-
Unapaswa Kuwa Mwaminifu kwa Nani?Mnara wa Mlinzi—2002 | Agosti 15
-
-
Uaminifu Wajaribiwa
Mwanamke mmoja aliyekulia nchini Zambia asema: “Nilipendezwa na dini tangu nilipokuwa mchanga. Tulisali kila siku tukiwa familia kwenye chumba kitakatifu, tukaadhimisha sikukuu za kidini, na kuhudhuria ibada kwa ukawaida kwenye hekalu. Dini na ibada yangu ilihusiana sana na utamaduni, jumuiya, na familia yangu.”
Hata hivyo, alipokuwa tineja, alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova na muda mfupi baadaye akaamua kubadili dini yake. Je, huo ulikuwa ukosefu wa uaminifu?
-
-
Unapaswa Kuwa Mwaminifu kwa Nani?Mnara wa Mlinzi—2002 | Agosti 15
-
-
Utajibu maswali hayo kupatana na maoni yako. Mwanamke aliyetangulia kutajwa anasema: “Katika jumuiya yetu, kubadili dini huonwa kuwa jambo lenye kuaibisha; ni kukosa uaminifu, kusaliti familia na jamii.”
-
-
Unapaswa Kuwa Mwaminifu kwa Nani?Mnara wa Mlinzi—2002 | Agosti 15
-
-
Uaminifu kwa Yehova unategemea upendo. Sifa hiyo huchochea mtu apende mambo ambayo Yehova hupenda na kuchukia mambo maovu ambayo Yehova huchukia. (Zaburi 97:10) Kwa kuwa upendo ndiyo sifa kuu ya Yehova, uaminifu kwa Mungu humzuia mtu asiwatendee wengine kwa njia isiyo ya upendo. (1 Yohana 4:8) Kwa hiyo iwapo mtu anabadili imani yake ya kidini ili kuonyesha uaminifu kwa Mungu, hiyo haimaanishi kwamba hapendi familia yake.
Uaminifu kwa Mungu Hunufaisha
Mwanamke aliyetangulia kutajwa asema hivi kuhusu hatua alizochukua: “Kwa kujifunza Biblia, nilipata kumjua Yehova kuwa Mungu wa kweli, na kusitawisha uhusiano wa karibu pamoja naye. Yehova si kama miungu niliyoabudu hapo awali; yeye husawazisha upendo, haki, hekima, na nguvu zake. Kwa kuwa Yehova hutaka ujitoaji usiohusisha wengine, nililazimika kuacha kuabudu miungu mingine.
“Mara kwa mara wazazi wangu waliniambia kwamba nimewakasirisha sana na kwamba ninawakatisha tamaa. Jambo hilo lilikuwa gumu sana kwangu kwa kuwa ninatamani sana kupata kibali cha wazazi. Lakini nilipozidi kuongeza ujuzi wa kweli ya Biblia hatua kwa hatua, nilijua uamuzi ambao ningefanya. Singeweza kumkataa Yehova.
“Kuamua kuwa mwaminifu kwa Yehova badala ya kuwa mwaminifu kwa mapokeo ya kidini hakumaanishi kwamba mimi si mwaminifu kwa familia yangu. Mimi hujitahidi kuwaonyesha kwa maneno na matendo kwamba ninaelewa jinsi wanavyohisi. Lakini nisipokuwa mwaminifu kwa Yehova, basi huenda nikazuia familia yetu wasipate kumjua, na kufanya hivyo kungekuwa kukosa uaminifu kabisa.”
-