Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uadilifu Wachipuka Katika Sayuni
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • a Isaya 61:5 yaweza kuwa ilitimizwa nyakati za kale, kwa kuwa watu wasio Wayahudi waliambatana na Wayahudi wa asili wakati wa kurudi kwao Yerusalemu, na inaelekea walisaidia kuirudishia nchi hali yake ya kwanza. (Ezra 2:43-58)

  • Uadilifu Wachipuka Katika Sayuni
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 10. Wayahudi wanaorudi kutoka Babiloni wanapatwa na hisia gani kutokana na tendo kubwa ambalo Yehova anawafanyia?

      10 Wayahudi wanaorudi kutoka Babiloni wanatambua kwamba Yehova amewafanyia tendo kubwa. Kuomboleza kwao wakiwa mateka kunageuka kuwa furaha nyingi na sifa kwa sababu hatimaye wamekuwa huru. Hivyo, Isaya anatimiza utume wake wa kiunabii, yaani, “kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti [“mikubwa,” “NW”] ya haki [“uadilifu,” “NW”], iliyopandwa na BWANA, ili atukuzwe.”—Isaya 61:3.

  • Uadilifu Wachipuka Katika Sayuni
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 12, 13. (a) Ni akina nani waliokuwa ‘miti mikubwa ya haki’ miongoni mwa Wayahudi wenye kurudi mwaka wa 537 K.W.K.? (b) Ni akina nani ambao wamekuwa ‘miti mikubwa ya haki’ tangu Pentekoste ya 33 W.K.?

      12 Yehova anawabariki watu wake kwa kuwapa ‘miti mikubwa ya haki.’ Miti hiyo mikubwa ni akina nani? Katika miaka iliyofuata mwaka wa 537 K.W.K., miti hiyo ilikuwa watu mmoja-mmoja waliojifunza Neno la Mungu na kulitafakari, kisha wakasitawisha viwango vya Yehova vya uadilifu. (Zaburi 1:1-3; Isaya 44:2-4; Yeremia 17:7, 8) Wanaume kama vile Ezra, Hagai, Zekaria, na Kuhani Mkuu Yoshua walionekana hakika kwamba wao ni ‘miti mikubwa’ ya kutokeza—watu walio imara kuitetea kweli na kupinga uchafuzi wa kiroho katika taifa hilo.

  • Uadilifu Wachipuka Katika Sayuni
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 14, 15. Waabudu wa Yehova waliofunguliwa walianza miradi gani kuanzia mwaka wa (a) 537 K.W.K.? (b) 33 W.K.? (c) 1919?

      14 Akikazia kazi ya “miti” hii, Isaya anaendelea kusema hivi: “Nao watajenga mahali pa kale palipoharibiwa, watapainua mahali palipokuwa ukiwa zamani, watatengeneza miji iliyoharibiwa, mahali palipoachwa kizazi baada ya kizazi.” (Isaya 61:4) Chini ya amri ya Mfalme Koreshi wa Uajemi, Wayahudi waaminifu waliorudi Babiloni walijenga upya Yerusalemu na hekalu lake lililokuwa limeachwa ukiwa muda mrefu sana.

  • Uadilifu Wachipuka Katika Sayuni
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Yehova alimpulizia Isaya kutangaza hivi: “Wageni watasimama na kulisha makundi yenu, na watu wa kabila nyingine watakuwa wakulima wenu, na watunzaji wa mizabibu yenu.” (Isaya 61:5)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki