-
‘Nafsi Zilizochinjwa’ ZathawabishwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
12. Ni katika njia gani Wakristo waliofufuliwa ‘hupumzika kwa kitambo kidogo zaidi,’ na mpaka lini?
12 Ithibati yote huonyesha kwamba ufufuo huu wa kimbingu ulianza katika 1918, baada ya Yesu kuketishwa juu ya kiti cha ufalme katika 1914 na kutoka kwake aende akipanda farasi kuanza ushindi wake wa kifalme kwa kuzisafisha mbingu watoke Shetani na roho waovu wake.
-
-
‘Nafsi Zilizochinjwa’ ZathawabishwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
‘Wale Ambao Wamekufa Wainuka Kwanza’
13, 14. (a) Kulingana na mtume Paulo, ufufuo wa kimbingu huanza lini, na ni nani wanaofufuliwa? (b) Wale wapakwa-mafuta wanaoendelea kuishi kufikia siku ya Bwana wanafufuliwa lini waende mbinguni?
13 Ule muono-ndani unaotolewa kwa kufunguliwa kwa kifungo cha tano unakubaliana kabisa kabisa na maandiko mengine yanayohusiana na ufufuo wa kimbingu. Mathalani, mtume Paulo aliandika hivi: “Kwa maana hili ndilo ambalo sisi tunaambia nyinyi kwa neno la Yehova, kwamba sisi tulio hai ambao twaishi kufikia kuwapo kwa Bwana hatutatangulia kwa vyovyote wale ambao wamelala usingizi katika kifo; kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni akiwa na mwito wa kuamuru, na sauti ya malaika mkuu na tarumbeta ya Mungu, na wale ambao wamekufa katika muungano pamoja na Kristo watainuka kwanza. Baadaye sisi tulio hai ambao twaendelea kuishi, pamoja nao, tutadakwa mbali katika mawingu ili kumkuta Bwana katika hewa; na hivyo sisi tutakuwa na Bwana sikuzote.”—1 Wathesalonike 4:15-17, NW.
14 Ni hadithi yenye kusisimua kama nini ambayo mistari hii inasimulia! Wale wa ndugu za Yesu wapakwa-mafuta ambao huendelea kuishi kufikia kuwapo kwa Yesu, yaani, ambao wangali hai duniani wakati wa kuwapo kwake, wanatanguliwa kuingia ndani ya mbingu na wale ambao tayari wamekufa. Hao, ambao wamekufa katika muungano pamoja na Kristo, huinuka kwanza. Yesu hushuka, yaani, huelekeza uangalifu kwao, na kuwafufua kwenye uhai wa roho, akiwapa “joho jeupe.” Baadaye, wale ambao wangali hai wakiwa binadamu wanamaliza mwendo wao wa kidunia, wengi wao wakifa kijeuri mikononi mwa wapinzani. Hata hivyo, wao hawalali usingizi katika kifo kama watangulizi wao walivyofanya. Badala ya hivyo, wanapokufa, wao huinuliwa mara hiyo—“katika kufumba na kufumbua jicho”—wakidakwa mbali kwenda katika mbingu wakawe pamoja na Yesu na washiriki wenzi wa mwili wa Kristo. (1 Wakorintho 15:50-52, NW; linga Ufunuo 14:13.) Hivyo, kufufuliwa kwa Wakristo wapakwa-mafuta huanza upesi baada ya wale wapandaji-farasi wanne wa Apokalipsi kuanza upandaji wao.
-