Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Hakuna Aliye na Upendo Mkuu Kuliko Huu”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • 9 Kuna sababu nyingine iliyomchochea Yesu kutoa uhai wake—anawapenda wanadamu. Alianza kuwapenda tangu walipoumbwa. Biblia inafunua jinsi Yesu alivyohisi muda mrefu kabla ya kuja duniani inaposema: “Vitu nilivyopenda sana vilihusiana na wana wa binadamu.” (Methali 8:30, 31) Alionyesha waziwazi upendo wake alipokuwa duniani. Kama tulivyoona katika sura tatu zinazotangulia, Yesu alionyesha katika njia nyingi kwamba anawapenda wanadamu wote na hasa wafuasi wake. Lakini Nisani 14, mwaka wa 33 W.K., alitoa nafsi yake kwa ajili yao. (Yohana 10:11) Kwa kweli, hiyo ndiyo njia kuu zaidi ambayo alionyesha kwamba anatupenda.

  • “Hakuna Aliye na Upendo Mkuu Kuliko Huu”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • Biblia inatuambia: “Kwa hili tumeujua upendo, kwa sababu huyo aliitoa nafsi yake kwa ajili yetu; na sisi tuko chini ya wajibu kuzitoa nafsi zetu kwa ajili ya ndugu zetu.” (1 Yohana 3:16) Kama Yesu, tunapaswa kuwa tayari hata kufa kwa ajili ya ndugu zetu ikihitajika. Wakati wa mateso, afadhali tufe kuliko kuwasaliti ndugu zetu wa kiroho na hivyo kuhatarisha maisha yao. Katika nchi ambazo zimegawanyika kwa sababu ya mizozo ya kikabila au kijamii, tutakuwa tayari kuhatarisha maisha yetu ili kuwalinda ndugu zetu, haidhuru jamii au kabila lao. Mataifa yanapoenda vitani, afadhali tufungwe au hata kufa kuliko kupigana na waamini wenzetu au mtu mwingine yeyote.—Yohana 17:14, 16; 1 Yohana 3:10-12.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki