-
DiniKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Ni nani aliyeanzisha mvurugo huo wa kidini? Biblia inamtambulisha Shetani Ibilisi kuwa “mungu wa mfumo huu wa mambo.” (2 Kor. 4:4) Inatuonya kwamba “vitu ambavyo mataifa huvitoa dhabihu wao huvitoa dhabihu kwa roho waovu, na si kwa Mungu.” (1 Kor. 10:20) Basi ni jambo muhimu kama nini kuhakikisha kwamba tunamwabudu Mungu wa kweli, yule Muumba wa dunia na mbingu, na kwamba ibada yetu inampendeza!
-
-
DiniKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
2 Kor. 11:14, 15: “Shetani mwenyewe huendelea kujigeuza mwenyewe kuwa malaika wa nuru. Kwa hiyo si jambo kubwa kama wahudumu wake wakiendelea pia kujigeuza wenyewe kuwa wahudumu wa uadilifu.” (Hapa tunatahadharishwa kwamba si kila kitu kinachotoka kwa Shetani kitakachoonekana kuwa kibaya sana. Moja ya njia zake kuu za kuwadanganya wanadamu ni dini za uwongo, naye huzifanya baadhi ya dini hizo zionekane kuwa zenye uadilifu.)
-