Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuzungumza kwa njia ya kawaida
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    • Unaposoma Mbele ya Watu. Unahitaji kutia bidii ili usome kwa njia ya kawaida. Ili ufaulu, tambua mawazo makuu katika habari utakayosoma, na utazame jinsi mawazo hayo yanavyokuzwa. Uyaweke wazi akilini; ama sivyo, utakuwa ukisoma tu maneno. Chunguza jinsi maneno usiyofahamu yanavyotamkwa. Fanya mazoezi ya kusoma kwa sauti ili ujue jinsi ya kubadili sauti na kusoma maneno fulani pamoja kwa njia inayofanya maana iwe wazi. Fanya mazoezi hayo kwa kurudia-rudia mpaka uweze kusoma vizuri. Fahamu habari hiyo kabisa ili unaposoma kwa sauti, usomaji wako usikike kana kwamba ni mazungumzo yenye shauku. Huko ndiko kuzungumza kwa njia ya kawaida.

  • Kuzungumza kwa njia ya kawaida
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    • Ndugu wengine wanaostahili hupewa migawo ya kutoa hotuba za kusoma katika kusanyiko. Iwe unasoma Biblia au vichapo vingine, soma sehemu zenye alama za mnukuo kwa njia inayofanya habari iwe halisi. Kama watu kadhaa wananukuliwa katika habari unayosoma, badili sauti yako kwa njia fulani ili kuiga sauti zao. Lakini tahadhari: Usiige sauti hizo kupita kiasi, lakini usome kwa uchangamfu na kwa njia ya kawaida.

      Kusoma kwa njia ya kawaida ni kama mazungumzo. Ni halisi na inasadikisha.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki