-
Je, Una Sababu ya Kuamini Kwamba Kutakuwa na Paradiso?Mnara wa Mlinzi—2004 | Oktoba 15
-
-
7. Ni nini ambacho kingetukia baada ya ile miaka 70 ya ukiwa?
7 Hilo lilitukia baada ya ile miaka 70. Hali ziliboreka kwa sababu ya baraka za Mungu. Wazia jambo hili: “Nyika na nchi isiyo na maji itafurahi; na nchi tambarare ya jangwani itakuwa na shangwe na kuchanua maua kama zafarani. Itachanua maua bila shaka, nayo itashangilia kwa shangwe na kwa kilio cha furaha. . . . Kilema atapanda juu kama vile paa anavyofanya, na ulimi wa bubu utapaaza sauti kwa furaha. Kwa maana maji yatakuwa yamebubujika katika nyika, na mito katika nchi tambarare ya jangwani. Na nchi iliyokaushwa na joto itakuwa kama dimbwi lenye matete, na nchi yenye kiu kama mabubujiko ya maji. Katika makao ya mbwa-mwitu, mahali pao pa kupumzika, patakuwa na majani mabichi na matete na mimea ya mafunjo.”—Isaya 35:1-7.
Watu Waliorudishwa na Kubadilika
8. Tunajuaje kwamba Isaya sura ya 35 iliwahusu watu?
8 Hilo lilikuwa badiliko lililoje! Nchi yabadilika kutoka hali ya ukiwa na kuwa paradiso. Hata hivyo, unabii huo na pia unabii mwingine wenye kutegemeka ulionyesha kwamba watu wangebadilika, kama vile nchi iliyo ukiwa inavyoweza kubadilika na kuwa yenye kuzaa. Kwa nini tuseme hivyo? Isaya alikuwa anakazia fikira wale “hasa waliokombolewa na Yehova,” ambao wangerudi katika nchi yao “kwa vigelegele vya shangwe” na kupata “furaha na kushangilia.” (Isaya 35:10) Unabii huo ulihusu watu, bali si udongo halisi. Isitoshe, katika sehemu nyingine Isaya alitabiri hivi kuhusu watu waliorudishwa Sayuni: ‘Nao wataitwa miti mikubwa ya uadilifu, bustani ya Yehova. Kwa maana kama vile dunia inavyotoa chipukizi lake, ndivyo Yehova atakavyotoa chipukizi la uadilifu na la sifa mbele ya mataifa yote.’ Isaya pia alisema hivi kuhusu watu wa Mungu: “Yehova hatakosa kukuongoza sikuzote . . . , naye ataitia nguvu mifupa yako; nawe utakuwa kama bustani iliyonyweshwa maji vizuri.” (Isaya 58:11; 61:3, 11; Yeremia 31:10-12) Kwa hiyo, kama vile ambavyo hali za mazingira ya nchi halisi zingeboreka, ndivyo ambavyo Wayahudi waliorudishwa wangebadilika.
-
-
Je, Una Sababu ya Kuamini Kwamba Kutakuwa na Paradiso?Mnara wa Mlinzi—2004 | Oktoba 15
-
-
Hata hivyo, fikiria paradiso ya kiroho tunayofurahia sasa. Tunapoilinganisha na hali mbaya tulimokuwa zamani, tumeponywa kiroho. Linganisha njaa tuliyokuwa nayo zamani na chakula cha kiroho tunachofurahia sasa. Badala ya kupambana kana kwamba wako katika nchi kame ya kiroho, watu wa Mungu wana kibali chake na baraka zisizo na kifani. (Isaya 35:1, 7) Badala ya kupofushwa na giza zito la kiroho, tunaona nuru ya uhuru na ya kibali cha Mungu. Wengi ambao hawakuwa wamewahi kusikia unabii wa Biblia wamepata kusikia na kuelewa vile Maandiko yanavyosema. (Isaya 35:5) Kwa mfano, mamilioni ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote wamejifunza unabii wa Danieli, mstari kwa mstari. Kisha wakachunguza kwa makini kila sura ya kitabu cha Biblia cha Isaya. Chakula hicho cha kiroho chenye kuburudisha kinathibitisha kwamba tuko katika paradiso ya kiroho.
-
-
Je, Una Sababu ya Kuamini Kwamba Kutakuwa na Paradiso?Mnara wa Mlinzi—2004 | Oktoba 15
-
-
18. Ni lazima andiko la Isaya 35:2 liwe liliwapa Waisraeli waliokuwa uhamishoni wazo gani kuhusu jinsi Nchi ya Ahadi ingekuwa?
18 Nchi ya Ahadi ilikuwa yenye rutuba na yenye kuzaa sana hivi kwamba, kutaja tu maeneo fulani kulimkumbusha mtu hali za kiparadiso. Jambo hilo linaonekana wazi katika unabii wa Isaya sura ya 35, ambao ulitimizwa mara ya kwanza wakati Waisraeli waliporudi kutoka Babiloni. Isaya alitabiri hivi: “Itachanua maua bila shaka, nayo itashangilia kwa shangwe na kwa kilio cha furaha. Itapewa utukufu wa Lebanoni, fahari ya Karmeli na ya Sharoni. Kutakuwa na wale watakaouona utukufu wa Yehova, fahari ya Mungu wetu.” (Isaya 35:2) Bila shaka, kutajwa kwa maeneo ya Lebanoni, Karmeli, na Sharoni kulitokeza picha nzuri na yenye kuridhisha katika akili za Waisraeli.
19, 20. (a) Fafanua eneo la Sharoni la kale. (b) Ni katika njia gani tunaweza kuimarisha tumaini letu katika Paradiso?
19 Fikiria Sharoni, nchi tambarare iliyo kwenye ukingo wa bahari kati ya milima ya Samaria na Bahari Kuu, au Mediterania. (Ona picha kwenye ukurasa wa 10.) Nchi hiyo ilikuwa maarufu kwa kuwa ilikuwa nzuri na yenye kuzaa. Ilikuwa yenye maji mengi, na hivyo ilifaa kwa malisho ingawa ilikuwa na misitu ya mialoni pande za kaskazini. (1 Mambo ya Nyakati 27:29; Wimbo wa Sulemani 2:1; Isaya 65:10) Hivyo, andiko la Isaya 35:2 lilitabiri kuhusu kurudishwa na kuhusu nchi inayochanuka kwa fahari, na kuwa kama paradiso. Kupatana na maono ambayo Paulo aliona baadaye, unabii huo pia ulikuwa ukielekeza kwenye paradiso nzuri ya kiroho. Mwishowe, unabii huo pamoja na unabii mwingine mwingi huimarisha tumaini letu katika paradiso ya kidunia kwa ajili ya wanadamu.
-