-
Kukua Pamoja Katika UpendoMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Sura ya 19
Kukua Pamoja Katika Upendo
WAKATI walipoandikia Wakristo wenzao, mitume wa Yesu Kristo walitaja uhitaji wa watu mmoja-mmoja kukua si katika ujuzi sahihi tu bali pia katika upendo. Msingi wa jambo hilo ulikuwa ule upendo ulioonyeshwa na Mungu mwenyewe na ule upendo wa kujidhabihu wa Kristo, ambaye walijitahidi kufuata hatua zake. (Yn. 13:34, 35; Efe. 4:15, 16; 5:1, 2; Flp. 1:9; 1 Yoh. 4:7-10) Walikuwa udugu, na waliposaidiana mmoja na mwenzake, vifungo vya upendo vilipata kuwa vyenye nguvu hata zaidi.
Wakati njaa ilipotokeza magumu ya kiuchumi kwa akina ndugu katika Yudea, Wakristo katika Siria na katika Ugiriki walishiriki mali zao ili kuwasaidia. (Mdo. 11:27-30; Rum. 15:26) Wakati baadhi yao waliponyanyaswa, mateso waliyopata yalihisiwa sana na Wakristo wengine, nao walitafuta kutoa usaidizi.—1 Kor. 12:26; Ebr. 13:3.
-
-
Kukua Pamoja Katika UpendoMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Msaada Wenye Upendo Katika Makutaniko ya Mahali
Miongoni mwa Mashahidi wa Yehova, utunzaji wa mayatima na wajane kutanikoni, pamoja na waaminifu wowote wapatwao na msiba mkali, huonwa kuwa sehemu ya ibada yao. (Yak. 1:27; 2:15-17; 1 Yoh. 3:17, 18)
-
-
Kukua Pamoja Katika UpendoMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Katika makutaniko zaidi ya 69,000 ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote, mahitaji ya pekee ambayo hutokea kwa sababu ya uzee na udhaifu wa watu mmoja-mmoja hushughulikiwa kwa kawaida na watu mmoja-mmoja. Kama inavyoonyeshwa kwenye 1 Timotheo 5:4, 8, daraka hilo hukalia kwanza kabisa kila Mkristo kutunza wale wa nyumba yake mwenyewe. Watoto, wajukuu, au wengine wa jamaa ya karibu huonyesha upendo wa Kikristo kwa kuandaa usaidizi kwa wazee-wazee na wenye udhaifu. Makutaniko ya Mashahidi wa Yehova hayadhoofishi hisi hii ya kuwa na daraka kwa kujitwalia wajibu mbalimbali wa familia. Hata hivyo, ikiwa hakuna washiriki wa familia wa karibu, au ikiwa wale wenye daraka hawawezi hata kidogo kubeba mzigo huo peke yao, wengine katika kutaniko huja kuwasaidia kwa upendo. Ikihitajiwa, kutaniko kwa ujumla laweza kufanya uandalizi wa usaidizi fulani kwa ndugu au dada mwenye uhitaji ambaye ana rekodi ndefu ya utumishi wa uaminifu.—1 Tim. 5:3-10.
Kushughulikia mahitaji hayo hakuachiwi nasibu. Kwenye vipindi vya Shule ya Huduma ya Ufalme, ambayo wazee wamehudhuria kwa kurudiarudia tangu 1959, wajibu wao mbele za Mungu kuhusiana na jambo hilo wakiwa wachungaji wa kundi umefikiriwa kipekee mara nyingi. (Ebr. 13:1, 16) Si kwamba hawakujua uhitaji huo kabla ya hapo. Kwa kielelezo, katika 1911, msaada wa vitu vya kimwili uliandaliwa na Kutaniko la Oldham katika Lancashire, Uingereza, kwa wale miongoni mwao waliokuwa wakikabili matatizo makali ya kiuchumi. Hata hivyo, tangu hapo tengenezo la duniani pote limekua, idadi ya wale wenye kupatwa na matatizo makali imeongezeka, na Mashahidi wa Yehova wamezidi kujua juu ya yale ambayo Biblia huonyesha wapaswa kufanya katika hali hizo. Hasa katika miaka ya majuzi, madaraka ya kila Mkristo kuelekea wale miongoni mwao wenye mahitaji ya pekee—wazee-wazee, wenye udhaifu, familia zenye mzazi mmoja, na wale walio na magumu ya kiuchumi—yamezungumzwa na makutaniko yote kwenye mikutano yao.a
Hangaikio ambalo Mashahidi mmoja-mmoja huonyesha kwa wengine huwa zaidi ya kusema, “mkaote moto na kushiba.” Wao binafsi huonyesha hangaikio lenye upendo. (Yak. 2:15, 16)
-