-
UfufuoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Ufufuo unahusisha kuanzisha tena maisha ya mtu, ambayo Mungu amehifadhi katika kumbukumbu lake. Kulingana na mapenzi ya Mungu kwake, mtu huyo anarudishwa katika mwili wa kibinadamu au katika mwili wa roho na bado abaki na utambulisho wake mwenyewe, akiwa na utu uleule na kumbukumbu zilezile alizokuwa nazo wakati alipokufa.
-
-
UfufuoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Je, ufufuo ni kuunganishwa tena kwa nafsi isiyo na mwili pamoja na mwili wenye nyama?
Bila shaka, ili hilo liwezekane, ingekuwa lazima wanadamu wawe na nafsi isiyo na mwili ambayo ingeweza kutengana na mwili wenye nyama. Biblia haifundishi jambo hilo. Wazo hilo lilitolewa katika falsafa ya Kigiriki. Fundisho la Biblia kuhusu nafsi liko katika ukurasa wa 221-224. Ili upate uthibitisho kuhusu chanzo cha imani ya Jumuiya ya Wakristo katika nafsi isiyo na mwili, isiyoweza kufa, ona ukurasa wa 225, 226.
-