-
Kutumia Maswali VizuriFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
SOMO LA 44
Kutumia Maswali Vizuri
MASWALI huhusisha wasikilizaji kwa sababu yanahitaji majibu ya mdomo au ya kimoyomoyo. Maswali yanaweza kukusaidia kuanzisha mazungumzo na kuyafurahia. Ukiwa msemaji na mwalimu, unaweza kutumia maswali kuamsha upendezi wa mtu, kumsaidia mtu asababu kuhusu habari fulani, au kukazia jambo unalosema. Maswali mazuri yanawasaidia wengine kufikiri badala ya kusikiliza tu. Uwe na kusudi fulani akilini, na uulize maswali kwa njia inayokusaidia kutimiza kusudi hilo.
-
-
Kutumia Maswali VizuriFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Ili Kutokeza Mambo Muhimu. Ikiwa unahutubia watu au unazungumza na mtu, jaribu kutumia maswali yanayoelekeza kwenye mambo muhimu. Hakikisha unauliza maswali ambayo kwa kweli wasikilizaji wangependa kujua majibu yake. Pia unaweza kutumia maswali yanayochochea fikira kwa sababu majibu yake si wazi. Ukitua kifupi baada ya kuuliza swali, inaelekea wasikilizaji watasikiliza kwa hamu zaidi mambo yanayofuata.
Pindi moja nabii Mika alitumia maswali kadhaa. Baada ya kuuliza juu ya takwa la Mungu kwa waabudu wake, nabii huyo aliuliza maswali mengine manne, labda kila swali likiwa na jibu. Maswali hayo yote yanawasaidia wasomaji kutazamia majibu yenye ufahamu wa ndani ambayo nabii huyo anamalizia mazungumzo. (Mika 6:6-8) Je, unaweza kufanya hivyo unapofundisha? Ebu jaribu.
Ili Kusababu Juu ya Habari. Maswali yanaweza kutumiwa kuwasaidia wengine waelewe sababu zinazotolewa. Yehova alifanya hivyo alipotoa matangazo mazito dhidi ya Israeli kama tunavyoona katika Malaki 1:2-10. Kwanza aliwaambia: “Nimewapenda ninyi.” Hawakuthamini upendo huo, akawauliza: “Je, Esau siye ndugu yake Yakobo?” Kisha Yehova akataja hali ya ukiwa ya Edomu ili kuthibitisha kwamba kwa sababu ya uovu wao, Mungu hakupenda taifa hilo. Kisha akaendelea kutoa mifano na kuuliza maswali ili kukazia jinsi ambavyo Israeli limeshindwa kuitikia vizuri upendo wake. Baadhi ya maswali hayo yanaulizwa kana kwamba ni makuhani wasio waaminifu wanayauliza. Mengine ni maswali ambayo Yehova anawauliza makuhani. Mazungumzo hayo yanatugusa moyo na kuvuta uangalifu wetu, na kusababu kunakotumiwa ni wazi kabisa, na ujumbe unaotolewa hauwezi kusahaulika.
Wasemaji wengine huuliza maswali mazuri kwa njia hiyo. Hata ingawa wasikilizaji hawatarajiwi kujibu, wao huyafikiria, kana kwamba wanashiriki katika mazungumzo hayo.
-
-
Kutumia Maswali VizuriFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Ili Kutia Mkazo. Unaweza kutumia maswali pia kukazia mawazo. Mtume Paulo alifanya hivyo katika Waroma 8:31, 32: “Ikiwa Mungu yuko upande wetu, nani atakayekuwa dhidi yetu? Yeye ambaye hakumwachilia hata Mwana wake mwenyewe bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, kwa nini pia yeye pamoja naye hatatupa sisi kwa fadhili vitu vingine vyote?” Ona kwamba kila swali linategemea maneno anayotangulia kutaja.
Nabii Isaya alionyesha usadikisho thabiti baada ya kuandika hukumu ya Yehova dhidi ya mfalme wa Babiloni, akiongezea kusema: “Maana BWANA wa majeshi amekusudia, naye ni nani atakayelibatili? na mkono wake ulionyoshwa, ni nani atakayeugeuza nyuma?” (Isa. 14:27) Maswali kama hayo huonyesha kwamba jambo linalotajwa haliwezi kukanushwa. Jibu halihitajiwi.
Ili Kufichua Fikira Zisizofaa. Maswali ambayo yamefikiriwa vizuri pia yanasaidia sana kufichua kufikiri kusikofaa. Kabla ya Yesu kumponya mtu fulani, aliwauliza Mafarisayo na wanasheria swali hili: “Je, yaruhusika kisheria kuponya siku ya sabato au sivyo?” Baada ya kumponya, akawauliza swali jingine: “Ni nani kati yenu, ikiwa mwana wake au fahali aanguka ndani ya kisima, hatamtoa nje mara hiyo siku ya sabato?” (Luka 14:1-6) Yesu hakutarajia wamjibu wala hawakumjibu. Maswali hayo yalifichua fikira zao zisizofaa.
Nyakati nyingine, hata Wakristo wa kweli wanaweza kufikiri isivyofaa. Katika karne ya kwanza, wengine katika Korintho walikuwa wakishtaki ndugu zao mahakamani ili kusuluhisha matatizo ambayo wao wenyewe walipaswa kuyasuluhisha kati yao. Mtume Paulo alifanyaje? Aliuliza maswali mengi hususa ili kurekebisha fikira zao.—1 Kor. 6:1-8.
-