-
Kumtambua Mjumbe wa Aina InayofaaMnara wa Mlinzi—1997 | Mei 1
-
-
Habari Njema ya Mjumbe kwa Ajili ya Sayuni!
16. Ni habari gani njema ingeweza kupigwa mbiu katika jiji lililofanywa ukiwa la Yerusalemu wakati Babiloni liliposhindwa?
16 Lakini kuna mengi zaidi. Isaya 52:7 hutuambia juu ya habari njema kwa ajili ya Yerusalemu: “Jinsi ilivyo mizuri juu ya milima miguu yake aletaye habari njema, yeye aitangazaye amani, aletaye habari njema ya mambo mema, yeye autangazaye wokovu, auambiaye Sayuni, Mungu wako anamiliki!” Wazia jinsi ilivyofurahisha kumwona mjumbe akikaribia Yerusalemu kutoka milimani! Lazima awe ana habari! Habari gani? Ni habari yenye kusisimua kwa ajili ya Sayuni. Habari ya amani, ndiyo, habari ya nia njema ya Mungu. Yerusalemu na hekalu lalo litajengwa upya! Na huyo mjumbe apiga mbiu akiwa na idili ya ushindi: “Mungu wako anamiliki!”
17, 18. Ushindi wa Sairasi dhidi ya Babiloni uliathirije jina la Yehova mwenyewe?
17 Yehova aliporuhusu Wababiloni kukipindua kiti chake cha ufalme cha kimfano, ambapo wafalme wa ukoo wa Daudi walikaa, huenda ikawa ilionekana kwamba Yeye hakuwa Mfalme tena. Marduki, mungu mkuu wa Babiloni, ndiye aliyeonekana kuwa mfalme badala yake. Lakini, Mungu wa Sayuni alipopindua Babiloni, alionyesha kuwa mwenye enzi kuu ya ulimwengu wote mzima—kwamba alikuwa Mfalme mkuu kupita wote. Na kukazia jambo hili la hakika, Yerusalemu, “mji wa Mfalme mkuu,” lilipasa kusimamishwa tena, pamoja na hekalu lalo. (Mathayo 5:35) Kwa habari ya mjumbe aliyeleta habari hizo njema, ingawa miguu yake ilikuwa na vumbi sana, ilikuwa michafu, na kuchubuka, machoni pa wapenda-Sayuni na Mungu wake, ilionekana, loo, mizuri saana!
18 Katika maana ya kiunabii, kuanguka kwa Babiloni kulimaanisha kwamba ufalme wa Mungu ulisimamishwa naye mchukuaji wa habari njema alikuwa mpiga-mbiu wa jambo hilo la hakika. Na zaidi, mpeleka-habari huyu wa kale, aliyetabiriwa kupitia Isaya, alifananisha mjumbe wa habari njema tukufu zaidi—tukufu zaidi kwa sababu ya yaliyomo yaliyo bora na kichwa chayo cha Ufalme, kukimaanisha mambo mazuri ajabu kwa ajili ya watu wote wa imani.
-
-
Kumtambua Mjumbe wa Aina InayofaaMnara wa Mlinzi—1997 | Mei 1
-
-
20. Isaya alitolea kiunabii Yerusalemu himizo gani lenye furaha?
20 Katika utekwa wa Babiloni, watu wa Mungu walikuwa wakiombolezea Sayuni. (Zaburi 137:1) Sasa wangeweza kushangilia. Isaya alihimiza hivi: “Pigeni kelele za furaha, imbeni pamoja, enyi mahali pa Yerusalemu palipokuwa ukiwa; kwa kuwa BWANA amewafariji watu wake, ameukomboa Yerusalemu. BWANA ameweka wazi mkono wake mtakatifu machoni pa mataifa yote; na ncha zote za dunia zitauona wokovu wa Mungu wetu.”—Isaya 52:9, 10.
21. Maneno ya Isaya 52:9, 10 yalitimizwaje kufuatia ushinde wa Babiloni?
21 Ndiyo, watu wa Yehova waliochaguliwa walikuwa na sababu kubwa ya kushangilia. Sasa walikuwa wakae tena katika sehemu zile zilizokuwa ukiwa wakati mmoja, wakizifanya ziwe kama bustani ya Edeni. Yehova alikuwa “ameweka wazi mkono wake,” kwa ajili yao. Alikunja mkono wa shati lake, kwa kusema kitamathali, ili aweze kufanya kazi ya kurudisha watu wake kwenye bara-pendwa la kwao. Hilo halikuwa tukio dogo, la kisiri katika historia. La, watu wote waliokuwa wakiishi wakati huo waliona ‘mkono wazi’ wa Mungu ukikakamua nguvu katika mambo ya kibinadamu ili kuleta wokovu wa pekee kwa taifa. Walipewa ithibati isiyotilika shaka kwamba Isaya na Ezekieli walikuwa wajumbe wa kweli wa Yehova. Hakuna yeyote angeweza kushuku kwamba Mungu wa Sayuni alikuwa Mungu pekee anayeishi na wa kweli katika dunia yote. Kwenye Isaya 35:2, twasoma juu ya urudisho huo: “Watauona utukufu wa BWANA, ukuu wa Mungu wetu.” Wale waliokubali ithibati hii ya Uungu wa Yehova na walianza kumwabudu.
-