-
Unaalikwa kwa UchangamfuMnara wa Mlinzi—2009 | Februari 1
-
-
Hotuba ya Biblia
Mkutano wa kwanza ambao watu wengi wanahudhuria ni hotuba inayotegemea Biblia iliyokusudiwa watu wote, ambayo kwa kawaida inatolewa mwisho wa juma. Mara nyingi Yesu Kristo alitoa hotuba za watu wote, na hotuba inayojulikana zaidi ni Mahubiri ya Mlimani. (Mathayo 5:1; 7:28, 29) Mtume Paulo aliwahutubia wanaume wa Athene. (Matendo 17:22-34) Kwa kufuata kielelezo hicho, mikutano ya Mashahidi wa Yehova inatia ndani hotuba iliyokusudiwa watu wote, baadhi yao wakiwa watu ambao wamehudhuria mkutano kwa mara ya kwanza.
Mkutano huo unaanza kwa wimbo kutoka katika kitabu Mwimbieni Yehova Sifa.a Wote ambao wanataka kusimama na kuimba wimbo huo wanakaribishwa kufanya hivyo. Baada ya sala fupi, msemaji anayestahili anatoa hotuba ya dakika 30. (Ona sanduku “Hotuba za Watu Wote Zinazohusu Mambo Halisi.”) Hotuba yake inategemea kabisa Biblia. Msemaji anawaomba mara nyingi wasikilizaji wafungue maandiko yanayopatana na kichwa cha hotuba na kufuatana naye anapoyasoma. Hivyo, unaweza kuja na Biblia yako mwenyewe, au umwombe mmoja wa Mashahidi wa Yehova akupe Biblia kabla ya mkutano.
-
-
Unaalikwa kwa UchangamfuMnara wa Mlinzi—2009 | Februari 1
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 21]
Hotuba za Watu Wote Zinazohusu Mambo Halisi
Kuna hotuba za Biblia zaidi ya 170 zinazotegemea vichwa mbalimbali kutoka katika Maandiko kama vile:
◼ Asili ya Wanadamu—Je, Ni Muhimu Kuchunguza Unaloamini?
◼ Maoni ya Kimungu Juu ya Ngono na Ndoa
◼ Kuangamiza Dunia Huleta Lipizo la Kimungu
◼ Kushughulika na Mahangaiko ya Maisha
◼ Je, Uhai Ndio Uu Huu Tu?
[Picha katika ukurasa wa 21]
Hotuba ya Biblia
-