Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • ‘maserafi wakiwa wamesimama juu yake.’ Isaya alisema: “Ole wangu! Kwa maana ni kama nimekufa, kwa maana mimi ni mtu asiye na midomo safi, nami ninaishi kati ya watu wasio na midomo safi; kwa maana macho yangu yamemwona Mfalme, Yehova wa majeshi mwenyewe!” Kwa kweli, Isaya aliogopa na kunyenyekea alipotambua ukubwa wa tengenezo la Yehova. Alichochewa sana na jambo hilo hivi kwamba mwito ulipotolewa kutoka mbinguni kuhusu kazi ya pekee ya kutangaza hukumu za Yehova, Isaya aliitikia hivi: “Mimi hapa! Nitume mimi.”—Isa. 6:1-5, 8.

      13 Vivyo hivyo, watu wa Yehova huchochewa wanapolitambua na kulithamini tengenezo lake. Tengenezo linaposonga mbele, sisi hujitahidi kwenda nalo sambamba. Tunajitahidi kuonyesha kwamba tunalitumaini tengenezo la Yehova leo.

      TENGENEZO LA YEHOVA LINASONGA MBELE

      14 Katika sura ya kwanza ya unabii wa Ezekieli, Yehova anaonekana akiendesha gari kubwa sana la kimbingu. Gari hilo lenye fahari linawakilisha sehemu isiyoonekana ya tengenezo la Yehova. Analiendesha gari hilo katika maana ya kwamba analielekeza ifaavyo na kulitumia kutimiza kusudi lake.—Zab. 103:20.

      15 Kila gurudumu la gari hilo lina gurudumu lingine ndani yake lenye ukubwa uleule. Ndiyo sababu inasemekana kwamba magurudumu hayo yaliweza “kwenda upande wowote kati ya zile pande nne.” (Eze. 1:17) Magurudumu hayo yanaweza kubadili mwelekeo mara moja. Hata hivyo, haimaanishi kwamba gari hilo linajielekeza lenyewe tu. Yehova haliachi tengenezo lake liende popote linapotaka. Andiko la Ezekieli 1:20 linasema hivi: ‘Lilienda popote ambapo roho ililielekeza kwenda.’ Kwa hiyo, Yehova ndiye hufanya tengenezo lake liende mahali popote ambapo roho yake inalielekeza. Basi, tunapaswa kujiuliza, ‘Je, ninaenda sambamba na tengenezo hilo?’

      16 Kwenda sambamba na tengenezo la Yehova kunahusisha mengi zaidi ya kuhudhuria mikutano na kushiriki katika huduma ya shambani. Kwanza kabisa, kwenda sambamba na tengenezo kunahusisha kufanya maendeleo na kukua kiroho. ‘Tunahakikisha mambo muhimu zaidi’ na kwenda sambamba na programu ya ulishaji wa kiroho. (Flp. 1:10; 4:8, 9; Yoh. 17:3) Pia, lazima tukumbuke kwamba kila shirika au tengenezo linahitaji kuwa na utaratibu na ushirikiano mzuri. Kwa hiyo tunapaswa kutambua umuhimu wa kutumia kikamili vipaji, mali, na ujuzi wa kiroho ambao Yehova ametupatia ili tutimize kazi yake. Tunapoenda sambamba na gari la kimbingu la Yehova, maisha yetu yanapatana na ujumbe tunaotangaza.

      17 Kwa msaada wa tengenezo la Yehova, sote tunaendelea kufanya mapenzi ya Mungu. Kumbuka kwamba Mwendeshaji wa gari hilo la kimbingu ni Yehova. Kwa hiyo, kwenda sambamba na gari hilo kunaonyesha kwamba tunamheshimu na kumtumaini Yehova, Mwamba wetu. (Zab. 18:31) Biblia inaahidi hivi: “Yehova atawapa nguvu watu wake. Yehova atawabariki watu wake kwa amani.” (Zab. 29:11) Tukiwa sehemu ya tengenezo la Yehova leo, tunapata nguvu kutoka kwake na kuwa na amani anayowapa watu walio katika tengenezo lake. Naam, hatuna shaka hata kidogo kwamba tutaendelea kupata baraka nyingi tunapofanya mapenzi ya Yehova sasa na milele.

  • Kutambua Jukumu la Kristo Katika Mpango wa Mungu
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • SURA YA 2

      Kutambua Jukumu la Kristo Katika Mpango wa Mungu

      “HAPO mwanzo Mungu aliziumba mbingu na dunia,” na kila kitu alichofanya kilikuwa “chema sana.” (Mwa. 1:1, 31) Yehova aliwaumba wanadamu wakiwa na tumaini zuri sana la wakati ujao. Hata hivyo, uasi katika Edeni ulivuruga kwa muda furaha ya wanadamu. Ingawa hivyo, kusudi la Yehova kwa dunia na wanadamu halikubadilika. Mungu alidokeza kwamba wazao watiifu wa Adamu wangekombolewa. Ibada ya kweli ingerudishwa, na Mungu angemharibu yule mwovu pamoja na kazi zake mbovu. (Mwa. 3:15) Kwa mara nyingine tena kila kitu kingekuwa “chema sana.” Yehova angetimiza jambo hilo kupitia Mwana wake, Yesu Kristo. (1 Yoh. 3:8) Kwa hiyo, tunapaswa kutambua jukumu la Kristo katika mpango wa Mungu.—Mdo. 4:12; Flp. 2:9, 11.

      JUKUMU LA KRISTO

      2 Tunapofikiria jukumu la Kristo katika mpango wa Mungu, tunatambua kwamba jukumu lake linahusisha mambo mengi. Yesu ni Mkombozi wa wanadamu, ni Kuhani Mkuu, ni Kichwa cha kutaniko la Kikristo, na sasa ni Mfalme wa Ufalme wa Mungu. Kutafakari majukumu hayo hutufanya tuthamini sana mpango wa Mungu na huzidisha upendo wetu kwa Kristo Yesu. Biblia hufafanua majukumu yake mbalimbali.

      Yesu anatimiza jukumu la msingi katika kutimizwa kwa kusudi la Yehova kwa wanadamu

      3 Wakati wa huduma ya Kristo hapa duniani, ilionekana wazi kwamba wanadamu watiifu kwa Mungu wangepatanishwa kupitia Yesu. (Yoh. 14:6) Akiwa Mkombozi wa wanadamu, Yesu alijitoa awe fidia badala ya wengi. (Mt. 20:28) Kwa hiyo, Yesu anafanya mengi zaidi ya kutuwekea mfano wa kumtumikia Mungu. Anatimiza jukumu la msingi katika kutimizwa kwa kusudi la Yehova kwa wanadamu. Yeye ndiye njia pekee inayotuwezesha kupata tena kibali cha Mungu. (Mdo. 5:31; 2 Kor. 5:18, 19) Kupitia kifo cha Yesu cha kidhabihu na ufufuo wake, wanadamu watiifu wamefunguliwa njia ya kupata baraka za milele chini ya utawala wa Ufalme wa mbinguni wa Mungu.

      4 Akiwa Kuhani Mkuu, Yesu anaweza “kuusikitikia udhaifu wetu” na kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi za wafuasi wake waliojiweka wakfu hapa duniani. Mtume Paulo alieleza hivi: “Kwa maana hatuna kuhani mkuu ambaye hawezi kuusikitikia udhaifu wetu, bali tuna yule ambaye amejaribiwa katika mambo yote kama tulivyojaribiwa, lakini hakutenda dhambi.” Kisha, Paulo akawatia moyo wale wanaomwamini Yesu Kristo watumie kikamili mpango huo wa kupatanishwa na Mungu, aliposema: “Basi na tukikaribie kiti cha ufalme cha fadhili zisizostahiliwa tukiwa na uhuru wa kusema, ili tupokee rehema na kupata fadhili zisizostahiliwa tunapohitaji msaada.”—Ebr. 4:14-16; 1 Yoh. 2:2.

      5 Pia, Yesu ni Kichwa cha kutaniko la Kikristo. Kama ilivyokuwa kwa wafuasi wake wa karne ya kwanza, leo hatuhitaji kiongozi wa kibinadamu. Yesu huongoza kupitia roho takatifu na kupitia wachungaji walio chini yake na chini ya Baba yake wa mbinguni wanapolitunza kundi la Mungu. (Ebr. 13:17; 1 Pet. 5:2, 3) Yehova alitabiri hivi kumhusu Yesu: “Tazameni! Nilimfanya awe shahidi kwa mataifa, Kiongozi na kamanda kwa mataifa.” (Isa. 55:4) Yesu alithibitisha kutimizwa kwa unabii huo alipowaambia hivi wanafunzi wake: “Wala msiitwe viongozi, kwa maana Kiongozi wenu ni mmoja, Kristo.”—Mt. 23:10.

      6 Akionyesha kwamba anataka na yuko tayari kutusaidia, Yesu anatoa mwaliko huu: “Njooni kwangu, nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawaburudisha. Chukueni nira yangu na mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu moyoni, nanyi mtapata burudisho kwa ajili yenu. Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.” (Mt. 11:28-30) Kwa kuwa Yesu Kristo anaongoza kutaniko la Kikristo kwa upole na kwa njia ambayo hutuburudisha, amethibitika kuwa “mchungaji mwema” anayemwiga Baba yake wa mbinguni, Yehova Mungu.—Yoh. 10:11; Isa. 40:11.

      7 Akieleza jambo lingine kuhusu jukumu la Yesu Kristo, Paulo alisema hivi katika barua yake ya kwanza kwa Wakorintho: “Lazima atawale akiwa mfalme mpaka Mungu atakapoweka maadui wote chini ya miguu yake. Lakini vitu vyote vitakapotiishwa kwake, ndipo Mwana mwenyewe atakapojitiisha pia kwa Yule aliyevitiisha vitu vyote kwake, ili Mungu awe vitu vyote kwa kila mtu.” (1 Kor. 15:25, 28) Kabla ya kuja duniani, Yesu alikuwa “mfanyakazi stadi” wa Mungu, na ndiye aliyekuwa wa kwanza kuumbwa na Mungu. (Met. 8:22-31) Mungu alipomtuma duniani, Yesu alifanya mapenzi ya Mungu nyakati zote. Alivumilia jaribu kubwa zaidi na kufa akiwa mwaminifu kwa Baba yake. (Yoh. 4:34; 15:10) Kwa kuwa Mwana wake aliendelea kuwa mshikamanifu hadi kifo, Mungu alimfufua na kumrudisha mbinguni na kumpa haki ya kuwa Mfalme wa Ufalme wa mbinguni. (Mdo. 2:32-36) Kwa hiyo, Kristo Yesu amepewa jukumu kubwa na Mungu la kuongoza maelfu ya viumbe wa roho wenye nguvu katika kukomesha utawala wa wanadamu na kuondoa uovu wote duniani. (Met. 2:21, 22; 2 The. 1:6-9; Ufu. 19:11-21; 20:1-3) Kisha, Ufalme wa mbinguni wa Mungu ukiongozwa na Kristo, utaitawala dunia yote.—Ufu. 11:15.

      INAMAANISHA NINI KUTAMBUA JUKUMU LA KRISTO?

      8 Yesu Kristo ni mkamilifu na ametuwekea mfano bora. Amepewa jukumu la kututunza. Ili tufaidike na utunzaji wake wenye upendo, tunapaswa kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova na kwenda sambamba na tengenezo linalosonga mbele.

      9 Katika karne ya kwanza, wafuasi wa Yesu walielewa kikamili jukumu la Kristo katika mpango wa Mungu. Walionyesha hivyo kwa kufanya kazi kwa umoja chini ya ukichwa wa Kristo, wakifuata mwongozo wake uliotolewa kupitia roho takatifu. (Mdo. 15:12-21) Mtume

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki