-
Kuwasaidia Wasikilizaji Kutumia BibliaFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
SOMO LA 19
Kuwasaidia Wasikilizaji Kutumia Biblia
KUSUDI letu ni kuelekeza fikira za kila mtu kwenye Neno la Mungu, Biblia. Kitabu hicho kitakatifu ndicho msingi wa ujumbe tunaohubiri, na tunataka watu watambue kwamba yale tunayosema yanatokana na Mungu wala hatusemi mambo yetu wenyewe. Watu wanahitaji kuitumaini Biblia.
-
-
Kuwasaidia Wasikilizaji Kutumia BibliaFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Katika Mikutano ya Kutaniko. Wote wasaidiwe kutumia Biblia katika mikutano ya kutaniko. Kuna faida nyingi za kufanya hivyo. Kunawasaidia wasikilizaji wakazie fikira mambo yanayozungumzwa. Kunakazia maneno ya msemaji kwa sababu wasikilizaji wenyewe wanayasoma maneno hayo. Na kufanya hivyo kunawasadikisha wale wanaopendezwa kwamba kwa kweli Biblia ndiyo msingi wa imani yetu.
Wasikilizaji watafuatana nawe unaposoma Maandiko katika Biblia ikiwa tu utawasaidia kufanya hivyo. Mojawapo ya njia bora ya kuwatia moyo kutumia Biblia ni kuwaomba wafuatane nawe unaposoma andiko fulani.
Ni daraka la msemaji kuamua maandiko anayotaka kukazia anapowaomba wasikilizaji wafuatane naye. Inafaa kusoma maandiko yanayokusaidia kufafanua mambo makuu. Kisha kadiri wakati unavyoruhusu, ongezea maandiko mengine machache yanayotegemeza jambo unalozungumzia.
Kwa kawaida, haitoshi tu kutaja andiko fulani wala haitoshi kuwaomba wasikilizaji wafuatane nawe unapolisoma. Ukisoma andiko moja kisha usome jingine mbiombio hata kabla ya wasikilizaji kupata wakati wa kufungua lile la kwanza, upesi watachoka na wataacha kujaribu kufuatana nawe unaposoma Biblia. Uwe na utambuzi. Soma andiko wakati wengi wamelipata.
Fikiria kimbele. Taja vizuri andiko hilo mapema kabla ya kulisoma. Jambo hilo litapunguza wakati unaopotea unapongojea wasikilizaji wafungue Biblia zao. Ingawa hutaweza kuzungumzia mambo mengi sana ukiwapa wasikilizaji wakati wa kufungua Biblia, utawafaidi sana.
-