Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uhudumiaji wa Kitheokrasi Katika Enzi ya Ukristo
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Mei 15
    • Tegemeo kwa Ajili ya Israeli wa Mungu

      10. Ni nani ambao wamejiunga na watiwa-mafuta katika utumishi wa Yehova siku hizi za mwisho, na hilo lilitolewaje unabii?

      10 Huko nyuma mwaka wa 1884 karibu wote walioshirikishwa na Israeli wa Mungu walikuwa Wakristo watiwa-mafuta. Hata hivyo, hatua kwa hatua, kikundi kingine kikaanza kuonekana, na mwaka wa 1935 kikundi hicho kilitambuliwa kuwa “umati mkubwa” wa Ufunuo sura ya 7. Wakiwa na tumaini la kidunia, hao wawakilisha “vitu vilivyo duniani” ambavyo Yehova akusudia kukusanya pamoja katika Kristo. (Waefeso 1:10) Wao wawakilisha “kondoo wengine” wa mfano wa Yesu wa mazizi ya kondoo. (Yohana 10:16) Tangu mwaka wa 1935, kondoo wengine wamemiminika katika tengenezo la Yehova. Wamekuja ‘wakiruka kama wingu, kama njiwa waendao madirishani kwao.’ (Isaya 60:8) Kwa sababu ya ongezeko katika umati mkubwa na upunguo katika jamii ya watiwa-mafuta huku wengi wao wamalizapo mwendo wao wa kidunia katika kifo, kondoo wengine wenye sifa ya kustahili wamepata kuwa na madaraka zaidi katika utendaji mbalimbali wa Kikristo. Katika njia zipi?

      11. Ni mapendeleo gani yamepewa kondoo wengine, ambayo hapo awali yalikuwa ya Wakristo watiwa-mafuta peke yao?

      11 Sikuzote kutangaza kotekote sifa bora kabisa za Yehova kumekuwa wajibu wa pekee wa “taifa takatifu” la Mungu. Paulo alisema juu ya wajibu huo kuwa dhabihu ya hekalu, na wale ambao wangekuwa “ukuhani wa kifalme,” Yesu aliwapa utume wa kuhubiri na kufundisha. (Kutoka 19:5, 6; 1 Petro 2:4, 9; Mathayo 24:14; 28:19, 20; Waebrania 13:15, 16) Hata hivyo, toleo la Agosti 1, 1932, la Mnara wa Mlinzi (la Kiingereza), liliwatia moyo hususani wale waliofananishwa na Yonadabu washiriki katika utendaji huo. Kwa kweli, wengi wa hao kondoo wengine walikuwa tayari wakifanya hivyo. Leo, karibu kazi yote ya kuhubiri inafanywa na kondoo wengine ikiwa sehemu ya maana ya ‘kumtolea kwao Mungu utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake.’ (Ufunuo 7:15) Vivyo hivyo, katika sehemu ya mapema ya historia ya kisasa ya watu wa Yehova, wazee wa kutaniko walikuwa Wakristo watiwa-mafuta, “nyota” katika mkono wa kuume wa Yesu Kristo. (Ufunuo 1:16, 20) Lakini toleo la Mei 1, 1937, la Mnara wa Mlinzi (la Kiingereza), lilitangaza kwamba kondoo wengine wenye sifa ya kustahili wangeweza kuwa watumishi wa kampuni (waangalizi-wasimamizi). Hata ikiwa wanaume watiwa-mafuta walipatikana, kondoo wengine wangeweza kutumiwa ikiwa wanaume watiwa-mafuta wasingeweza kuchukua daraka hilo. Leo, karibu wazee wote wa kutaniko ni kondoo wengine.

      12. Kuna vielelezo gani vya Kimaandiko vionyeshavyo kwamba kondoo wengine wenye sifa ya kustahili wangepokea madaraka mazito ya kitengenezo?

      12 Je, ni kosa kuwapa kondoo wengine madaraka hayo mazito? La, hilo lafuata kielelezo cha kihistoria. Baadhi ya wageuzwa-imani wa kigeni (wakazi wa kutoka nchi nyingine) walikuwa na vyeo vya juu katika Israeli la kale. (2 Samweli 23:37, 39; Yeremia 38:7-9) Baada ya uhamisho wa Babiloni, Wanethini (watumishi wa hekaluni wasio Waisraeli) wenye sifa ya kustahili walipewa mapendeleo ya utumishi wa hekalu ambayo awali yalikuwa ya Walawi peke yao. (Ezra 8:15-20; Nehemia 7:60) Kwa kuongezea, Musa, aliyeonwa pamoja na Yesu katika ono la mgeuko-umbo, alikubali lile shauri zuri la Mmidiani Yethro. Baadaye, alimwomba Hobabu, mwana wa Yethro, awaongoze kupitia jangwa.—Kutoka 18:5, 17-24; Hesabu 10:29.

      13. Watiwa-mafuta wamekuwa wakiiga kielelezo kipi chema katika kuwakabidhi madaraka kwa unyenyekevu kondoo wengine wenye sifa ya kustahili?

      13 Kuelekea mwisho wa ile miaka 40 jangwani, Musa, akijua kwamba asingeingia Bara Lililoahidiwa, alisali kwamba Yehova angeandaa mwandamizi. (Hesabu 27:15-17) Yehova alimwambia Musa ampe Yoshua utume mbele ya watu wote, na Musa akafanya hivyo, hata ingawa alikuwa bado mwenye nguvu kimwili na hakuacha kutumikia Israeli papo hapo. (Kumbukumbu la Torati 3:28; 34:5-7, 9) Wakiwa na mtazamo huohuo wenye unyenyekevu, watiwa-mafuta tayari wamekuwa wakiwapa mapendeleo zaidi wanaume wenye sifa ya kustahili kutoka miongoni mwa kondoo wengine.

      14. Ni unabii gani mbalimbali uonyeshao kwamba kondoo wengine wangepata madaraka zaidi katika tengenezo?

      14 Kuwapa kondoo wengine madaraka zaidi katika tengenezo ni habari inayozungumziwa katika unabii pia. Zekaria alitabiri kwamba Mfilisti asiye Mwisraeli angekuwa “kama shehe katika Yuda.” (Zekaria 9:6, 7, NW) Mashehe walikuwa wakuu wa makabila, kwa hiyo Zekaria alikuwa akisema kwamba mtu ambaye zamani alikuwa adui wa Israeli angefuata ibada ya kweli na kupata kuwa kama mkuu wa makabila katika Bara Lililoahidiwa. Zaidi, alipokuwa akisema na Israeli wa Mungu, Yehova alisema hivi: “Wageni watasimama na kulisha makundi yenu, na watu wa kabila nyingine watakuwa wakulima wenu, na watunzaji wa mizabibu yenu. Bali ninyi mtaitwa makuhani wa BWANA; watu watawaiteni wahudumu wa Mungu wetu.” (Isaya 61:5, 6) Hao “wageni” na “watu wa kabila nyingine” ni kondoo wengine. Hawa wamekabidhiwa madaraka ili waweze kufanya kazi nyingi zaidi huku mabaki watiwa-mafuta wanaozeeka wamalizapo mwendo wao wa kidunia na kwenda kutumikia kwa maana kamili wakiwa “makuhani wa [kimbingu] wa BWANA,” wakizunguka kiti cha ufalme cha Yehova chenye fahari wakiwa “wahudumu wa Mungu wetu.”—1 Wakorintho 15:50-57; Ufunuo 4:4, 9-11; 5:9, 10.

  • Uhudumiaji wa Kitheokrasi Katika Enzi ya Ukristo
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Mei 15
    • 18. (a) Hali ni nini kwa habari ya ‘kukusanya pamoja katika Kristo vitu vilivyomo katika mbingu’? (b) Twaweza kusema nini juu ya ‘kukusanya pamoja katika Kristo vitu vilivyo duniani’?

      18 Kwa kupatana na uhudumiaji wake wa vitu, Yehova anasonga kwa mwendeleo “kukusanya tena pamoja vitu vyote katika Kristo.” Kwa habari ya “vitu vilivyomo katika mbingu,” kusudi lake lakaribia ukamilisho. Kuunganishwa kwa Yesu pamoja na wale 144,000 wote mbinguni kwa ajili ya “ndoa ya Mwana-Kondoo” kuko karibu. Kwa sababu hiyo, ndugu wengi zaidi walio wakomavu, ambao wametumikia muda mrefu kati ya wale kondoo wengine, wanaowakilisha “vitu vilivyo duniani,” wamekabidhiwa madaraka mazito zaidi katika kuwategemeza ndugu zao watiwa-mafuta. Twaishi katika nyakati zenye kusisimua kama nini! Kuona kusudi la Yehova likisonga hadi kwenye utimizo walo kunasisimua kama nini! (Waefeso 1:9, 10; 3:10-12; Ufunuo 14:1; 19:7, 9) Na kondoo wengine wanashangilia kama nini kuwategemeza ndugu zao watiwa-mafuta huku vikundi hivyo viwili vitumikiapo pamoja vikiwa “kundi moja” chini ya “mchungaji mmoja” katika ujitiisho kwa Mfalme, Yesu Kristo, na kwa utukufu wa mwenye Enzi Kuu mkubwa wa Ulimwengu Wote Mzima, Yehova Mungu!—Yohana 10:16; Wafilipi 2:9-11.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki