Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)
    2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
    • Ofisi za Tawi za Ulaya Zasaidia Nyakati za Shida

      Maeneo mengi ya Kongo yamekumbwa na vita tangu mwaka wa 1996, na watu wengi wamekuwa wakimbizi. Maelfu ya akina ndugu kutoka Kongo walikimbilia kambi za wakimbizi nchini Tanzania na Zambia. Majeshi ya waasi yalipozidi kuteka maeneo mengi ya Kongo, ikawa vigumu zaidi kwa ofisi ya tawi kuwatunza na kuwasiliana na ndugu wanaoishi kwenye maeneo ya waasi. Halmashauri za kutoa misaada ziliundwa katika majiji makubwa ili kugawa misaada. Familia ya Betheli ilionyesha roho ya kujitoa na kujidhabihu kwa kufanya kazi hadi usiku wa manane ili kusaidia kugawa misaada. Mashahidi wa Yehova nchini Ubelgiji, Ufaransa, na Uswisi walisafirisha kwa ndege tani nyingi za chakula, mavazi, dawa, majozi 18,500 ya viatu, na mablangeti 1,000. Kazi ya kutoa misaada ingali inaendelea na inapunguza matatizo. Mashahidi wa Yehova na watu wengine wanafaidika.

      Mnamo Oktoba 1998, makala moja katika gazeti fulani la Kinshasa ilisema hivi: “Makutaniko ya Kikristo ya Mashahidi wa Yehova katika nchi mbalimbali za Ulaya yamekusanya zaidi ya tani 400 za bidhaa za misaada na kuzituma Kongo-Kinshasa na Kongo-Brazzaville. Watu ambao wamejitolea kutoka Uingereza, Ufaransa, na Uswisi, tayari wamepeleka jijini Kinshasa tani 37 za mchele, maziwa ya unga, maharagwe, na biskuti zenye vitamini. Zilisafirishwa kwa ndege kutoka Ostend, Ubelgiji, zikafika kwenye ofisi kuu ya Mashahidi wa Yehova huko Kinshasa. Ndege nyingine . . . itafika . . . ikiwa na tani 38 za chakula.

      “Inapendeza kwamba Mashahidi wa Yehova wamewasaidia wakimbizi katika Afrika Mashariki tangu yale mauaji makubwa yaliyotukia nchini Rwanda. . . . Msemaji wa Mashahidi wa Yehova alitangaza kwamba misaada hiyo ya hiari yenye uzito wa zaidi ya tani 200, kutia ndani chakula na dawa, ilisaidia kupambana na ugonjwa wa kipindupindu. Wakati huo, Mashahidi wa Yehova kutoka Ufaransa na Ubelgiji waliunda vikundi kadhaa vya kuwasaidia wakimbizi kambini. Alitaja pia misaada ambayo Mashahidi wa Yehova wamewapa maskini huko Ulaya Mashariki na Bosnia.”

  • Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)
    2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
    • [Picha katika ukurasa wa 244, 245]

      Misaada iliwasili kutoka Ulaya na kugawiwa wenye uhitaji mwaka wa 1998

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki