-
Mungu Anapendekeza Upendo Wake KwetuMnara wa Mlinzi—2011 | Juni 15
-
-
11. Fidia au dhabihu ya ukombozi inategemea ulinganifu gani?
11 Katika andiko lingine Paulo alisema hiyo ni “fidia inayolingana.” (1 Tim. 2:6) Ililingana katika maana gani? Adamu aliwaletea mabilioni ya wazao wake hali ya kutokamilika na kifo. Ni kweli kwamba Yesu, akiwa mwanadamu mkamilifu, angetokeza mabilioni ya wazao wakamilifu.a Hivyo, ilieleweka kwamba maisha ya Yesu pamoja na maisha ya wale wote ambao wangekuwa wazao wake wakamilifu yangetokeza dhabihu inayolingana na maisha ya Adamu na wazao wake wasio wakamilifu. Hata hivyo, Biblia haisemi kwamba wote ambao wangeweza kuwa wazao wa Yesu walikuwa sehemu ya dhabihu ya ukombozi. Andiko la Waroma 5:15-19 linaonyesha kwamba kifo cha “mtu mmoja” tu ndicho kilichowawezesha wanadamu wawekwe huru. Ndiyo, uhai mkamilifu wa Yesu ulilingana na uhai wa Adamu. Jambo ambalo linakaziwa, na ambalo linapaswa kukaziwa ni, Yesu Kristo peke yake.
-
-
Mungu Anapendekeza Upendo Wake KwetuMnara wa Mlinzi—2011 | Juni 15
-
-
a Kwa mfano, maoni hayo kuhusu wazao yalitiwa ndani ya Insight on the Scriptures, Buku la 2, ukurasa wa 736, fungu la 4 na 5 (Étude perspicace des Écritures, Buku la 2, ukurasa wa 728 fungu la 1 na 2).
-