-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
3. Maneno ya kiunabii ya Isaya sura ya 61 yanatimizwa kwa njia zipi?
3 Kurudishwa huku kunatabiriwa katika Isaya sura ya 61. Hata hivyo, ingawa ni wazi kwamba unabii huo ulitimizwa mwaka wa 537 K.W.K., unatimizwa kwa njia kubwa zaidi baadaye. Utimizo ulio na mambo mengi zaidi unahusu Yesu na wafuasi wake katika karne ya kwanza na watu wa Yehova katika nyakati za kisasa. Basi, maneno hayo yaliyopuliziwa ni muhimu sana!
“Mwaka wa Nia Njema”
4. Katika utimizo wa kwanza wa Isaya 61:1, ni nani anayepewa utume wa kuhubiri habari njema, na ni nani anayepewa utume huo katika utimizo wa pili?
4 Isaya anaandika hivi: “Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu BWANA amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.” (Isaya 61:1) Ni nani aliyepewa utume wa kuhubiri habari njema?
-
-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
5. Ni nani ambao wamekuwa wakihubiri zile habari njema kwa muda wa miaka 2,000 hivi?
5 Zaidi ya hilo, Yesu aliwafundisha wafuasi wake kuwa waeneza-injili, au wahubiri wa zile habari njema. Kwenye Pentekoste 33 W.K., karibu watu 120 kati ya wahubiri hao walitiwa mafuta kwa roho takatifu wakawa wana wa kiroho wa Mungu. (Matendo 2:1-4, 14-42; Waroma 8:14-16) Wao pia walipewa utume wa kuwaeleza watu watiifu na waliovunjika moyo kuhusu zile habari njema. Hao 120 walikuwa wa kwanza miongoni mwa watu 144,000 kutiwa mafuta kwa njia hiyo. Leo wale walio wa mwisho katika kikundi hiki wangali wakiendelea na utendaji wao duniani. Kwa hiyo, kwa karibu miaka 2,000, wafuasi watiwa-mafuta wa Yesu wamekuwa wakitoa ushahidi “juu ya toba kuelekea Mungu na imani katika Bwana wetu Yesu.”—Matendo 20:21.
-