Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Uwaambie Neno Hili”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
    • 13, 14. (a) Kuhusu ziara za kurudia, mfano wa Yeremia unatusaidia jinsi gani? (b) Kwa nini tunapaswa kuwa wenye kutegemeka tunapoahidi kufanya ziara za kurudia?

      13 Pindi kadhaa, Yehova alimwamuru Yeremia atangaze ujumbe wa kinabii akiwa amesimama katika malango ya hekalu au ya Yerusalemu. (Yer. 7:2; 17:19, 20) Kwa kufanya hivyo, Yeremia aliweza kuwafikia watu wengi na neno la Yehova. Kwa kuwa watu wengi, kutia ndani watu mashuhuri wa jiji na wafanyabiashara walipita hapo mara nyingi, huenda alizungumza na baadhi yao tena na tena akijaribu kuwasaidia kuelewa mambo waliyokuwa wamesikia. Tunaweza kufuata jinsi gani mfano huo tunapowarudia watu wanaopendezwa?

      14 Yeremia alijua kwamba ujumbe aliokuwa nao ungeweza kuokoa uhai. Pindi moja, wakati ambapo hangeweza kuwaambia watu maagizo ya Mungu, alimtuma rafiki yake, Baruku, amwakilishe. (Soma Yeremia 36:5-8.) Tunaweza kufuata jinsi gani mfano wa Yeremia? Tukimwahidi mwenye nyumba kwamba tutarudi, je, sisi hufanya hivyo? Ikiwa hatuwezi, je, tunapanga mtu mwingine amrudie? Yesu alisema: “Neno lenu Ndiyo limaanishe Ndiyo.” (Mt. 5:37) Ni muhimu kutimiza ahadi, kwa kuwa tunamwakilisha Mungu wa kweli mwenye utaratibu.—1 Kor. 14:33, 40.

      Picha katika ukurasa wa 39

      Umebadili ratiba yako na njia zako za kuhubiri ili uweze kuwafikia watu wengi zaidi?

  • “Uwaambie Neno Hili”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
    • Shahidi mmoja huko Chile alianzisha mazungumzo na mwanamke aliyekuwa akitoka katika kituo cha gari-moshi. Mwanamke huyo alipendezwa sana na ujumbe wa Biblia naye akakubali kujifunza Biblia nyumbani kwake. Hata hivyo, Shahidi huyo, hakuandika mahali ambapo mwanamke huyo anaishi. Baadaye, akiwa na nia ya kuendeleza hamu ya mwanamke huyo ya kujifunza kweli, dada yetu alimwomba Yehova msaada katika sala. Siku iliyofuata, alirudi kwenye kituo kilekile. Alikutana na mwanamke yule tena. Wakati huo, aliandika mahali anapoishi na baadaye akamtembelea nyumbani kwake ili kumsaidia kuelewa Maandiko.

      Picha katika ukurasa wa 40

      Je, wewe hufanya yote uwezayo ili kuwarudia watu wanaopendezwa?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki