-
Ishara za Mwili na za UsoFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
WATU wa malezi fulani-fulani hutumia ishara zaidi kuliko watu wa malezi mengine. Lakini, karibu kila mtu hutumia ishara za uso na ishara fulani za mwili wanapoongea na watu wengine au wanapohutubia watu.
Yesu na wanafunzi wake wa mapema walizoea kutumia ishara. Pindi moja, mtu fulani alimwambia Yesu kwamba mama yake na ndugu zake wanataka kuongea naye. Yesu alijibu: “Ni nani mama yangu, na ni nani ndugu zangu?” Biblia inaendelea kusema: “Akinyoosha mkono wake kuelekea wanafunzi wake, akasema: ‘Tazama! Mama yangu na ndugu zangu!’” (Mt. 12:48, 49) Biblia inaonyesha katika Matendo 12:17 na 13:16 kwamba mtume Petro na mtume Paulo pia walitumia ishara, na kuna marejeo mengine kama hayo.
-
-
Ishara za Mwili na za UsoFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Jaribu kutoa ishara kwa njia ya kawaida katika hotuba yote. Kama unashindwa kutoa ishara, unaweza kutafuta maneno yanayoonyesha mahali, umbali, ukubwa, au maneno yanayolinganisha mahali fulani na mahali pengine. Hata hivyo, mara nyingi unahitaji tu kutoa hotuba kwa moyo wako, bila kujali watu wanakuonaje, lakini ukiongea na kufanya mambo kama kawaida yako. Mtu akitulia, ishara zake hutokea zenyewe tu.
-
-
Ishara za Mwili na za UsoFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Unapoendelea kupata ujuzi na kuzoea kutulia unapotoa hotuba, ishara zozote za mkazo unazotumia zitaonyesha hisia zako za ndani, usadikisho wako na unyofu wako. Zitafanya maneno yako yawe na maana.
-