Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mungu Aliye “Tayari Kusamehe”
    Mkaribie Yehova
    • Theluji nyeupe imefunika milima

      “Dhambi zenu . . . zitakuwa nyeupe kama theluji”

      10. Yehova anapotusamehe dhambi zetu, kwa nini hatupaswi kuhisi kwamba tuna hatia ya dhambi hizo maisha yetu yote?

      10 Je, umewahi kujaribu kuondoa doa katika nguo nyeupe? Huenda hukufaulu kuondoa doa hilo licha ya jitihada zako zote. Ona jinsi Yehova anavyoeleza msamaha wake: “Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.” (Isaya 1:18, italiki ni zetu.) Usemi “nyekundu sana” waonyesha kwamba rangi hiyo ni nyangavu.b Rangi “nyekundu” ilikuwa mojawapo ya rangi zilizotiwa kwenye nguo. (Nahumu 2:3) Hatuwezi kamwe kuondoa doa la dhambi kwa jitihada zetu. Lakini Yehova anaweza kuondoa dhambi ambazo ni nyekundu sana na kuzifanya nyeupe kama theluji au sufu isiyotiwa rangi. Yehova anapotusamehe dhambi zetu, hatupaswi kuhisi kwamba tuna hatia ya dhambi hizo maisha yetu yote.

  • Mungu Aliye “Tayari Kusamehe”
    Mkaribie Yehova
    • b Msomi mmoja anasema kwamba rangi nyekundu “ilikuwa rangi isiyofifia, rangi ya kudumu. Haingeweza kuondolewa na umande, wala mvua, wala kwa kufuliwa, wala kwa kutumiwa kwa muda mrefu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki