Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Arusi Zenye Kuheshimika Machoni pa Mungu na Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 15
    • 11. Katika nchi fulani, mwanamume na mwanamke hufungaje ndoa, na ni mambo gani yatakayotajwa katika hotuba ya arusi?

      11 Katika nchi fulani, huenda sheria isiruhusu mwanamume na mwanamke wafunge ndoa kwa kufuata utaratibu fulani rasmi, hata mbele ya ofisa wa serikali. Arusi hutukia wakati wanapompa ofisa cheti cha ndoa kilichotiwa sahihi. Mara tu baada ya hapo, cheti hicho cha ndoa huandikishwa. Katika njia hiyo, mwanamume na mwanamke huonwa kuwa mume na mke, na siku hiyo kuwa tarehe ya ndoa yao. Kama ilivyotajwa mwanzoni, huenda wenzi hao waliofunga ndoa wakaamua kwamba hotuba inayotegemea Biblia itolewe kwenye Jumba la Ufalme.

  • Arusi Zenye Kuheshimika Machoni pa Mungu na Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 15
    • 7 Katika nchi nyingi, Kaisari, au serikali, huamua ni nani anayestahili kufunga ndoa. Kwa hiyo, Wakristo wawili ambao wako huru Kimaandiko wanapoamua kufunga ndoa, wanajitahidi kufuata sheria za nchi yao kuhusu ndoa. Huenda sheria hizo zikatia ndani kupata cheti cha ndoa, kutumia ofisa aliyewekwa rasmi na serikali, na labda kuiandikisha ndoa. Kaisari Agusto alipoagiza watu wakafanye “uandikisho,” Maria na Yosefu walitii agizo hilo, nao wakaenda Bethlehemu ‘ili wapate kuandikishwa.’—Luka 2:1-5.

  • Arusi Zenye Kuheshimika Machoni pa Mungu na Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 15
    • Huenda zoea hilo likakubaliwa katika maeneo mengine ingawa si ndoa halali kabisa.d Tunazungumzia ndoa ambayo inafuata desturi zinazotambuliwa na wengi katika kabila au eneo fulani. Huenda hilo likatia ndani kulipa kabisa na kukubaliwa kwa mahari, na hivyo wenzi hao wanakuwa wamefunga ndoa halali kisheria na Kimaandiko. Serikali huona ndoa hiyo ya kimila kuwa halali kisheria na isiyoweza kuvunjwa. Kwa kawaida, ndoa hiyo ya kimila inaweza baadaye kuandikishwa na wenzi kupewa cheti rasmi. Kuandikisha ndoa kunaweza kuwa ulinzi kwa wenzi hao au kwa mke ikiwa atakuwa mjane na kwa watoto wowote ambao huenda wakazaliwa baadaye. Kutaniko linapaswa kumhimiza yeyote ambaye amefanya ndoa ya kimila aiandikishe haraka iwezekanavyo. Inaonekana kwamba chini ya Sheria ya Musa, ndoa na kuzaliwa kwa watoto kuliandikishwa kirasmi.—Mathayo 1:1-16.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki