-
“Jina Jipya”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Sura Ya Ishirini Na Tatu
“Jina Jipya”
1. Ni uhakikisho gani ambao umeandikwa katika Isaya sura ya 62?
WAYAHUDI walioshuka moyo kule Babiloni wanahitaji hasa kupewa uhakikisho, faraja, na tumaini la kurudishwa. Miongo kadhaa imepita tangu Yerusalemu na hekalu lake ziharibiwe. Umbali wa kilometa 800 hivi kutoka Babiloni, nchi ya Yuda imekaa hali ya ukiwa, na inaonekana ni kama Wayahudi wamesahauliwa na Yehova. Ni nini kinachoweza kuleta maendeleo katika hali yao? Ni ahadi za kwamba Yehova atawarejesha nyumbani na kuwaruhusu warudishe ibada safi. Ndipo mitajo kama vile “Aliyeachwa” na “Ukiwa” zitaondolewa, na badala yake kuweko majina yanayoonyesha ukubali wa Mungu. (Isaya 62:4; Zekaria 2:12) Sura ya 62 ya Isaya imejaa ahadi hizo.
-
-
“Jina Jipya”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
2. Kwa mara nyingine, Yehova anaonyeshaje kwamba anamkubali Sayuni?
2 Babiloni yapinduliwa mwaka wa 539 K.W.K. Baada ya hapo, Mfalme Koreshi wa Uajemi anatoa amri inayowawezesha Wayahudi wanaomhofu Mungu warejee Yerusalemu wakairudishe ibada ya Yehova. (Ezra 1:2-4) Mwaka wa 537 K.W.K., Wayahudi wa kwanza kurudi wamekwisha fikia nchi yao. Kwa mara nyingine Yehova anaonyesha kwamba anamkubali Yerusalemu, kama vile inavyoonyeshwa kwa uchangamfu unaotumiwa kutoa tangazo lake la kiunabii: “Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, na kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia [“sitakaa kimya,” “NW”], hata haki yake itakapotokea kama mwangaza, na wokovu wake kama taa iwakayo [“mwenge,” “VB”].”—Isaya 62:1.
3. (a) Kwa nini Sayuni wa kidunia anakataliwa na Yehova mwishowe, na ni nani anayechukua mahali pake? (b) Ni ukengeufu gani unaotukia, unatukia wakati gani, nasi tunaishi katika kipindi gani leo?
3 Mwaka wa 537 K.W.K., Yehova alitimiza ahadi yake kuelekea Sayuni, au Yerusalemu, iliyorudishwa. Wakaaji wake waliona akiwapa wokovu, na uadilifu wao ukang’aa sana.
-
-
“Jina Jipya”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Wapewa “Jina Jipya” na Yehova
6. Yehova ana lengo gani kuhusu Sayuni?
6 Yehova ana lengo gani kuhusu Sayuni, “mwanamke” wake wa kimbingu, aliyewakilishwa na Yerusalemu la kale? Anasema hivi: “Mataifa wataiona haki yako [“Ee mwanamke,” “NW”], na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha BWANA.” (Isaya 62:2) Wakati Waisraeli wanapotenda uadilifu, mataifa yanalazimika kuangalia kwa makini. Hata wafalme wanalazimika kukubali kwamba Yehova anatumia Yerusalemu na kwamba utawala wowote walio nao si kitu ukilinganishwa na Ufalme wa Yehova.—Isaya 49:23.
7. Jina jipya la Sayuni linamaanisha nini?
7 Sasa Yehova anampa Sayuni jina jipya ili kuthibitisha kwamba hali yake imebadilika. Jina hilo jipya linamaanisha hali yenye baraka na cheo chenye heshima kinachofurahiwa na watoto wa kidunia wa Sayuni kuanzia mwaka wa 537 K.W.K.a Linaonyesha kwamba Yehova anamkubali Sayuni kuwa mali yake.
-
-
“Jina Jipya”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
8. Yehova amemheshimu Sayuni kwa njia zipi?
8 Akiisha kumpa Sayuni jina jipya, sasa Yehova anaahidi hivi: “Utakuwa taji ya uzuri katika mkono wa BWANA, na kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako.” (Isaya 62:3) Yehova anamwinua mke wake wa mfano, Sayuni wa kimbingu, atazamwe kwa mshangao kwa sababu anavutia. (Zaburi 48:2; 50:2) Taji la uzuri na “kilemba cha kifalme” zinaonyesha kwamba mke huyo amevikwa heshima na mamlaka. (Zekaria 9:16)
-