-
Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na mimi nikaona wafu, wakubwa na wadogo, wakisimama mbele ya kiti cha ufalme na hati-kunjo zilifunguliwa.” (Ufunuo 20:12a, NW) “Wakubwa na wadogo” hutia ndani walio mashuhuri pamoja na wasio mashuhuri sana wa wanadamu ambao wameishi na wakafa kwenye dunia hii wakati wa miaka 6,000 iliyopita. Katika Gospeli ambayo Yohana aliandika muda mfupi baada ya Ufunuo, Yesu alisema kwa habari ya Baba yake: “Naye akampa [Yesu] amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu. Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka.” (Yohana 5:27-29) Ni mradi mkubwa ajabu kama nini—kutangua vifo na makaburi ya muda wote wa historia! Hapana shaka hayo mamilioni yasiyohesabika yaliyo katika kumbukumbu la Mungu watatokezwa hatua kwa hatua hivi kwamba umati mkubwa—ambao ni wachache sana kwa kulinganisha—utaweza kushughulikia matatizo ambayo huenda yatazuka kwa sababu huenda mwanzoni wafufuliwa wakaelekea kufuata mtindo wao wa maisha ya kale, pamoja na udhaifu wa mnofu wao na mielekeo.
Nani Wanainuliwa na Kuhukumiwa?
7, 8. (a) Ni hati-kunjo gani inayofunguliwa, na ni jambo gani linalotukia baada ya hapo? (b) Ni kwa akina nani hakutakuwa na ufufuo?
7 Yohana anaongeza: “Lakini hati-kunjo nyingine ikafunguliwa; ndiyo hati-kunjo ya uhai. Na wafu walihukumiwa kutoka kwa vile vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo kulingana na matendo yao. Na bahari ikatoa wafu wale walio ndani yayo na kifo na Hadesi vikatoa wafu wale walio ndani yavyo na wao walihukumiwa mmoja mmoja kulingana na matendo yao.” (Ufunuo 20:12b, 13, NW) Tamasha yenye kusisimua kweli kweli! ‘Bahari, kifo, na Hadesi’ kila mojapo inatimiza sehemu, lakini angalia kwamba semi hizi si za pekee baina yazo zenyewe.a Wakati Yona alipokuwa tumboni mwa samaki mmoja na kwa hiyo akawa katikati ya bahari, yeye alisema juu yake mwenyewe kuwa alikuwa katika Sheoli, au Hadesi. (Yona 2:2) Ikiwa mtu anashikwa na kifo cha Adamu, basi yaelekea yeye pia yumo katika Hadesi. Maneno haya ya kiunabii yanatoa uhakikisho imara kwamba hakuna hata mmoja atakayekosa kuonwa.
-
-
Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
9. Mtume Paulo anaonyeshaje kwamba baadhi yao watapendelewa kipekee katika ufufuo, na hao wanatia ndani akina nani?
9 Kwa upande mwingine, baadhi yao watapendelewa kipekee katika ufufuo huu. Mtume Paulo alionyesha hivyo wakati aliposema: “Mimi nina tumaini kuelekea Mungu . . . kwamba kutakuja kuwa na ufufuo wa wote walio waadilifu na wasio waadilifu.” (Matendo 24:15, NW) Kwa habari ya ufufuo wa kidunia, “walio waadilifu” watatia ndani wanaume na wanawake waaminifu wa kale—Abrahamu, Rahabu, na wengine wengi—ambao walijulishwa wazi kuwa waadilifu kwa habari ya kuwa na urafiki na Mungu. (Yakobo 2:21, 23, 25) Katika kikundi iki hiki watakuwamo wale kondoo wengine waadilifu ambao walikufa wakiwa waaminifu kwa Yehova katika nyakati za ki-siku-hizi. Yaelekea, washika ukamilifu wote hao watafufuliwa mapema katika Utawala wa Mileani wa Yesu. (Ayubu 14:13-15; 27:5; Danieli 12:13; Waebrania 11:35, 39, 40) Pasi na shaka wengi wa hawa waadilifu waliofufuliwa watapewa migawo ya pendeleo la pekee katika kusimamia kazi kubwa mno ya urudisho katika Paradiso.—Zaburi 45:16; linga Isaya 32:1, 16-18; 61:5; 65:21-23.
10. Kati ya wale watakaofufuliwa, ni nani “wasio waadilifu”?
10 Ingawa hivyo, ni nani “wasio waadilifu” wanaotajwa katika Matendo 24:15, NW? Hawa wangetia ndani matungamo ya aina ya binadamu ambayo yamekufa muda wote wa historia, hasa wale ambao waliishi katika ‘nyakati za ujinga.’ (Matendo 17:30) Hawa, kwa sababu ya mahali walipozaliwa au wakati walimoishi, hawakuwa na fursa ya kujifunza kutii penzi la Yehova. Kwa kuongezea, huenda kukawa na baadhi ya waliosikia ujumbe wa wokovu lakini ambao hawakuitikia kikamili katika wakati huo au ambao walikufa kabla ya wao kuendelea kufikia wakfu na ubatizo. Katika ufufuo watu kama hao watahitaji kufanya marekebisho zaidi katika kufikiri na mwendo wao wa maisha ikiwa wao watanufaika na fursa hii kwa ajili ya kupata uhai wa milele.
-