Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Suluhisho Pekee la Kifo!
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Machi 15
    • Ni Nani Watakaofufuliwa?

      Yesu alisema hivi: “Saa inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti [ya Yesu] na kutoka.” (Yohana 5:28, 29) Kulingana na ahadi hiyo, wale waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho, yaani, wale walio katika kumbukumbu ya Yehova, watafufuliwa. Basi swali ni, Kati ya watu wote ambao wamekufa, ni nani walio katika kumbukumbu ya Mungu wakingojea kufufuliwa?

      Kitabu cha Biblia cha Waebrania sura ya 11 kinaorodhesha majina ya wanaume na wanawake ambao walimtumikia Mungu kwa uaminifu. Wao pamoja na watumishi washikamanifu wa Mungu ambao wamekufa katika miaka ya karibuni, watafufuliwa. Namna gani watu ambao hawakuishi kulingana na viwango vya Mungu vya uadilifu, labda kwa sababu ya kutokuwa na ujuzi? Je, wao pia wamo katika kumbukumbu ya Mungu? Ndiyo, wengi wamo, kwa kuwa Biblia inaahidi: “Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.”—Matendo 24:15.

  • Suluhisho Pekee la Kifo!
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Machi 15
    • Ni Nani Watakaofufuliwa Ili Waishi Duniani?

      Kulingana na Maandiko, watu wengi waliokufa watarudishwa kwenye uhai duniani. (Zaburi 37:29; Mathayo 6:10) Akieleza maono yake yenye kustaajabisha ya wale watakaofufuliwa, mtume Yohana aliandika hivi: “Bahari ikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake, na kifo na Kaburi [“Hadesi,” maelezo ya chini] vikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake, nao walihukumiwa kila mmoja kulingana na matendo yake. Na kifo na Kaburi vikatupwa ndani ya lile ziwa la moto. Hili linamaanisha kifo cha pili, lile ziwa la moto.” (Ufunuo 20:11-14) Wale walio katika Hadesi au Sheoli, yaani, kaburini, wamo katika kumbukumbu ya Mungu. Kila mmoja wao atafufuliwa. (Zaburi 16:10; Matendo 2:31) Kila mmoja wao atahukumiwa kulingana na mambo atakayofanya baada ya kufufuliwa. Kisha itakuwaje kwa kifo na Kaburi? Vitatupwa katika “ziwa la moto.” Hiyo inamaanisha kwamba wanadamu hawataathiriwa tena na kifo ambacho walirithi kutoka kwa Adamu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki