Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Uwasiliani-roho Waweza Kutosheleza Mahitaji Yetu ya Kiroho?
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Mei 1
    • Wale wanaowasiliana na roho husema kwamba watu wanapokufa wanakuwa viumbe wa roho na kuacha mwili—kama vile kipepeo aachapo kifukofuko chake. Wanaamini kwamba baadaye viumbe hao wa roho huzaliwa upya wakiwa wanadamu ili kuondolea mbali dhambi walizofanya katika maisha ya awali. Lakini dhambi hizo za awali hazikumbukwi tena. “Mungu aliona inafaa dhambi zilizofanywa katika maisha ya awali zisahauliwe,” yasema The Gospel According to Spiritism.

  • Je, Uwasiliani-roho Waweza Kutosheleza Mahitaji Yetu ya Kiroho?
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Mei 1
    • Kwa Nini Watu Wanateseka?

      Wanadamu wengi huteseka sana kwa sababu ya mambo yanayofanywa na watu wasio na hekima, uzoefu, au watu waovu. Namna gani maafa ambayo hayasababishwi na watu? Kwa mfano, kwa nini kuna aksidenti na misiba ya asili? Kwa nini watoto wengine huzaliwa wakiwa na kasoro? Allan Kardec aliona mambo hayo kuwa adhabu. Aliandika: “Ikiwa tunaadhibiwa basi ni lazima tuwe tulifanya kosa fulani. Ikiwa kosa hilo si la wakati huu basi lilifanywa katika maisha yetu ya awali.” Wale wanaowasiliana na roho wanafunzwa kusali hivi: “Bwana, Wewe ni mwenye haki yote. Lazima iwe ninastahili kupatwa na ugonjwa uliochagua unipate . . . naukubali kuwa adhabu kwa makosa niliyofanya katika maisha ya awali na majaribu ya imani na ujitiisho wangu kwa mapenzi Yako matakatifu.”—The Gospel According to Spiritism.

      Je, Yesu alifundisha jambo kama hilo? La. Yesu alifahamu vema maneno haya ya Biblia: “Wakati na tukio lisilotazamiwa huwapata wote.” (Mhubiri 9:11, NW) Alijua kwamba wakati mwingine mambo mabaya hutokea. Si lazima tuwe tunaadhibiwa kwa sababu ya dhambi.

      Fikiria jambo hili lililotukia katika maisha ya Yesu: “[Yesu] alipokuwa akipita aliona mtu aliye kipofu tangu kuzaliwa. Nao wanafunzi wake wakamwuliza: ‘Rabi, ni nani aliyefanya dhambi, mtu huyu au wazazi wake, hivi kwamba akazaliwa kipofu?’” Jibu alilotoa Yesu lilikuwa lenye kuarifu sana: “Mtu huyu hakufanya dhambi wala wazazi wake, bali ilikuwa ili kazi za Mungu zipate kufanywa dhahiri katika kisa chake. Baada ya kusema mambo haya, alitema mate chini akafanya udongo wa mfinyanzi kwa hayo mate, akaweka udongo wake wa mfinyanzi juu ya macho ya mtu huyo na kumwambia: ‘Nenda kajioshe katika dimbwi la Siloamu.’ . . . Na kwa hiyo akaenda na kujiosha, akarudi akiona.”—Yohana 9:1-3, 6, 7.

      Maneno ya Yesu yalionyesha kwamba siyo mtu huyo wala wazazi wake waliofanya azaliwe akiwa kipofu. Kwa hiyo, Yesu hakuunga mkono wazo la kwamba mtu huyo alikuwa akiadhibiwa kwa sababu ya dhambi alizofanya katika maisha yake ya awali. Ni kweli kwamba Yesu alijua kuwa wanadamu wote wamerithi dhambi. Lakini wanarithi dhambi ya Adamu, si dhambi fulani walizofanya kabla ya kuzaliwa. Kwa sababu ya dhambi ya Adamu, wanadamu wote huzaliwa wakiwa watu wasio wakamilifu na wanaweza kupatwa na ugonjwa na kifo. (Ayubu 14:4; Zaburi 51:5; Waroma 5:12; 9:11) Bila shaka, Yesu alitumwa kurekebisha hali hiyo. Yohana Mbatizaji alisema kwamba Yesu alikuwa “Mwana-Kondoo wa Mungu ambaye huondolea mbali dhambi ya ulimwengu!”a—Yohana 1:29.

      Ona pia kwamba, Yesu hakusema kwamba Mungu alifanya mtu huyo azaliwe akiwa kipofu kimakusudi ili Yesu aweze kuja kumponya siku fulani. Hilo lingekuwa tendo la ukatili na lenye kutweza kama nini! Je, jambo hilo lingemletea Mungu sifa? La. Kuponywa kimuujiza kwa mwanamume huyo kipofu ‘kulifanya kazi za Mungu ziwe dhahiri.’ Kama maponyo mengi ambayo Yesu alifanya, ponyo hilo lilionyesha upendo wa kweli wa Mungu kwa wanadamu wanaoteseka. Lilithibitisha pia kutegemeka kwa ahadi Yake ya kumaliza ugonjwa na kuteseka kwa wanadamu katika wakati Wake alioweka.—Isaya 33:24.

      Je, si jambo lenye kufariji kujua kwamba badala ya kusababisha kuteseka, Baba yetu wa mbinguni huwapa “vitu vyema wale wanaomwomba”? (Mathayo 7:11) Aliye Juu Zaidi Sana atapata utukufu ulioje wakati macho ya vipofu yatakapofumbuliwa, na masikio ya viziwi kuzibuliwa, na walemavu kutembea, kuruka, na hata kukimbia!—Isaya 35:5, 6.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki