-
Nawezaje Kujijengea Jina Bila Kuwategemea Ndugu Zangu?Amkeni!—2003 | Novemba 22
-
-
Jifunze Kutokana Nao!
Jitahidi kuona hali yako kuwa fursa ya kujifunza. Kwa mfano, wafikirie ndugu na dada za Yesu Kristo. (Mathayo 13:55, 56) Wazia mambo ambayo wangeweza kujifunza kutokana na ndugu yao mkamilifu! Hata hivyo, “ndugu zake walikuwa hawamwamini.” (Yohana 7:5) Huenda hawakumwamini kwa sababu ya kiburi na wivu. Ndugu za kiroho wa Yesu, yaani wanafunzi wake, ndio walioitikia mwaliko wake: “Mjifunze kutoka kwangu.” (Mathayo 11:29) Baada ya ufufuo wake, ndipo ndugu za Yesu walitambua kwamba wangejifunza kutokana naye. (Matendo 1:14) Kabla ya wakati huo, walipoteza nafasi za pekee za kujifunza kutokana na ndugu yao mashuhuri.
Kaini alifanya kosa hilohilo. Abeli, ndugu yake, alikuwa mtumishi wa Mungu mwenye sifa nzuri. Biblia inasema kwamba “Yehova alikuwa akimtazama Abeli na toleo lake kwa kibali.” (Mwanzo 4:4) Hata hivyo, kwa sababu fulani Mungu “hakumtazama Kaini na toleo lake kwa kibali chochote.” Kaini angejinyenyekeza na kujifunza kutokana na ndugu yake. Badala yake, “Kaini akawaka hasira” na mwishowe akamuua Abeli.—Mwanzo 4:5-8.
Bila shaka huwezi kumkasirikia hivyo ndugu yako. Lakini unaweza pia kupoteza fursa za pekee ukiruhusu kiburi na wivu ukuzuie. Ikiwa ndugu yako anajua sana hesabu, ni hodari katika historia, ni bingwa katika mchezo unaoupenda, anajua Maandiko sana, au ni msemaji stadi, hupaswi kumwonea wivu! Kwani, “wivu hufanya mifupa iwe na ubovu” na unaweza tu kukudhuru. (Methali 14:30; 27:4) Badala ya kumkasirikia ndugu yako, jaribu kujifunza kutoka kwake. Tambua kwamba ana vipawa au stadi ambazo huna. Tazama jinsi anavyofanya mambo au hata umwombe akusaidie.
Barry, aliyetajwa mapema, alifaidika kutokana na mfano mzuri wa ndugu zake. Anasema hivi: “Niliona jinsi ndugu zangu walivyokuwa na furaha kwa sababu walikuwa tayari kuwasaidia wengine kutanikoni na katika mahubiri. Kwa hiyo niliamua kuiga mfano wao, na nikashiriki ujenzi wa Majumba ya Ufalme na Betheli. Uzoefu niliopata umenisaidia kujiamini na kukuza uhusiano wangu pamoja na Yehova.”
-
-
Nawezaje Kujijengea Jina Bila Kuwategemea Ndugu Zangu?Amkeni!—2003 | Novemba 22
-
-
Ni rahisi kuona wivu ikiwa una ndugu ambaye husifiwa mara nyingi. Katika nyakati za Biblia, kijana Yosefu alikuwa mashuhuri kuliko ndugu zake. Ndugu zake walimwonaje? ‘Walianza kumchukia, nao hawakusema naye kwa amani.’ (Mwanzo 37:1-4) Bila shaka, Yosefu alikuwa mnyenyekevu. Lakini ndugu au dada yako anaweza kuchochea chuki na hasira akitajataja mafanikio yake kila wakati.
Vijana fulani huamua kuasi—labda kwa kutofanya vizuri shuleni kimakusudi, kupunguza bidii yao katika utendaji wa Kikristo, au kuwa na mwenendo mbaya. Huenda wakafikiri kwamba ikiwa hawawezi kufanya vyema kama ndugu zao, hakuna haja ya kujitahidi. Lakini, mwishowe uasi utakuumiza tu. Unawezaje kujijengea jina bila kuwategemea ndugu zako na bado ujiheshimu?
-