-
Kukua Pamoja Katika UpendoMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kuongezea kutunza mahitaji ya kimwili, Mashahidi wa Yehova hutoa uangalifu wa pekee kwa mahitaji ya kiroho ya ndugu zao katika maeneo yenye msiba. Mipango hufanywa vivyo hivyo upesi kwa kadiri iwezekanayo ili mikutano ya kutaniko ianze tena. Katika Ugiriki, katika 1986, hema kubwa ilihitajiwa nje ya jiji la Kalamata litumiwe kama Jumba la Ufalme, na mengine madogo kwenye sehemu mbalimbali kwa ajili ya Mafunzo ya Kitabu ya Kutaniko katikati ya juma. Vivyo hivyo, baada ya mahitaji ya kimwili ya waokokaji wa poromoko la tope lenye kuharibu sana katika Armero, Kolombia, katika 1985, yalipokuwa yameshughulikiwa, fedha zilizobaki zilitumiwa kujenga Majumba ya Ufalme mapya kwa ajili ya makutaniko matatu katika eneo hilo.
-
-
Kukua Pamoja Katika UpendoMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 314]
Jitihada za kutoa kitulizo za Mashahidi hutia ndani kujengana kiroho. Katika Kalamata, Ugiriki, na pia nje ya jiji, mahema yalisimamishwa haraka kwa ajili ya mikutano
-