Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Wapaswa Kuamini Katika Kutwaa Umbo Jipya?
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Mei 15
    • Utu wa Mungu na Sheria ya Karma

      “Sheria ya Karma,” akafafanua Mohandas K. Gandhi, “ni isiyobadilika na isiyoweza kuepukwa. Hivyo hakuna uhitaji wa Mungu kuingilia mambo. Aliiweka hiyo sheria na, kusema kitamathali, akastaafu.” Gandhi aliona ufafanuzi huo kuwa wenye kusumbua.

      Kwa upande mwingine, ahadi ya ufufuo hufunua kwamba Mungu anapendezwa sana na viumbe wake. Kumrudisha mfu kwenye uhai tena katika dunia iliyo paradiso, lazima Mungu ajue na kukumbuka kila jambo juu ya mtu huyo. Kwa kweli Mungu hujali kila mmoja wetu.—1 Petro 5:6, 7.

  • Je, Wapaswa Kuamini Katika Kutwaa Umbo Jipya?
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Mei 15
    • Mukundbhai, aliyetajwa katika makala iliyotangulia, amelala usingizi katika kifo bila kujua ahadi za ajabu za Mungu. Lakini mamilioni ya watu ambao wamekufa bila kumjua Mungu wana tazamio la kuamshwa katika ulimwengu huo mpya wenye amani, kwa kuwa Biblia yaahidi hivi: “Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.”—Matendo 24:15; Luka 23:43.

      Neno “ufufuo” latafsiriwa hapa kutoka neno la Kigiriki a·naʹsta·sis, linalomaanisha kihalisi “kusimama tena.” Hivyo ufufuo huhusisha kutendesha upya kwa kiolezo cha maisha ya mtu.

      Muumba wa mbingu na dunia ana hekima isiyo na kikomo. (Ayubu 12:13) Kukumbuka violezo vya maisha za wafu si tatizo kwake. (Linganisha Isaya 40:26.) Yehova Mungu pia ana upendo mwingi. (1 Yohana 4:8) Kwa sababu hiyo, yeye aweza kutumia kumbukumbu lake kamilifu, si kwa minajili ya kuadhibu wafu kwa sababu ya ubaya ambao wamefanya, bali ili kuwarudisha kwenye uhai katika dunia iliyo paradiso wakiwa na utu waliokuwa nao kabla hawajafa.

      Kwa mamilioni ya watu kama Mukundbhai, ufufuo utamaanisha kuwa na wapendwa wao tena. Lakini wazia uwezalo kumaanisha kwa wale wanaoishi sasa. Kwa kielelezo, chukua mwana wa Mukundbhai, ambaye amekuja kujua kweli ya ajabu juu ya Mungu na makusudi yake. Yafariji kama nini kwake kujua kwamba baba yake hakukwama katika duru isiyoelekea kwisha ya kuzaliwa upya mara nyingi, kila duru ikiwa imezingirwa na uovu na kuteseka! Yeye amelala usingizi tu katika kifo, akingojea ufufuo. Yasisimua kama nini kwake kutafakari uwezekano wa kushiriki na babaye siku moja yale ambayo yeye mwenyewe amejifunza kutoka katika Biblia!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki