Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Uliwahi Kuishi Katika Mwili Mwingine?
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Desemba 1
    • Ufufuo​—Tumaini Lililothibitishwa kwa Ajili ya Wafu

      Biblia ina masimulizi manane kuhusu watu waliojionea wafu wakifufuliwa hapa duniani.b Masimulizi hayo yanataja watu hao walifufuliwa wala si kubadilika na kuwa na mwili mwingine. Watu wa ukoo na marafiki waliwatambua watu wao waliofufuliwa. Watu hao wa ukoo hawakuhitaji kutafuta kati ya watoto waliokuwa wamezaliwa hapo karibu na kuchagua yupi kati yao alikuwa na nafsi ya mtu wao aliyekuwa amekufa.​—Yohana 11:43-45.

      Jambo lenye kufariji ni kwamba Neno la Mungu linaonyesha kuwa watu wengi ambao wamekufa watafufuliwa wakati Mungu atakapowafufua watu katika ulimwengu mpya, ambao hivi karibuni utachukua mahali pa ulimwengu huu mwovu. (2 Petro 3:13, 14) Wakati huu, mtindo wa maisha wa mabilioni ya watu umehifadhiwa katika kumbukumbu kamilifu la Yehova ambalo halina kipimo, Mungu ambaye anakumbuka majina ya nyota zote! (Zaburi 147:4; Ufunuo 20:13) Atakapomaliza kuwarudishia watu wengi uhai katika ulimwengu mpya, watakuwa na uwezo wa kufuatilia ukoo wao na kutambua mababu zao. Hilo ni tumaini lenye kuvutia kama nini!

  • Je, Uliwahi Kuishi Katika Mwili Mwingine?
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Desemba 1
    • Tumaini Bora Zaidi

      Badala ya kujaribu kuunganisha habari kuhusu maisha ya zamani ambayo ni yenye kutiliwa shaka na yasiyoeleweka, kwa nini usitenge wakati uchunguze mambo ambayo Biblia inafundisha kuhusu ufufuo? Biblia inatoa majibu yenye kuridhisha sasa na faraja ya kweli tunapokuwa na huzuni.

      Kwa mfano, Theodore alijawa na majonzi alipompoteza Rosemarie, mke wake mpendwa ambaye walikuwa wamefunga ndoa kwa miaka 44. Alisema: “Ninajua Rosemarie yuko mahali salama kabisa, yaani, katika kumbukumbu la Yehova. Masimulizi ya Biblia yanayohusu ufufuo ni ya kweli, kuna watu wengi waliojionea kwa macho wanaoweza kuthibitisha kwamba ulitukia, ninasubiri kusikia Yesu akisema, kama alivyomwambia Lazaro: ‘Rosemarie, njoo huku nje!’”

      Costas na Maria walikumbwa na mkasa mkubwa sana walipompoteza binti yao mwenye umri wa miezi 20 kwa sababu ya tatizo la chembe za urithi. Maria anasema: “Kifo cha binti yetu Evi, kilitutia uchungu kwelikweli. Kutoka wakati huo na kuendelea, tumeelewa zaidi kuteseka, kifo, na ufufuo. Maandiko ya Biblia kama vile Isaya 33:24; 35:5, 6; na Ufunuo 21:4, 5 yana maana kubwa sana kwetu! Ndiyo, Yehova amekuwa Baba mwenye upendo na ametupa tumaini la kweli la ufufuo.”

      Majibu ya Biblia kuhusu uhai na kifo yanatoka moja kwa moja kwa Muumba wetu. Kama Theodore, Costas, na Maria, wewe pia unaweza kuwa na tumaini la kweli la wakati ujao ikiwa utajenga msingi wenye nguvu katika Neno la Mungu. Kamwe haliwezi kusema uwongo!​—Tito 1:2.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki