-
“Fanyeni Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu”Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
wa Kristo, tunaepuka kufanya biashara zinazovunja viwango vya Mungu, zinazoweza kulegeza msimamo wetu wa kutounga mkono upande wowote katika mambo ya kisiasa, au zinazohatarisha hali yetu ya kiroho. (Isa. 2:4; 2 Tim. 2:4) Pia, hatushirikiani na “Babiloni Mkubwa,” adui wa kidini wa Mungu.—Ufu. 18:2, 4; 2 Kor. 6:14-17.
27 Kufuata viwango vya uadilifu vya Mungu, kutatuepusha kutumia vibaya ushirika wetu wa Kikristo ili kuendeleza biashara au faida zetu za kibinafsi. Kusudi la kushirikiana na wenzetu kwenye mikutano na makusanyiko ya Kikristo ni kumwabudu Yehova. Tunalishwa katika meza yake ya kiroho na tunafurahia ‘kutiana moyo.’ (Rom. 1:11, 12; Ebr. 10:24, 25) Kwenye ushirika huo tunapaswa kuzungumzia mambo ya kiroho.
KUKAA KATIKA UMOJA WA KIKRISTO
28 Ili watu wa Yehova wafuate viwango vyake vya uadilifu wanahitaji “kudumisha roho ya umoja katika kifungo cha muungano cha amani.” (Efe. 4:1-3) Badala ya kujifikiria wenyewe, kila mmoja hujitahidi kufanya mambo yanayowapendeza wengine. (1 The. 5:15) Bila shaka umejionea roho hiyo katika kutaniko lako. Bila kujali kabila, taifa, jamii, hali yetu ya kiuchumi au elimu yetu, sote tunaongozwa na viwango vilevile vya uadilifu. Hata watu wasio Mashahidi wameona sifa hiyo ya pekee ya watu wa Yehova.—1 Pet. 2:12.
29 Akikazia msingi wa umoja, mtume Paulo aliandika hivi: “Kuna mwili mmoja, na roho moja, kama mlivyoitwa kwenye tumaini moja; Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja; Mungu mmoja ambaye ni Baba wa wote, aliye juu ya wote, na kupitia wote na katika wote.” (Efe. 4:4-6) Maneno hayo yanatuchochea tuwe na ufahamu uleule wa mafundisho ya msingi na pia mafundisho yenye kina ya Biblia ili tuonyeshe kwamba tunatambua mamlaka kuu ya Yehova. Kwa kweli, Yehova amewapa watu wake lugha safi ya kweli inayowawezesha wamtumikie bega kwa bega.—Sef. 3:9.
30 Umoja na amani ya kutaniko la Kikristo huwaburudisha wote wanaomwabudu Yehova. Tumeshuhudia utimizo wa ahadi hii ya Yehova: “Kwa umoja nitawaweka kama kondoo zizini.” (Mika 2:12) Tunataka kudumisha umoja na amani hiyo kwa kuishi kupatana na viwango vya uadilifu vya Yehova.
31 Wenye furaha ni wale waliokubaliwa katika kutaniko safi la Yehova! Tunapaswa kujidhabihu kwa njia yoyote ile ili tuitwe kwa jina la Yehova. Tunapodumisha uhusiano wetu wenye thamani na Yehova, tutajitahidi sana kufuata viwango vyake vya uadilifu na kuwafundisha wengine kufanya hivyo.—2 Kor. 3:18.
-
-
Kudumisha Amani na Usafi wa KutanikoTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
SURA YA 14
Kudumisha Amani na Usafi wa Kutaniko
KAMA unabii wa Biblia ulivyotabiri, kila mwaka maelfu ya watu humiminika kwenye nyumba ya Yehova ya ibada safi. (Mika 4:1, 2) Tunafurahia kwelikweli kuwakaribisha katika “kutaniko la Mungu”! (Mdo. 20:28) Wanathamini sana kumtumikia Yehova pamoja nasi na kufurahia mazingira safi na yenye amani ya paradiso yetu ya kiroho. Roho takatifu ya Mungu na hekima ya Neno lake inatusaidia kudumisha amani na usafi wa kutaniko.—Zab. 119:105; Zek. 4:6.
2 Tunapofuata kanuni za Biblia, tunavaa “utu mpya.” (Kol. 3:10) Hatutilii maanani mabishano madogo-madogo na tofauti za kibinafsi. Tunashinda ushawishi unaosababisha migawanyiko ulimwenguni, na kufanya kazi kwa umoja tukiwa undugu wa kimataifa kwa sababu tuna maoni kama ya Yehova.—Mdo. 10:34, 35.
3 Hata hivyo, mara kwa mara matatizo hutokea ambayo huathiri amani na umoja wa kutaniko. Yanasababishwa na nini? Katika visa vingi, husababishwa na kutofuata ushauri wa Biblia. Bado tunapambana na mwelekeo wetu mbaya tukiwa wanadamu wasio wakamilifu. Hakuna hata mmoja wetu asiyetenda dhambi. (1 Yoh. 1:10) Huenda mtu fulani akachukua hatua isiyofaa ambayo inaweza kuchafua maadili au usafi wa kiroho wa kutaniko. Tunaweza kumkosea mtu fulani kwa
-