-
Kile Ambacho Watoto WanahitajiAmkeni!—2003 | Desemba 22
-
-
Kile Ambacho Watoto Wanahitaji
TANGU mtoto anapozaliwa, anahitaji kutunzwa kwa wororo. Anahitaji kupapaswa kwa wororo na kukumbatiwa. Madaktari fulani wanaamini kwamba saa 12 za kwanza za maisha yake ni muhimu sana. Wanasema kwamba mara tu baada ya kuzaliwa, kile ambacho mama na mtoto wanahitaji na wanataka sana ni “kupapasana, kukumbatiana, kutazamana na kusikilizana, bali si kulala wala kula.”a
Kwa kawaida wazazi humshika, humpakata, humpapasa, na kumkumbatia mtoto wao. Naye mtoto huanza kuwa na uhusiano wa karibu na wazazi wake na huitikia wanapomjali. Uhusiano huo ni wenye nguvu sana hivi kwamba wazazi hujitoa mhanga kumtunza mtoto lolote liwalo.
Kwa upande mwingine, mtoto anaweza kudhoofika na kufa wazazi wasipomjali. Hivyo, madaktari fulani husema kwamba mtoto anapaswa kuletwa kwa mama yake mara tu anapozaliwa. Wanapendekeza kwamba anapaswa kuwa na mama yake angalau dakika 30 mpaka 60 za kwanza kabisa za maisha yake.
Ingawa watu fulani husisitiza kwamba mama na mtoto wake wawe pamoja mara tu baada ya kuzaliwa, jambo hilo haliwi rahisi katika hospitali nyingine. Mara nyingi watoto hutenganishwa na mama zao kwa sababu inahofiwa kwamba watoto wataambukizwa magonjwa. Hata hivyo, uthibitisho unaonyesha kwamba mtoto anapokuwa na mama yake haielekei ataambukizwa ugonjwa hatari. Kwa hiyo, hospitali nyingi zaidi zinawaruhusu akina mama kuwa na watoto wao kwa muda mrefu zaidi baada ya kuzaliwa.
Kuhangaikia Uhusiano Wako na Mtoto
Akina mama fulani hawavutiwi na watoto wao wanapowatazama kwa mara ya kwanza. Kwa hiyo, wanajiuliza, ‘Je, nitampenda mtoto wangu?’ Ni kweli kwamba si mama wote wanaowapenda watoto wao mara tu wanapowaona. Lakini hakuna haja ya kuwa na wasiwasi.
Hata mama asipovutiwa na mtoto wake mara moja, anaweza kuvutiwa naye baadaye. Mama mmoja mwenye uzoefu anasema: “Uhusiano wako pamoja na mtoto wako hauathiriwi unapomtazama baada ya kujifungua.” Hata hivyo, ikiwa wewe ni mjamzito na una wasiwasi kuhusu uhusiano wako wa baadaye pamoja na mtoto wako, itafaa uzungumze na daktari wako mapema. Mweleze unataka kuwa na mtoto wako wakati gani na kwa muda gani.
-
-
Kile Ambacho Watoto WanahitajiAmkeni!—2003 | Desemba 22
-
-
“Tafadhali Nitazameni!”
Imegunduliwa kwamba katika mwaka wa kwanza au baadaye, mtoto huwa na uhusiano wa karibu na mtu anayemlea, hasa mama yake. Mtoto anapokuwa na uhusiano huo mzuri, anapatana na watu wengine kuliko watoto ambao hawana uhusiano mzuri na wazazi wao. Uhusiano huo unapaswa kusitawishwa kabla mtoto hajafikia umri wa miaka mitatu.
Ni nini kinachoweza kutukia mtoto anapopuuzwa wakati huo ambapo akili yake inaweza kuathiriwa kwa urahisi? Martha Farrell Erickson aliyewachunguza akina mama 267 na watoto wao kwa miaka zaidi ya 20, anasema: “Mtoto anapopuuzwa, pole kwa pole yeye hukosa uchangamfu na hatimaye anashindwa kuchangamana na wengine au kujifunza mambo mengine.”
-