa msingi wa mfuatano wa matukio ya historia ya kale, kutia ndani kipindi cha Milki Mpya ya Babiloni.
Ptolemy aliandika orodha yake miaka 600 hivi baada ya kipindi cha Milki Mpya ya Babiloni kuisha. Basi, aliamua jinsi gani mwaka ambao mfalme wa kwanza kwenye orodha yake alianza kutawala? Ptolemy alieleza kwamba kwa kutumia hesabu za wataalamu wa nyota, ambazo kwa kadiri fulani zilitegemea kupatwa kwa mwezi, “tumehesabu kurudi nyuma mpaka mwanzo wa utawala wa Nabonassar,” mfalme wa kwanza kwenye orodha yake.4 Hivyo, Christopher Walker wa Jumba la Makumbusho la Uingereza anasema kwamba orodha ya Ptolemy ilikuwa “mbinu iliyokusudiwa kuwapa wataalamu wa nyota mfuatano mzuri wa matukio,” bali “si kuwapa wanahistoria rekodi sahihi kuhusu kuinuka na kufa kwa wafalme.”5
“Kwa muda mrefu, wataalamu wa nyota wameona Orodha hiyo kuwa yenye kutegemeka,” anaandika Leo Depuydt, mmoja kati ya wasomi wanaomtetea sana Ptolemy, “lakini hilo halimaanishi kwamba lazima Orodha hiyo iwe inategemeka kihistoria.” Profesa Depuydt anaongeza hivi kuhusu orodha hiyo ya wafalme: “Kuhusiana na watawala wa kale [ambao wanatia ndani wafalme wa Milki Mpya ya Babiloni], Orodha hiyo inahitaji kulinganishwa na maandishi ya kikabari ili kujua wakati ambao kila mfalme alitawala.”6
‘Maandishi hayo ya kikabari’ ambayo yanatusaidia kuchunguza usahihi wa orodha ya kihistoria ya Ptolemy ni nini? Yanatia ndani mfuatano wa matukio ya Wababiloni, orodha ya wafalme, na mambo ya kiuchumi—ambayo yaliandikwa na waandishi walioishi wakati wa Milki Mpya ya Babiloni, au karibu na wakati huo.7
Orodha ya Ptolemy inalingana jinsi gani na maandishi ya kikabari? Sanduku lenye kichwa “Orodha ya Ptolemy Inatofautiana Jinsi Gani na Mabamba ya Kale?” (lililo hapa chini) linaonyesha sehemu ya orodha hiyo na kuilinganisha na hati nyingine za kale za maandishi ya kikabari. Ona kwamba Ptolemy anaorodhesha wafalme wanne tu katikati ya watawala wa Babiloni, Kandalanu na Nabonido. Hata hivyo Orodha ya Wafalme ya Uruk—ambayo ni sehemu ya maandishi ya kikabari—inaonyesha kwamba kulikuwa na wafalme saba katikati ya wafalme hao wawili wa Babiloni. Je, wafalme hao saba walitawala kwa vipindi vifupi visivyo na umaana wowote? Kulingana na maandishi ya kikabari kuhusu mambo ya kiuchumi, mmoja wao alitawala kwa miaka saba.8
Pia, kuna uthibitisho mkubwa kwenye hati za maandishi ya kikabari kwamba kabla ya utawala wa Nabopolasa (mfalme wa kwanza katika kipindi cha Milki Mpya ya Babiloni), mfalme mwingine (Ashur-etel-ilani) alitawala milki ya Babiloni kwa miaka minne. Pia, kwa zaidi ya mwaka mmoja, hakukuwa na mfalme katika nchi hiyo.9 Hata hivyo, habari hizo zote hazipo katika orodha ya Ptolemy.
Kwa nini Ptolemy hakuorodhesha watawala fulani? Inaelekea kwamba hakuwaona kuwa watawala halali wa Babiloni.10 Kwa mfano, hakuorodhesha Labashi-Marduk, ambaye alikuwa mfalme katika Milki Mpya ya Babiloni. Lakini kulingana na maandishi ya kikabari, kwa kweli wafalme ambao hawakuorodheshwa na Ptolemy walitawala milki ya Babiloni.
Kwa ujumla, orodha ya Ptolemy inaonwa kuwa sahihi. Lakini kwa kufikiria habari ambazo haikutaja, je, inapaswa kutumiwa kama msingi hakika wa mfuatano wa matukio ya kihistoria?
-
-
Jiji la Kale la Yerusalemu Liliharibiwa Mwaka Gani?—Sehemu ya KwanzaMnara wa Mlinzi—2011 | Oktoba 1
-
-
4. Kitabu Almagest, cha Tatu, 7, kilichotafsiriwa na G. J. Toomer, katika Ptolemy’s Almagest, kilichochapishwa mwaka wa 1998, ukurasa wa 166. Ptolemy alijua kwamba wataalamu wa nyota wa Babiloni walitumia mbinu fulani za “kuhesabu” wakati uliopita na wakati ambao ungefuata wa kupatwa kwa mwezi kwa sababu walitambua kwamba vipindi vinavyofanana vya kupatwa kwa mwezi vilitukia kila baada ya miaka 18.—Almagest, cha Nne, 2.
-
-
Jiji la Kale la Yerusalemu Liliharibiwa Mwaka Gani?—Sehemu ya KwanzaMnara wa Mlinzi—2011 | Oktoba 1
-
-
[Chati/Picha katika ukurasa wa 30]
(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)
ORODHA YA PTOLEMY INATOFAUTIANA JINSI GANI NA MABAMBA YA KALE?
Ptolemy hataji wafalme fulani katika orodha yake. Kwa nini?
ORODHA YA PTOLEMY
Nabonassar
Nabu-nadin-zeri (Nadinu)
Mukin-zeri na Pul
Ululayu (Shalmanesa wa Tano) “Mfalme wa Ashuru”
Merodak-baladani
Sargoni wa Pili “Mfalme wa Ashuru”
Kipindi cha Kwanza Ambacho Hakikuwa na Mfalme
Shamash-shuma-ukin
Kandalanu
Nabopolasa
Nebukadneza
Amel-Marduk
Neriglissar
Nabonido
Koreshi
Cambyses
ORODHA YA WAFALME YA URUK INAYOPATIKANA KATIKA MABAMBA YA KALE
Kandalanu
Sin-shumu-lishir
Sin-sharra-ishkun
Nabopolasa
Nebukadneza
Amel-Marduk
Neriglissar
Labashi-Marduk
Nabonido
[Picha]
Mfuatano wa matukio ya Wababiloni ni sehemu ya maandishi ya kikabari ambayo yanatusaidia kuchunguza usahihi wa orodha ya Ptolemy
[Hisani]
Photograph taken by courtesy of the British Museum
-