-
Mwongozo Bora wa Kupata FurahaMnara wa Mlinzi—2006 | Juni 15
-
-
Yesu alithibitisha ukweli huo baada ya kifo cha rafiki yake Lazaro. Yesu alilinganisha kifo na usingizi. Ikiwa Lazaro alienda mbinguni kuwa pamoja na Mungu Mweza-Yote, halingekuwa jambo la fadhili kwa Yesu kumrudisha duniani ili mwishowe afe tena. Simulizi lililoongozwa kwa roho ya Mungu linasema kwamba kwenye kaburi, Yesu alipaaza sauti hivi: “Lazaro, njoo huku nje!” Biblia inaendelea kusema: “Huyo mtu aliyekuwa mfu akatoka.” Hivyo, Lazaro akawa hai tena. Yesu alijua kwamba Lazaro hakuondoka duniani na kwenda mahali pengine. Alikuwa amelala kaburini akiwa amekufa.—Yohana 11:11-14, 34, 38-44.
-
-
Mwongozo Bora wa Kupata FurahaMnara wa Mlinzi—2006 | Juni 15
-
-
Kuna angalau sababu mbili zilizomchochea Yesu kufanya muujiza huo. Sababu ya kwanza ilikuwa kuondoa huzuni ya Martha, Maria, na pia marafiki waliokuwa wakiomboleza. Kwa mara nyingine tena, wangeweza kushirikiana na mpendwa wao. Hata hivyo, Yesu alimtajia Martha sababu ya pili iliyokuwa muhimu zaidi: “Je, sikukuambia kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?” (Yohana 11:40) Kitabu kimoja (The New Testament in Modern English) kilichoandikwa na J. B. Phillips, kinatafsiri sentensi ya mwisho kuwa “maajabu ambayo Mungu anaweza kufanya.” Kwa kumfufua Lazaro, Yesu alionyesha kimbele yale ambayo Yehova Mungu anaweza kufanya na yale ambayo atafanya wakati ujao.
-