-
Furahia Likizo Bila Majuto!Amkeni!—1996 | Juni 22
-
-
Kudumisha Mahusiano Mema
Likizo pamoja na familia au marafiki zaweza kuimarisha vifungo vya upendo. Kwa upande ule mwingine, likizo zaweza kusababisha mvunjiko katika uhusiano uwezao kuwa vigumu sana kurekebisha baadaye. Mwandikaji wa habari Lance Morrow alisema hivi: “Hatari halisi ya likizo iko katika uwezo wayo wa kufanya kutoafikiana katika familia kuwe dhahiri zaidi. . . . Watu katika maisha yao ya kawaida wana kazi, madaraka, marafiki na taratibu ambazo hueneza na kufyonza hisia-moyo. Katika mazingira ya nyumba inayotumiwa kwa ajili ya likizo, masuala ya familia yaliyokandamizwa kwa miaka 20 yaweza kuzuka kama mlipuko.”
Kwa hiyo kabla ya kwenda likizoni, azimieni kikweli kuifanya iwe pindi yenye kufurahisha. Kumbukeni kwamba mapendezi hutofautiana. Huenda watoto wakawa wanatafuta utendaji wenye kujasiria, wazazi huenda wanatafuta pumziko. Uwe tayari kuacha mapendezi ya kibinafsi ya jambo la kufanya au mahali pa kwenda. Ikiwa ni jambo la hekima na la kiakili, afikianeni kuruhusu kila mtu kwa kipindi fulani afuatie kile ambacho kinampendeza hasa. Jifunzeni kudhihirisha sifa za roho ya Mungu kila siku katika mwaka wote, kisha haitakuwa vigumu kuendelea kufanya hivyo wakati wa likizo yenu.—Wagalatia 5:22, 23.
Ingawa kudumisha uhusiano mzuri pamoja na familia na marafiki ni jambo la maana, uhusiano wetu pamoja na Mungu ni wa maana hata zaidi. Tukiwa likizoni mara nyingi sisi hukutana na watu ambao hawashiriki maoni yetu ya Kikristo juu ya Mungu na matakwa yake. Kushirikiana karibu nao—labda hata kwenda mara kwa mara mahali penye vitumbuizo vyenye kutilika shaka—kwaweza kutuongoza kwenye matokeo yenye kuleta majuto. Kumbuka Biblia huonya: “Msiongozwe vibaya. Mashirika mabaya huharibu mazoea yenye mafaa.”—1 Wakorintho 15:33, NW.
-
-
Furahia Likizo Bila Majuto!Amkeni!—1996 | Juni 22
-
-
Dumisha Mahusiano Yakiwa Yenye Furaha
1. Onyesha upendo na ufikirio kwa wale walio pamoja nawe.
2. Weka viwango vya ushirika wa kibinafsi vikiwa juu.
3. Usiruhusu waenda-likizo wengine wakuongoze kwenye matendo unayotilia shaka.
4. Weka kando wakati kwa ajili ya kujazilia mahitaji ya kiroho.
-