Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uadilifu Wachipuka Katika Sayuni
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 5. Ni nani ambao wamekuwa wakihubiri zile habari njema kwa muda wa miaka 2,000 hivi?

      5 Zaidi ya hilo, Yesu aliwafundisha wafuasi wake kuwa waeneza-injili, au wahubiri wa zile habari njema. Kwenye Pentekoste 33 W.K., karibu watu 120 kati ya wahubiri hao walitiwa mafuta kwa roho takatifu wakawa wana wa kiroho wa Mungu. (Matendo 2:1-4, 14-42; Waroma 8:14-16) Wao pia walipewa utume wa kuwaeleza watu watiifu na waliovunjika moyo kuhusu zile habari njema. Hao 120 walikuwa wa kwanza miongoni mwa watu 144,000 kutiwa mafuta kwa njia hiyo. Leo wale walio wa mwisho katika kikundi hiki wangali wakiendelea na utendaji wao duniani. Kwa hiyo, kwa karibu miaka 2,000, wafuasi watiwa-mafuta wa Yesu wamekuwa wakitoa ushahidi “juu ya toba kuelekea Mungu na imani katika Bwana wetu Yesu.”—Matendo 20:21.

  • Uadilifu Wachipuka Katika Sayuni
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Leo, mamilioni walionaswa katika mtego wa desturi za kipagani za Jumuiya ya Wakristo na mapokeo yanayomvunjia Mungu heshima ‘wanaugua na kulia’ kwa sababu ya machukizo yanayofanywa katika mfumo huo wa kidini. (Ezekieli 9:4) Wale wanaoziitikia habari njema wanakombolewa watoke katika hali hiyo ya kusikitisha. (Mathayo 9:35-38) Macho yao ya ufahamu yanafunguliwa wazi wanapojifunza kumwabudu Yehova “kwa roho na kweli.”—Yohana 4:24.

      7, 8. (a) Kuna miaka gani miwili ‘ya nia njema’? (b) ‘Siku za kisasi’ cha Yehova ni zipi?

      7 Kuna wakati hususa uliowekwa ili habari njema zihubiriwe. Yesu na wafuasi wake walipewa utume wa “kutangaza mwaka wa BWANA uliokubaliwa [“mwaka wa nia njema,” “NW”], na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao.” (Isaya 61:2) Mwaka ni muda mrefu, lakini una mwanzo na mwisho. “Mwaka wa nia njema” wa Yehova ni kile kipindi ambacho yeye huwapa watu watiifu nafasi ya kuitikia anapowatangazia uhuru.

  • Uadilifu Wachipuka Katika Sayuni
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sisi leo tunaishi katika mwaka mwingine wa nia njema, ulioanza wakati Ufalme wa Mungu uliposimamishwa katika mbingu mwaka wa 1914. Mwaka huu wa nia njema utamalizika na siku nyingine ya kisasi yenye kuenea sana, wakati Yehova atakapoleta uharibifu wa mfumo mzima wa mambo ya ulimwengu huu kwenye “dhiki kubwa.”—Mathayo 24:21.

      9. Ni nani leo wanaofaidika na mwaka wa Yehova wa nia njema?

      9 Ni nani leo wanaofaidika na mwaka wa Mungu wa nia njema? Ni wale wanaoukubali ujumbe, wanaotii, na kuunga mkono kwa bidii kazi ya kutangaza Ufalme wa Mungu katika “mataifa yote.” (Marko 13:10) Watu wa jinsi hiyo wanaona kuwa zile habari njema huleta faraja halisi. Hata hivyo, wale wanaoukataa ujumbe, na kukataa kuutumia vizuri mwaka wa nia njema ya Yehova maadamu ungali upo, watakabiliana na siku yake ya kisasi hivi karibuni.—2 Wathesalonike 1:6-9.

  • Uadilifu Wachipuka Katika Sayuni
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Hivyo, Isaya anatimiza utume wake wa kiunabii, yaani, “kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti [“mikubwa,” “NW”] ya haki [“uadilifu,” “NW”], iliyopandwa na BWANA, ili atukuzwe.”—Isaya 61:3.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki