Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Likiwa tokeo la kuhubiri kwa jamii ya Yohana, hesabu kubwa za watu zimepitia ule mlango uliofunguliwa wakaingia ndani ya utumishi wa Ufalme.b

  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • b Gazeti Mnara wa Mlinzi linalotangazwa na jamii ya Yohana, limeendelea kukazia umuhimu wa kutwaa nafasi hii na kushiriki kikamilifu kadiri iwezekanavyo katika kazi ya kuhubiri; mathalani, ona makala “Wote na Wautangaze Utukufu wa Yehova” na “Sauti Yao Ilifika Katika Dunia Yote” katika toleo la Januari 1, 2004. Katika toleo la Juni 1, 2004, katika makala “Wanaomtukuza Mungu Hubarikiwa,” mkazo uliwekwa juu ya kuingia “mlango uliofunguliwa” ndani ya utumishi wa wakati wote. Kulikuwako kilele cha mapainia 1,093,552 walioripoti utumishi kama huo katika pindi ya mwezi mmoja katika 2005.

  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 9. Ni jinsi gani Yesu anatumia ufunguo wa Daudi kufungua na kufunga?

      9 Kwa wakati uliopo Yesu angetumia ule ufunguo wa Daudi, akifungua nafasi na mapendeleo yanayohusiana na Ufalme wa Mungu. Kupitia Yesu, Yehova angekomboa Wakristo wapakwa-mafuta duniani “kutoka mamlaka ya lile giza,” na kuwahamisha awaingize “ndani ya ufalme wa Mwana wa upendo wake.” (Wakolosai 1:13, 14, NW) Ufunguo ule ungetumiwa pia kuzuia wasipate mapendeleo hayo wowote ambao wangethibitika kuwa wasioaminika. (2 Timotheo 2:12, 13) Kwa kuwa mrithi huyu wa kudumu wa ufalme wa Daudi ana utegemezo wa Yehova, hakuna kiumbe anayeweza kumzuia asitimize wajibu huo ulio mwingi.—Linga Mathayo 28:18-20.

      10. Ni kitia-moyo gani anachotoa Yesu kwa kundi katika Filadelfia?

      10 Yakija kutoka chanzo kama hicho chenye mamlaka, maneno ya Yesu kwa Wakristo katika Filadelfia lazima yawe yenye kufariji hasa! Yeye anawasifu, akisema: “Mimi najua matendo yako—tazama! mimi nimeweka mbele yako mlango uliofunguliwa, ambao hakuna mmoja awezaye kufunga—kwamba wewe una nguvu chache, na wewe ulishika neno langu na hukuthibitika kuwa bandia kwa jina langu.” (Ufunuo 3:8, NW) Kundi limekuwa lenye kutenda, nao mlango umefunguliwa mbele yalo—bila shaka mlango wa nafasi ya utumishi wa kihuduma. (Linga 1 Wakorintho 16:9; 2 Wakorintho 2:12.) Kwa hiyo, Yesu analitia moyo kundi litumie kwa faida kamili ile nafasi ya kuhubiri. Wao wamevumilia na kuonyesha kwamba wana nguvu za kutosha, kwa msaada wa roho ya Mungu, kuendelea kufanya “matendo” zaidi katika utumishi wa Yehova. (2 Wakorintho 12:10; Zekaria 4:6) Wametii amri za Yesu nao hawakumkana Kristo ama kwa neno ama kwa tendo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki