Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Jina Jipya”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 12. (a) Yehova amejulishaje wazi kwamba Wakristo watiwa-mafuta ni sehemu ya tengenezo ambalo limeungana naye katika ndoa? (b) Shughuli za Yehova pamoja na watu wake zinatoaje kielelezo cha ndoa ya hali ya juu leo? (Ona sanduku katika ukurasa wa 342.)

      12 Kwa njia ya ulinganifu, tangu mwaka wa 1919 watoto wa Sayuni wa kimbingu wamemiliki nchi yao, miliki yao ya kiroho, iliyo na jina la kiunabii “Ameolewa.” Utendaji wao wa Kikristo katika nchi hiyo umeonyesha wazi kwamba Wakristo hawa watiwa-mafuta ni “watu kwa ajili ya jina lake” Yehova. (Matendo 15:14) Kuzaa kwao matunda ya Ufalme na kutangaza jina la Yehova kumeonyesha wazi kwamba Yehova huwafurahia sana Wakristo hawa. Yeye ameonyesha wazi kwamba wao ni sehemu ya tengenezo ambalo limeungana naye katika umoja usiovunjika. Kwa kuwatia mafuta Wakristo hawa kwa roho takatifu, kuwakomboa watoke katika utekwa wa kiroho, na kuwatumia ili wahubirie jamii yote ya wanadamu tumaini la Ufalme, Yehova ameonyesha kwamba anawashangilia kwa shangwe ya bwana-arusi kumwelekea bibi-arusi.—Yeremia 32:41.

  • “Jina Jipya”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 11. Wayahudi wanamwoaje mama yao?

      11 Yehova anazidi kukazia hali mpya ya kukubalika kwa watu wake, anapotangaza hivi: “Kama vile kijana amwoavyo mwanamwali, ndivyo wana wako watakavyokuoa wewe; na kama vile bwana arusi amafurahiavyo bibi arusi, ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.” (Isaya 62:5)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki