Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka
    Huduma ya Ufalme—1997 | Februari
    • 3 Unaweza kuendeleza mazungumzo ya wakati uliopita ya Ufunuo 21:1, 4 kwa utoaji huu mfupi:

      ◼ “Katika ziara yangu iliyopita, tuliongea kuhusu ahadi ya Mungu ya kutayarisha jamii mpya ya kidunia kwa ajili ya wanadamu. [Elekeza fikira tena kwenye picha iliyo kwenye ukurasa wa 302 katika kitabu Upeo wa Ufunuo.] Je, ungependa kuona familia yako ikifurahia hali kama hizo? [Ruhusu itikio.] Swali ni, Ahadi za Mungu ni zenye kutegemeka kadiri gani? Tafadhali ona yale ambayo yeye mwenyewe husema.” Soma Ufunuo 21:5, 6a katika fungu la 8 kwenye ukurasa wa 303. Uliza swali lililochapwa la fungu la 9 kwenye ukurasa wa 304, na usome jibu, kutia ndani sentensi ya mwisho ya fungu hilo. Taja toleo la funzo la Biblia bila malipo. Panga kulionyesha baadaye.

  • Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka
    Huduma ya Ufalme—1997 | Februari
    • 5 Ikiwa uliahidi kurudi ueleze utatuzi wa Mungu wa matatizo ya leo, unaweza kujaribu mfikio huu:

      ◼ “Nilifanya jitihada ya pekee kurudi ili tuweze kuendeleza mazungumzo yetu juu ya utatuzi halisi wa matatizo yanayokabili wanadamu. Katika ziara yangu iliyopita, tuliona kwamba Biblia humtambulisha Shetani Ibilisi kuwa anayeongoza vibaya dunia nzima inayokaliwa na watu. Kwa kuwa yeye ni kiumbe-roho mwenye uwezo kupita ule wa binadamu, unafikiri kuna njia ya kuondoa uvutano wake? [Ruhusu itikio.] Tafadhali ona vile Biblia husema.” Soma na ueleze Ufunuo 20:1-3. Kwa kutumia picha iliyo kwenye kurasa 4-5 za kitabu Ujuzi, onyesha hali zitakavyokuwa bila uvutano wa Shetani. Mtolee funzo la Biblia na ujitahidi kulianzisha mara hiyo.

  • Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka
    Huduma ya Ufalme—1997 | Februari
    • 7 Unaporudia mtu aliyeonyesha kupendezwa katika dunia ya Paradiso, unaweza kusema hivi:

      ◼ “Katika ziara yangu iliyopita, tulikubaliana kwamba ili kutatua matatizo ya dunia iliyochafuliwa, itambidi Mungu aingilie mambo ya mwanadamu. Lakini swali ni, Lazima tufanye nini ili kuokoka kuingia katika ulimwengu mpya wenye uadilifu uliofanyizwa na Mungu?” Soma Yohana 17:3. Alika mwenye nyumba atwae manufaa ya mtaala wetu wa funzo la Biblia bila malipo ili apate ujuzi huu wa pekee.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki