-
Fundisha kwa Ufahamu Wenye Kina na UshawishiMnara wa Mlinzi—1999 | Machi 15
-
-
Kutumia Maswali kwa Njia Yenye Matokeo
8. Yesu alitumiaje maswali kwa njia yenye matokeo?
8 Ustadi mwingine wa kufundisha wenye mafaa wahusisha kuuliza maswali yenye matokeo. Yesu Kristo alitumia maswali kwa wingi sana katika ufundishaji wake. Kwa mfano, Yesu alimwuliza Petro: “‘Wewe wafikiri nini, Simoni? Ni kutoka kwa nani wafalme wa dunia hupokea ushuru wa forodhani au kodi ya kichwa? Ni kutoka kwa wana wao au ni kutoka kwa wageni?’ Aliposema: ‘Kutoka kwa wageni,’ Yesu akamwambia: ‘Basi, kwa kweli hao wana hawalipi kodi.’” (Mathayo 17:24-26) Akiwa Mwana mzaliwa-pekee wa Yule aliyeabudiwa kwenye hekalu, kwa kweli Yesu hakuhitajika kulipa kodi ya hekalu. Lakini Yesu aliwasilisha kweli hiyo kwa kutumia maswali kwa njia yenye matokeo. Hivyo, Yesu alimsaidia Petro kufikia mkataa unaofaa uliotegemea habari ambazo tayari alikuwa nazo.
9. Twaweza kutumiaje maswali tunapokuwa kwenye mafunzo ya Biblia?
9 Twaweza kutumia maswali kwa njia nzuri tunapokuwa kwenye mafunzo ya Biblia. Ikiwa mwanafunzi atoa jibu lisilo sahihi, huenda ikashawishi kumweleza jibu sahihi, lakini je, kweli atashika habari hizo? Mara nyingi ni vizuri kumwelekeza mwanafunzi afikie mkataa unaofaa kwa kuuliza maswali. Kwa mfano, ikiwa anapata ugumu wa kuelewa ni kwa nini apaswa kulitumia jina la Mungu, huenda tukauliza, ‘Je, jina lako ni muhimu kwako? . . . Kwa nini? . . . Ungehisije ikiwa mtu fulani angekataa kulitumia jina lako? . . . Je, si jambo lenye sababu nzuri kwa Mungu kututaka tulitumie jina lake la kibinafsi?’
-
-
Fundisha kwa Ufahamu Wenye Kina na UshawishiMnara wa Mlinzi—1999 | Machi 15
-
-
12. Kuna faida gani kuuliza maswali ya maoni?
12 Maswali ya maoni ni yenye mafaa katika kutambua ikiwa kweli mwanafunzi wa Biblia anaamini yale anayojifunza. (Mathayo 16:13-16) Huenda mwanafunzi akajibu kwa usahihi kwamba uasherati ni mbaya. Lakini kwa nini usifuatilie hilo kwa maswali kama vile, Wewe binafsi wahisije juu ya kiwango cha Mungu cha adili? Je, unahisi kwamba ni chenye kuzuia mno? Je, ungeweza kusema kwamba haidhuru ikiwa unafuata viwango vya Mungu au huvifuati?
-