-
Unaweza Kufanikiwa Licha ya Malezi YakoMnara wa Mlinzi—2001 | Aprili 15
-
-
Hata ingawa malezi yetu yalikuwa mabaya tunaweza pia kujinyenyekeza mbele za Mungu, Yehova, na kumstahi yeye na Neno lake, Biblia. Nicholas aliyetajwa mapema, alifanya hivyo. Anasema hivi: “Maisha yangu yalijaa matatizo na taabu kwa sababu nilikuwa mlevi na nilitumia dawa za kulevya, hata hivyo nilipendezwa na Biblia na kutaka kuwa na kusudi maishani. Hatimaye, nilikutana na Mashahidi wa Yehova, nikabadili mwenendo wangu wa maisha, nikakubali ukweli.”
-
-
Unaweza Kufanikiwa Licha ya Malezi YakoMnara wa Mlinzi—2001 | Aprili 15
-
-
Tangu utotoni, Nicholas alikuwa mkaidi. Hata alipojifunza ukweli wa Neno la Mungu, udhaifu huo ulimzuia asimtumikie Yehova kikamili. Kubadili mwelekeo huo hakukuwa jambo rahisi kwake. Hata hivyo, mwishowe akafaulu. Jinsi gani? “Wazee wawili wenye huruma walinisaidia,” Nicholas asema. “Nilikubali kwamba nilikuwa na tatizo, nikaanza kufuata ushauri wao wenye upendo wa Kimaandiko.” Aongeza hivi: “Ijapokuwa mara kwa mara ninaudhika kidogo, sasa nimeshinda ukaidi wangu.”
-