-
“Kifo Kitafanywa Kuwa Si Kitu”Mnara wa Mlinzi—1998 | Julai 1
-
-
11. (a) Twajuaje kwamba Mungu aweza kuumba tena nafsi zilizokufa? (b) Watakaofufuliwa duniani watapewa miili ya aina gani?
11 Hilo lamaanisha kuumba tena nafsi za kibinadamu. Je, ni jambo lisilowezekana? La, kwa kuwa andiko la Zaburi 104:29, 30 latuhakikishia kwamba Mungu aweza kufanya hivyo: “Waiondoa pumzi yao, wanakufa, na kuyarudia mavumbi yao, waipeleka roho yako, wanaumbwa.” Ingawa wenye kufufuliwa watakuwa watu walewale waliokuwa kabla ya kufa, hawatahitaji kuwa na miili ileile. Sawa na wale watakaofufuliwa kwenda mbinguni, Mungu atawapa mwili kama vile impendezavyo. Bila shaka miili yao mipya itakuwa yenye afya na kwa kufaa itakuwa sawa na miili yao ya hapo awali, hivi kwamba wapendwa wao wataweza kuwatambua.
-
-
“Kifo Kitafanywa Kuwa Si Kitu”Mnara wa Mlinzi—1998 | Julai 1
-
-
8. (a) Twajuaje kwamba wenye kufufuliwa watakuwa watu walewale waliokuwa hai duniani? (b) Ni unabii gani mbalimbali unaotimizwa ufufuo utokeapo?
8 Licha ya mgeuzo umbo huo, wenye kufufuliwa bado watakuwa watu walewale waliokuwa kabla ya kufa. Watafufuliwa na kumbukumbu zilezile na sifa zilezile bora za Kikristo. (Malaki 3:3; Ufunuo 21:10, 18) Katika hilo wanafanana na Yesu Kristo. Umbo lake la roho lilibadilika kuwa la kibinadamu. Kisha akafa na kufufuliwa akiwa roho. Hata hivyo, “Yesu Kristo ni yuleyule jana na leo, na milele.” (Waebrania 13:8)
-