-
Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya BwanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 18
Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya Bwana
1, 2. (a) Ikoje kuishi kupitia tetemeko la dunia kali? (b) Yohana anaeleza habari ya nini wakati kifungo cha sita kinapofunguliwa?
JE! WEWE umewahi kuishi kupitia tetemeko la dunia kali? Si ono zuri. Mtetemeko mkubwa huenda ukaanza kwa msukosuko wenye kugonjwesha na kelele yenye mtutumo. Myumboyumbo huenda ukazidi kuwa mbaya vipindi kwa vipindi na huku wewe ukikimbilia usalama—pengine chini ya dawati. Au huenda likaja likiwa mshtuo wa ghafula, wenye kuvunjavunja, ukifuatwa na kuvunjikavunjika kwa vikombe na sahani, samani na hata majengo. Uharibifu huenda ukawa wenye kuleta hasara sana, kukiwa na mishtuo ya baadaye ikileta uharibifu zaidi na kuongezea janga.
2 Ukiwa na hayo akilini, fikiria yale ambayo Yohana anaeleza wakati wa kufunguliwa kwa kifungo cha sita: “Na mimi nikaona wakati yeye alipofungua kifungo cha sita, na tetemeko la dunia kubwa likatukia.” (Ufunuo 6:12a, NW) Lazima hili lianguke katika muda wa wakati ule ule wa kufunguliwa kwa vile vifungo vingine. Ni wakati gani hasa katika siku ya Bwana tetemeko la dunia hili linatukia, nalo ni tetemo la namna gani?—Ufunuo 1:10.
3. (a) Ni matukio gani aliyotabiri Yesu katika unabii juu ya ishara ya kuwapo kwake? (b) Matetemeko ya dunia halisi yahusianaje na tetemeko la dunia la ufananisho la Ufunuo 6:12?
3 Matetemeko ya dunia ya kihalisi na ya kitamathali yametajwa katika Biblia mara kadhaa. Katika unabii mkubwa juu ya ishara ya kuwapo kwake katika mamlaka ya Ufalme, Yesu alitabiri “matetemeko ya dunia katika mahali pamoja baada ya pengine.” Hayo yangekuwa sehemu ya “mwanzo wa maumivu makali ya ghafula ya taabu.” Tangu 1914, idadi ya watu wa dunia ikiwa inaongezeka ghafula sana kuwa maelfu ya mamilioni, mitetemo hiyo imechangia kwa kutokeza sana taabu za nyakati zetu. (Mathayo 24:3, 7, 8, NW) Hata hivyo, hata ingawa yanatimiza unabii, matetemeko ya dunia hayo yamekuwa misiba asilia, yenye kuonekana. Hayo ni utangulizi wa lile tetemeko la dunia kubwa la ufananisho la Ufunuo 6:12. Kweli kweli, hili laja likiwa ndiyo tamati yenye kukumba ya mfululizo wa mitetemo yenye kutangulia inayotikisa mpaka misingi yenyewe mfumo wa mambo ya kibinadamu wa kidunia wa Shetani.a
Mitetemo Katika Jamii ya Kibinadamu
4. (a) Ni tangu lini watu wa Yehova walikuwa wamekuwa wakitaraji kwamba matukio yenye kuleta uharibifu yangeanza katika 1914? (b) 1914 ungetia alama ya mwisho wa kipindi gani cha wakati?
4 Kuanzia miaka ya katikati ya 1870 watu wa Yehova walikuwa wamekuwa wakitaraji kwamba matukio yenye kuleta uharibifu yangeanza katika 1914 nayo yangeonyesha mwisho wa Majira ya Mataifa. Hiki ndicho kipindi cha “nyakati saba” (miaka 2,520) kikianza na kupinduliwa kwa ufalme wa Kidaudi katika Yerusalemu katika 607 K.W.K. hadi kuketishwa kwa Yesu juu ya kiti cha ufalme katika Yerusalemu la kimbingu katika 1914 W.K.—Danieli 4:24, 25; Luka 21:24.b
5. (a) Ni tangazo gani alilofanya C. T. Russell katika Oktoba 2, 1914? (b) Ni mabadiliko makubwa gani ya kisiasa ambayo yametukia tangu 1914?
5 Hivyo, wakati C. T. Russell alipoonekana kwa ajili ya ibada ya asubuhi pamoja na jamaa ya Betheli ya Brooklyn, New York, asubuhi ya Oktoba 2, 1914, yeye alifanya tangazo hili lenye kusisimua: “Majira ya Mataifa yamekwisha; siku ya wafalme wayo imekwisha.” Kweli kweli, lile badiliko kubwa lililoanza katika 1914 lilikuwa na matokeo makubwa sana hivi kwamba falme nyingi zilizokuwa zimesimama kwa muda mrefu zilitoweka. Lile angusho la utawala wa zari katika pinduzi la Bolsheviki la 1917 liliongoza kwenye mkabiliano wa muda mrefu kati ya Umarksizimu na ukapitalisti (ubepari). Mitetemo ya badiliko la kisiasa yaendelea kusumbua jamii ya kibinadamu duniani pote. Leo, serikali nyingi zinashindwa kuendelea kwa muda unaozidi mwaka mmoja au miwili. Ukosefu wa imara katika ulimwengu wa kisiasa unatolewa kielezi na kisa cha Italia, ambayo ilikuwa na serikali mpya 47 katika muda wa miaka 42 tu kufuatia Vita ya Ulimwengu 2. Lakini mitetemo hiyo ni utangulizi tu wa badiliko kubwa la kiserikali lenye kufikia upeo mkuu. Tokeo litakuwa nini? Ufalme wa Mungu utachukua utawala kamili wa dunia.—Isaya 9:6, 7.
6. (a) H. G. Wells alielezaje habari ya muhula mpya wenye maana kubwa? (b) Mwanafalsafa mmoja na waziri wa serikali mmoja waliandika nini juu ya muhula wa tangu 1914?
6 Wanahistoria, wanafalsafa, na viongozi wa kisiasa wameelekeza kwenye mwaka 1914 kuwa mwanzo wa muhula mpya na wenye maana kubwa. Miaka 17 ya kuingia katika muhula huo, mwanahistoria H. G. Wells alitoa elezo hili: “Kwa mteremo nabii angetoa unabii wa vitu vizuri. Lakini wajibu wake ni kusimulia anachoona. Yeye anaona ulimwengu ambao ungali unadhibitiwa kiimara na askari-jeshi, wazalendo, wala-riba, na mabarakala wa kifedha; ulimwengu uliojikabidhi kwenye shuku na chuki, ukipoteza kwa haraka sana mauhuru ya faragha yaliyobaki, ukijongeza ki-upofu-upofu kuelekea mapambano makali ya kitabaka, na kutayarisha kwa ajili ya vita vipya.” Katika 1953 mwanafalsafa Bertrand Russell aliandika: “Tangu 1914, kila mtu anayejua maelekeo yaliyo katika ulimwengu amesumbuliwa sana na ule ambao umeonekana kuwa kama mwendo wenye tukio baya na uliokusudiwa kimbele kuelekea msiba unaozidi kuwa mkubwa. . . . Wao wanaona jamii ya kibinadamu, kama shujaa wa hadithi yenye misiba ya Kigiriki, akiendeshwa na miungu wenye kasirani na yeye siye bwana-mkubwa tena wa tukio baya.” Katika 1980 waziri wa serikali Harold Macmillan, akirudisha fikira nyuma kwenye mwanzo wenye amani wa karne ya 20, alisema: “Kila kitu kingezidi kuwa bora na bora. Huu ndio ulimwengu nilimozaliwa mimi. . . . Ghafula, asubuhi moja katika 1914 kitu kizima chote kilikuja kwenye mwisho.”
7-9. (a) Ni mabadiliko makubwa gani ambayo yametikisa jamii ya kibinadamu tangu 1914? (b) Mabadiliko makubwa katika jamii ya kibinadamu wakati wa kuwapo kwa Yesu hatimaye yangetia ndani hali gani miongoni mwa wanadamu?
7 Vita ya Ulimwengu 2 ilileta wimbi jingine la mabadiliko makubwa. Na vita vidogo zaidi pamoja na ugaidi wa kimataifa vinaendelea kutikisa dunia. Lile tisho la magaidi au mataifa yanayotumia silaha za maangamizi makubwa linafanya watu wengi wawe na wasiwasi.
8 Ingawa hivyo, mambo mengine licha ya vita yametikisa jamii ya kibinadamu mpaka kwenye misingi yayo tangu 1914. Mojapo mabadiliko makubwa ambalo lilikuwa lenye kuumiza zaidi sana lilianzishwa na anguko la soko la rasilimali la U.S. la Oktoba 29, 1929. Hilo lilileta Ule Mshuko Mkubwa wa Thamani ya Pesa, ambao uliathiri nchi zote za ukapitalisti. Mshuko huo ulifikia upeo wa chini zaidi kati ya 1932 na 1934, lakini sisi tungali tunahisi matokeo yao. Tangu 1929 ulimwengu mgonjwa kiuchumi umetiwa-tiwa viraka kwa kutumia mipango-badala. Serikali zinajitia katika madeni ya kifedha. Ile shida kubwa ya mafuta ya 1973 na mshuko-ghafula wa 1987 wa soko la rasilimali viliongezea mitikiso ya milki ya kifedha. Kwa wakati uliopo, mamilioni ya watu hununua vitu kwa mkopo. Idadi zisizohesabika huwa majeruhi ya madanganyo ya kifedha, mipango ya kipiramidi, na hila za michezo ya bahati-nasibu na kamari, mingi yayo ikiwa inadhaminiwa na serikali ambazo zapaswa kuwa zikiwapa himaya watu. Hata waevanjeli wa televisheni wa Jumuiya ya Wakristo hunyoosha mikono yao wapate hisa yao ya mamilioni ya dola!—Linga Yeremia 5:26-31.
9 Mapema zaidi, shida za kiuchumi zilikuwa zimefungulia njia Mussolini na Hitla wanyakue mamlaka. Babuloni Mkubwa hakupoteza wakati wowote akitafuta kupendwa nao, na Vatikani iliingia katika mapatano na Italia katika 1929 na Ujeremani katika 1933. (Ufunuo 17:5) Zile siku zenye huzuni zilizofuata hakika zilikuwa sehemu ya utimizo wa unabii wa Yesu kuhusu kuwapo kwake, ambao ungetia ndani “huzuni kuu ya mataifa, yasijue njia ya kutokea . . . huku watu wakizirai kwa woga na taraja la vitu vinavyokuja juu ya dunia inayokaliwa.” (Luka 21:7-9, 25-31, NW)c Ndiyo, yale matetemeko yaliyoanza kutikisa jamii ya kibinadamu katika 1914 yameendelea, kukiwa na mishtuo ya baadaye yenye nguvu.
Yehova Atikisa
10. (a) Ni kwa nini kuna mitetemo mingi sana katika mambo ya kibinadamu? (b) Yehova anafanya nini, kwa kutayarishia nini?
10 Mitetemo hiyo katika mambo ya kibinadamu ni matokeo ya kutoweza kwa binadamu kuelekeza hatua zake mwenyewe. (Yeremia 10:23) Zaidi ya hilo, Shetani, nyoka wa zamani, “ambaye anaongoza vibaya dunia nzima yote inayokaliwa,” analeta ole katika jaribio lake la mwisho la kukengeua aina ya binadamu kutoka ibada ya Yehova. Tekinolojia ya ki-siku-hizi imeifanya dunia iwe ndogo kama ujirani mmoja tu, ambapo chuki za kitaifa na za kijamii zinatikisa jamii ya kibinadamu mpaka misingi yayo, nao ule unaoitwa eti Umoja wa Mataifa, hauwezi kupata ponyo lenye kuleta matokeo. Kama isivyopata kuwa hapo zamani, mwanadamu anatawala mwanadamu kwa umizo lake. (Ufunuo 12:9, 12; Mhubiri 8:9, NW) Hata hivyo, Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu, Mfanyiza mbingu na dunia, amekuwa akifanya aina yake mwenyewe ya utikisaji kwa karibu miaka 90, katika kujitayarishia kutatua matatizo ya dunia mara moja na kwa wakati wote. Jinsi gani hivyo?
11. (a) Ni mtikiso gani unaoelezwa katika Hagai 2:6, 7? (b) Unabii wa Hagai unatimizwaje?
11 Kwenye Hagai 2:6, 7, NW, tunasoma hivi: “Kwa kuwa hivi ndivyo Yehova wa majeshi amesema, ‘Bado mara moja—ni kitambo kidogo—na mimi ninatikisa mbingu na dunia na bahari na nchi kavu. Na mimi nitatikisa mataifa yote, na vitu vyenye kutamanika vya mataifa yote lazima vije ndani; na mimi nitajaza nyumba hii utukufu,’ Yehova wa majeshi amesema.” Tangu 1919 hasa, Yehova amefanya mashahidi wake wapige mbiu ya hukumu zake miongoni mwa elementi zote za jamii ya kibinadamu duniani. Mfumo wa ulimwengu wa Shetani umetahadharishwa kwa onyo la pote katika tufe.d Kadiri onyo hilo linavyopata nguvu, binadamu wenye kumhofu Mungu, vile “vitu vyenye kutamanika,” wamechochewa wajitenge na mataifa. Si kwamba wanatikiswa na kule kutetemeshwa katika tengenezo la Shetani. Lakini wanapotambua hali, wao wanafanya uamuzi wao wenyewe washiriki pamoja na jamii ya Yohana yenye kupakwa mafuta katika kuijaza utukufu nyumba ya Yehova ya ibada. Hilo linatimizwaje? Kwa kazi ya bidii ya kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu uliosimamishwa. (Mathayo 24:14) Ufalme huu, ambao washiriki wao ni Yesu na wafuasi wake wapakwa-mafuta, utaendelea kusimama daima kwa utukufu wa Yehova ukiwa “ufalme usioweza kutikiswa.”—Waebrania 12:26-29, NW.
12. Ikiwa wewe umeanza kuitikia kazi ya kuhubiri iliyotabiriwa kwenye Mathayo 24:14, inakupasa wewe ufanye nini kabla halijatokea lile tetemeko la dunia kubwa la Ufunuo 6:12?
12 Je! wewe ni mmoja ambaye ameanza kuitikia kuhubiri huko? Je! pengine wewe ni mmoja wa wale mamilioni ambao katika miaka ya karibuni wamehudhuria Ukumbusho wa kifo cha Yesu? Ikiwa ndivyo, zidi kufanya maendeleo katika funzo lako la ukweli wa Biblia. (2 Timotheo 2:15; 3:16, 17) Acha kabisa ule mtindo wa maisha wenye ufisadi wa jamii ya kidunia ya Shetani iliyohukumiwa maangamizi! Njoo na kuingia mpaka ndani ya jamii ya ulimwengu mpya ya Kikristo na ushiriki kikamili katika utendaji wayo kabla ya lile “tetemeko la dunia” la mwisho lenye kuleta uharibifu halijavunja vipande vipande ulimwengu wote wa Shetani. Lakini ni nini hilo tetemeko la dunia kubwa? Acheni tuone sasa.
Lile Tetemeko la Dunia Kubwa!
13. Ni kwa njia gani hilo tetemeko la dunia kubwa ni ono jipya kabisa kwa binadamu?
13 Ndiyo, hizi siku za mwisho zenye hatari zimekuwa wakati wa matetemeko ya dunia—halisi na ya kitamathali. (2 Timotheo 3:1) Lakini hapana mojapo matetemeko haya ambalo ndilo ule mtikiso mkubwa wa mwisho ambao Yohana anaona wakati wa kufunguliwa kwa kifungo cha sita. Wakati wa mitetemo ya utangulizi umekwisha. Linakuja sasa tetemeko la dunia kubwa ambalo ni jipya kabisa kuonwa na aina ya binadamu. Ni tetemeko kubwa sana hivi kwamba mitetemo na misukosuko linayosababisha haiwezi kupimwa kwa kipima-tetemeko cha Richter au kwa kipimo kinginecho cha kibinadamu. Hili si mshtuo wa mahali tu bali mtikiso wenye msiba mkubwa ambao unakumba “dunia” nzima yote, yaani, jamii yote ya kibinadamu iliyo fasiki.
14. (a) Ni unabii gani ambao hutabiri tetemeko la dunia kubwa na matokeo yalo? (b) Ni lazima unabii wa Yoeli na Ufunuo 6:12, 13 urejezee nini?
14 Wengine wa manabii wa Yehova walitabiri tetemeko la dunia kama hilo na matokeo yalo yenye kuleta uharibifu. Mathalani, yapata 820 K.W.K., Yoeli alisema juu ya “kuja kwa siku kuu na yenye kuvuvia hofu ya Yehova,” akitaarifu kwamba ndipo “jua lenyewe litageuzwa kuwa giza, na mwezi kuwa damu.” Baadaye, yeye anaongezea maneno haya: “Halaiki za watu, halaiki za watu zimo katika bonde la uamuzi, kwa kuwa siku ya Yehova i karibu katika uwanda-bonde wa uamuzi. Jua na mwezi vyenyewe kwa hakika vitakuwa vyenye giza, na nyota zenyewe hakika zitaondoa uangavu wazo. Na kutoka Sayuni Yehova mwenyewe atanguruma, na kutoka Yerusalemu yeye atatoa nje sauti yake. Na mbingu na dunia kwa hakika zitatikiswa; lakini Yehova atakuwa kimbilio kwa ajili ya watu wake, na ngome kwa ajili ya wana wa Israeli.” (Yoeli 2:31; 3:14-16, NW) Kutikiswa huku kungetumika kuhusu tu kutekelezwa kwa hukumu ya Yehova wakati wa dhiki kubwa. (Mathayo 24:21) Kwa hiyo lile simulizi mlingano kwenye Ufunuo 6:12, 13 kimantiki lingetumika jinsi iyo hiyo.—Ona pia Yeremia 10:10; Sefania 1:14, 15.
15. Ni mtikiso gani wenye nguvu aliotabiri nabii Habakuki?
15 Yapata miaka 200 baada ya Yoeli, nabii Habakuki alisema na Mungu katika sala hivi: “O Yehova mimi nimesikia ripoti juu yako wewe. Mimi nimeogopa, O Yehova, utendaji wako. Katikati ya miaka O ulete kwenye uhai! Katikati ya miaka wewe na uufanye ujulikane. Wakati wa msukosuko, kuonyesha rehema wewe na ukumbuke.” Huo “msukosuko” ungekuwa nini? Habakuki anaendelea kutoa elezo dhahiri sana la dhiki kubwa, akisema kwa habari ya Yehova: “Yeye alisimama tuli, ili apate kutikisa dunia. Yeye aliona, na kisha akasababisha mataifa kuruka. . . . Pamoja na shutumu wewe ulienda ukipiga miguu kupitia dunia. Katika kasirani wewe ulienda ukiyapura mataifa. Hata hivyo, kwa habari yangu mimi, mimi nitachachawa katika Yehova mwenyewe; mimi nitakuwa mwenye shangwe katika Mungu wa wokovu wangu.” (Habakuki 3:1, 2, 6, 12, 18, NW) Lo! ni mtikiso wenye nguvu kama nini ambao Yehova atasababisha katika dunia yote wakati yeye atakapoyapura mataifa!
16. (a) Ni nini analotabiri nabii Ezekieli kwa ajili ya wakati ambao Shetani anafanya shambulio lake la mwisho juu ya watu wa Mungu? (b) Ni nini linalotokana na tetemeko la dunia kubwa la Ufunuo 6:12?
16 Ezekieli alitabiri kwamba wakati Gogu wa Magogu (Shetani aliyetwezwa) anapofanya shambulio la mwisho juu ya watu wa Mungu, Yehova atasababisha “tetemeko kubwa” litukie “katika udongo wa Israeli.” (Ezekieli 38:18, 19, NW) Ingawa huenda matetemeko ya dunia halisi yakahusika, inatupasa sisi kukumbuka kwamba Ufunuo umetolewa kwa ishara. Unabii huu pamoja na unabii mwingine uliotajwa ni wa ufananisho kabisa. Kwa sababu hiyo, kufunguliwa kwa kifungo cha sita inaelekea kunafunua ule upeo wa mitikiso yote ya huu mfumo wa mambo wa kidunia—lile tetemeko la dunia kubwa ambalo katika hilo binadamu wote wanaopinga enzi kuu ya Yehova Mungu wanaharibiwa.
Wakati wa Giza
17. Hilo tetemeko la dunia kubwa linaathirije jua, mwezi, na nyota?
17 Kama vile Yohana aendeleavyo kuonyesha, tetemeko la dunia kubwa linaandamana na matukio yenye kuogofya ambayo yanahusu hata mbingu. Yeye anasema: “Nalo jua likawa jeusi kama gunia la nywele, na mwezi mzima wote ukawa kama damu, na nyota zote za mbingu zikaanguka kwenye dunia, kama vile wakati mtini unapotikiswa na upepo mkali hurusha tini zao zisizoiva.” (Ufunuo 6:12b, 13, NW) Ni kituko chenye kugutusha kama nini! Je! wewe unaweza kuwazia giza lenye kuogopesha ambalo lingetokea kama unabii huo ungetimizwa kihalisi? Hakungekuwa tena na nuru ya jua yenye joto na yenye kufariji mchana! Hakungekuwa tena na nuru ya mwezi ya kirafiki na yenye rangi ya fedha usiku! Na zile miriadi za nyota hazingemetameta dhidi ya kisetiri-nyuma cha kimahameli cha anga. Badala ya hivyo, kungekuwa na weusi ti, wenye baridi, usiokoma.—Linga Mathayo 24:29.
18. Ni katika njia gani ‘mbingu zilipata kuwa zenye giza’ kwa ajili ya Yerusalemu katika 607 K.W.K.?
18 Katika maana ya kiroho, giza kama hilo lilitolewa unabii kwa Israeli wa kale. Yeremia alionya hivi: “Ukiwa mtupu ndivyo bara kwa ujumla litakuja kuwa, na je! mimi sitatimiza uharibifu kabisa? Kwa sababu hiyo bara litaomboleza, na mbingu zilizo juu zitakuwa giza.” (Yeremia 4:27, 28, NW) Katika 607 K.W.K. wakati unabii huo ulipotimizwa, mambo yalikuwa yenye giza kweli kweli kwa watu wa Yehova. Yerusalemu, jiji lao kuu, lilianguka kwa Wababuloni. Hekalu lao liliharibiwa, na bara lao likaachwa ukiwa. Kwa wao, hakukuwa na nuru yenye kufariji kutoka mbingu. Badala, ilikuwa kama vile Yeremia alivyoambia Yehova kwa kuomboleza: “Wewe umeua; wewe hukuonyesha huruma. Umefunga ufikio kwako wewe kwa tungamo la wingu, kwamba sala isipate kupenya.” (Maombolezo 3:43, 44, NW) Kwa Yerusalemu, giza hilo la kimbingu lilimaanisha kifo na uharibifu.
19. (a) Isaya, nabii wa Mungu anaelezaje habari ya giza katika mbingu juu ya Babuloni wa kale? (b) Ni wakati gani na jinsi gani unabii wa Isaya ulitimizwa?
19 Baadaye, giza linalofanana na hilo katika mbingu liliashiria uharibifu kwa Babuloni wa kale. Kwa habari ya hilo, nabii wa Mungu alivuviwa aandike hivi: “Tazama! Siku ya Yehova yenyewe inakuja, katili kwa kiruu na kasirani yenye kuwaka pia, ili kufanya bara liwe kitu cha mshangao, na kwamba iweze kutowesha wafanya dhambi wa bara kutoka kwayo. Kwa kuwa nyota zenyewe za zile mbingu na makundi ya Kesili yazo hazitameremesha nuru yazo; kwa hakika jua litakuwa giza wakati wa kutokea kwalo, na mwezi wenyewe hautafanya nuru yao kuangaza. Na mimi kwa hakika nitaonyesha wazi ubaya walo lenyewe juu ya bara lenye kuzaa, na kosa lao wenyewe juu ya waovu wenyewe.” (Isaya 13:9-11, NW) Unabii huu ulitimizwa katika 539 K.W.K. wakati Babuloni ilipoanguka kwa Wamedi na Waajemi. Unaeleza vizuri ule weusi ti, ule utotumaini, ule ukosefu wa nuru ya faraja kwa Babuloni ilipokuwa ikianguka milele kutoka cheo chayo cha kuwa serikali kuu ya ulimwengu.
20. Ni tokeo gani lenye kuhofisha linalongojea huu mfumo wa mambo wakati tetemeko la dunia kubwa linapopiga?
20 Kwa njia iyo hiyo, wakati tetemeko la dunia kubwa linapopiga, mfumo wote huu wa ulimwengu utagharikishwa katika tamausho la giza tititi. Vile vimeti viangavu, vyenye kung’aa vya mfumo wa kidunia wa Shetani havitatoa miale ya tumaini. Tayari leo, viongozi wa kisiasa wa dunia, hasa katika Jumuiya ya Wakristo, wana sifa mbaya sana kwa sababu ya ufisadi wao, kusema uwongo na mtindo wao wa maisha wa utovu wa adili. (Isaya 28:14-19) Hawawezi kuitibariwa tena. Nuru yao yenye kusinzia itapatwa na giza kabisa Yehova atekelezapo hukumu. Uvutano wao ulio kama mwezi juu ya mambo ya dunia utafunuliwa kuwa umetiwa damu, wenye kuleta kifo. Nyota zao mashuhuri za kilimwengu zitazimwa kama vimondo viangukavyo ghafula na zitatawanywa kama tini zisizoiva katika upepo-dhoruba wenye kuvuma. Tufe letu lote litatetemeka chini ya “dhiki kubwa kama ambayo haijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka sasa, la, wala haitatukia tena.” (Mathayo 24:21, NW) Lo! ni tazamio lenye kujaa hofu kama nini!
“Mbingu” Yaondoka
21. Katika njozi yake, Yohana anaona nini kuhusu “mbingu” na “kila mlima na kila kisiwa”?
21 Njozi ya Yohana inaendelea: “Na mbingu ikaondoka kama hati-kunjo inayokunjwa, na kila mlima na kila kisiwa viliondolewa mahali pavyo.” (Ufunuo 6:14, NW) Kwa wazi hizi si mbingu halisi au milima na visiwa halisi. Lakini hizo zinafananisha nini?
22. Katika Edomu ni aina gani za “mbingu” ‘zilizokunjwa, kama hati-kunjo’?
22 Kwa habari ya “mbingu,” sisi tunasaidiwa katika uelewevu wetu na unabii unaofanana na huo unaosema juu ya hasira kali ya Yehova dhidi ya mataifa: “Na wale wote wa lile jeshi la zile mbingu lazima waozee mbali. Na zile mbingu lazima zikunjwe kama hati-kunjo.” (Isaya 34:4, NW) Hasa Edomu lazima akione. Jinsi gani? Alishambuliwa na Wababuloni muda mfupi baada ya uharibifu wa Yerusalemu katika 607 K.W.K. Wakati huo, hakuna matukio yenye kutokeza yaliyorekodiwa kuwa yakitukia katika mbingu halisi. Lakini yalikuwako matukio yenye kuleta uharibifu katika “mbingu” za Edomu.e Mamlaka zake za serikali za kibinadamu zilishushwa kutoka cheo chazo kilichoinuliwa, mfano wa mbingu. (Isaya 34:5) ‘Zilikunjwa’ zikawa kana kwamba zimewekwa kando, kama hati-kunjo kuukuu ambayo haina matumizi yoyote tena kwa yeyote.
23. Ni “mbingu” gani ‘itakayoondoka kama hati-kunjo,’ nayo maneno ya Petro yanathibitishaje uelewevu huu?
23 Hivyo, “mbingu” inayopaswa ‘kuondoka kama hati-kunjo’ hurejeza kwenye serikali zinazopinga Mungu ambazo hutawala juu ya dunia hii. Hizo zitaondolewa kwa ukomo na yule Mpandaji-farasi mweupe. (Ufunuo 19:11-16, 19-21) Hilo linathibitishwa na aliyosema mtume Petro wakati alipotazama mbele kwenye matukio yaliyoashiriwa na kule kufunguliwa kwa kifungo cha sita: “Mbingu na dunia zilizopo sasa zimewekwa akiba kwa moto na zimehifadhiwa kwa ajili ya siku ya hukumu na ya uharibifu wa watu wasiohofu Mungu.” (2 Petro 3:7, NW) Lakini namna gani usemi huu, “kila mlima na kila kisiwa viliondolewa mahali pavyo”?
24. (a) Katika unabii wa Biblia, ni wakati gani inaposemwa kwamba milima na visiwa vinatikiswa au kuondolewa uimara? (b) ‘Milima ilitikisikaje’ wakati Ninawi ulipoanguka?
24 Katika unabii wa Biblia, milima na visiwa vinasemwa kuwa vinatikiswa au kuondolewa uimara wakati wa mabadiliko makubwa ya kisiasa. Mathalani, wakati wa kutabiri hukumu za Yehova dhidi ya Ninawi, nabii Nahumu aliandika: “Milima yenyewe imetikisika kwa ajili ya yeye, na vilima halisi vikajikuta vyenyewe vikiyeyuka. Nayo dunia itapinduliwa kwa sababu ya uso wake.” (Nahumu 1:5, NW) Hakuna maandishi yanayoonyesha kuvunjika kokote kwa milima halisi wakati Ninawi ulipoanguka kikweli katika 632 K.W.K. Lakini serikali kubwa ya ulimwengu ambayo hapo kwanza ilionekana kuwa kama mlima katika imara yayo ilianguka ghafula.—Linga Yeremia 4:24.
25. Kwenye ule mwisho unaokuja wa huu mfumo wa mambo, “kila mlima na kila kisiwa” vitaondolewaje mahali pavyo?
25 Kwa hiyo, kimantiki “kila mlima na kila kisiwa” kama inavyorejezewa mwanzoni mwa kufunguliwa kwa kifungo cha sita vingekuwa serikali za kisiasa na matengenezo yanayozitegemea ya ulimwengu huu ambazo zimeonekana kuwa imara sana kwa wengi wa aina ya binadamu. Zitatikiswa zitoke mahali pazo, kwa fadhaa na hofu ya wale ambao hapo kwanza waliziitibari. Kama vile unabii huo uendeleavyo kusimulia, hakutakuwa na shaka lolote kwamba ile siku kubwa ya hasira-kisasi ya Yehova na Mwana wake—lile tetemeko la mwisho kabisa ambalo linaondoa matengenezo yote ya Shetani—imekuja ikiwa na kisasi!
“Angukeni Juu ya Sisi na Kuficha Sisi”
26. Binadamu wanaopinga enzi kuu ya Mungu watatendaje katika hofu yao, na ni maneno gani ya hofu kuu watakayotamka?
26 Maneno ya Yohana yanaendelea: “Na wafalme wa dunia na wenye vyeo vya juu na makamanda wa kivita na matajiri na makamambe na kila mtumwa na kila mtu huru wakajificha wenyewe katika mapango na katika yale matungamo-miamba ya milima. Na wao walifuliza kusema kwa milima na kwa matungamo-miamba: ‘Angukeni juu ya sisi na kuficha sisi kutoka uso wa yule Mmoja aliyeketi juu ya kiti cha ufalme na kutoka hasira-kisasi ya Mwana-Kondoo, kwa sababu siku kubwa ya hasira-kisasi yao imekuja, na ni nani anaweza kusimama?’”—Ufunuo 6:15-17, NW.
27. Ni vilio gani vilivyotamkwa na Waisraeli wasio waaminifu wa Samaria, na maneno hayo yalitimizwaje?
27 Wakati Hosea alipokuwa akitamka hukumu ya Yehova juu ya Samaria, jiji kuu la ufalme wa kaskazini wa Israeli, yeye alisema hivi: “Sehemu za juu za Beth-aveni, dhambi ya Israeli, kwa kweli zitatoweshwa kabisa. Miiba na mibigili yenyewe itapanda juu ya madhabahu yao. Na kwa hakika watu watasema kwa milima yenyewe, ‘Funikeni sisi!’ na kwa vilima, ‘Angukeni juu ya sisi!’” (Hosea 10:8, NW) Maneno haya yalitimizwaje? Basi, wakati Samaria lilipoanguka kwa Waashuri wakatili katika 740 K.W.K. hapakuwa na mahali pa Waisraeli kukimbilia. Maneno ya Hosea huonyesha hisia ya utotumaini, hofu tupu, na kuachwa walikohisi watu hao walioshindwa. Wala vilima halisi wala matengenezo ya Samaria yaliyokuwa kama milima hayangeweza kuwapa himaya, hata ingawa yalikuwa yameonekana kuwa ya kudumu sana wakati uliopita.
28. (a) Ni onyo gani ambalo Yesu aliwapa wanawake wa Yerusalemu? (b) Onyo la Yesu lilitimizwaje?
28 Hali moja na hiyo, Yesu alipokuwa akipelekwa na askari-jeshi Waroma kwenye kifo, yeye alihutubia wanawake wa Yerusalemu na kusema: “Siku zinakuja ambazo katika hizo watu watasema, ‘Wenye furaha ni wale wanawake walio tasa, na matumbo-uzazi ambayo hayakuzaa na matiti ambayo hayakunyonyesha!’ Ndipo wataanza kusema kwa milima, ‘Angukeni juu ya sisi!’ na kwa vilima, ‘Funikeni sisi!’” (Luka 23:29, 30, NW) Ule uharibifu wa Yerusalemu ulioletwa na Waroma katika 70 W.K. umethibitishwa vizuri kimaandishi, na ni wazi kwamba maneno ya Yesu yana maana inayofanana na ile ya maneno ya Hosea. Wakati ule hapakuwa na mahali pa kujificha kwa Wayahudi ambao walikuwa wamebaki katika Yudea. Kokote walikojaribu kujificha katika Yerusalemu, au hata wakati walipokimbilia ngome ya Masada juu ya mlima, wao hawakuweza kuepuka wonyesho wenye jeuri wa hukumu ya Yehova.
29. (a) Wakati siku ya Yehova ya hasira-kisasi inapokuja, ni nini kitakachopata wale ambao wamejitoa kuunga mkono huu mfumo wa mambo? (b) Ni unabii gani wa Yesu utakaotimizwa wakati Yehova anapoonyesha hasira-kisasi Yake?
29 Sasa, kule kufunguliwa kwa kifungo cha sita kumeonyesha kwamba kitu fulani kama hicho kitatukia wakati wa siku inayokuja ya hasira-kisasi ya Yehova. Wakati wa kutikiswa kwa mwisho kabisa kwa huu mfumo wa mambo wa kidunia, wale waliojitoa kuuunga mkono watatafuta sana mahali pa kujificha, lakini hawatapata hata pamoja. Dini bandia, Babuloni Mkubwa, tayari imeshindwa vya kusikitisha sana kuwasaidia. Wala mapango katika milima halisi wala matengenezo ya kisiasa na ya kibiashara yaliyo mfano wa milima hayataandaa usalama wa kifedha au msaada mwingine wa aina yoyote. Hakuna kitu kitakachowakinga wasipatwe na hasira-kisasi ya Yehova. Hofu yao imeelezwa vizuri na Yesu: “Ndipo ishara ya Mwana wa binadamu itaonekana katika mbingu, na ndipo makabila yote ya dunia yatajipigapiga yenyewe kwa ombolezo, na yataona Mwana wa binadamu akija juu ya mawingu ya mbingu akiwa na nguvu na utukufu mkubwa.”—Mathayo 24:30, NW.
30. (a) Ni nini kinachodokezwa na swali hili: “Ni nani anaweza kusimama?” (b) Je! wowote wataweza kusimama wakati wa hukumu ya Yehova?
30 Ndiyo, wale ambao wamekataa kutambua mamlaka ya yule Mpandaji-farasi mweupe mwenye ushindi watalazimika kukubali kosa lao. Wanadamu ambao kwa kupenda wamekuwa mbegu ya yule nyoka wataelekeana na uharibifu wakati ulimwengu wa Shetani unapopitilia mbali. (Mwanzo 3:15; 1 Yohana 2:17) Hali ya ulimwengu kwenye wakati huo itakuwa ya aina ya kwamba, ni kana kwamba wengi watakuwa wakiuliza: “Ni nani anaweza kusimama?” Yaonekana kama watadhani hakuna yeyote kwa vyovyote ambaye anaweza kusimama akiwa anakubalika mbele za Mungu katika siku hiyo ya hukumu yake. Lakini watakuwa wenye kukosea, kama vile kitabu cha Ufunuo kinavyoendelea kuonyesha.
[Maelezo ya Chini]
a Matetemeko ya dunia halisi mara nyingi hutanguliwa na misukosuko yenye mtutumo ambayo husababisha mbwa kubweka au kutenda bila kutulia na hutaharakisha wanyama wengine na samaki, ingawa huenda wanadamu wasishuku mpaka tetemeko lenyewe linapopiga.—Ona Amkeni (Kiingereza), Julai 8, 1982, ukurasa 14.
b Ili kupata maelezo zaidi, ona kurasa 22, 24.
c Kwa zaidi ya miaka 35, kutoka 1895 mpaka 1931, maneno ya Luka 21:25, 28, 31 yalinukuliwa yakawekwa kwenye jalada la gazeti Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) dhidi ya kisetiri-nyuma cha mnara wa taa ukimulikia anga zenye dhoruba juu ya bahari yenye mchafuko.
d Mathalani, katika kampeni ya pekee katika 1931, Mashahidi wa Yehova binafsi walipelekea viongozi wa kidini, wanasiasa, na wafanya-biashara kotekote duniani, maelfu mengi ya kijitabu The Kingdom, the Hope of the World.
e Katika tumizi kama hilo la neno “mbingu,” unabii wa “mbingu mpya” katika Isaya 65:17, 18 ulikuwa na utimizo wao wa kwanza katika ule mfumo mpya wa kiserikali, uliohusu Gavana Zerubabeli na Kuhani Mkuu Yeshua, uliosimamishwa katika Bara la Ahadi baada ya Waisraeli kurudi kutoka uhamisho wa Kibabuloni.—2 Nyakati 36:23; Ezra 5:1, 2; Isaya 44:28.
-
-
Kutia Muhuri Israeli wa MunguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 19
Kutia Muhuri Israeli wa Mungu
Njozi ya 4—Ufunuo 7:1-17
Habari: Wale 144,000 watiwa muhuri, na umati mkubwa unaonwa umesimama mbele ya kiti cha ufalme cha Yehova na mbele ya Mwana-Kondoo
Wakati wa utimizo: Tangu kuketishwa katika kiti cha ufalme kwa Kristo Yesu katika 1914 na kuendelea kuingia Utawala wa Mileani wake
1. “Ni nani anaweza kusimama” wakati wa siku kubwa ya hasira-kisasi ya kimungu?
“NI NANI anaweza kusimama?” (Ufunuo 6:17, NW) Ndiyo, ni nani kweli kweli? Wakati siku kubwa ya hasira-kisasi ya kimungu inapokumba mfumo wa Shetani, watawala na watu wa ulimwengu huenda kwa kufaa wakauliza swali hilo. Itaonekana kwao kwamba kumbo hilo kubwa linalokuja litazima uhai wote wa kibinadamu. Lakini je! litafanya hivyo? Kwa furaha, nabii wa Mungu anatuhakikishia: “Kila mmoja ambaye anaita juu ya jina la Yehova ataponyoka akiwa salama.” (Yoeli 2:32, NW) Mitume Petro na Paulo wathibitisha uhakika huo. (Matendo 2:19-21; Warumi 10:13) Ndiyo, wale wanaoita juu ya jina la Yehova watakuwa waokokaji. Hao ni akina nani? Kadiri njozi inayofuata ikunjulikavyo, sisi tutaona.
2. Ni kwa nini ni jambo la kushangaza kwamba kutakuwa na waokokaji wa siku ya hukumu ya Yehova?
2 Kwa kweli ni jambo lenye kushangaza kwamba yapasa yeyote apitie siku ya Yehova ya hukumu akiwa hai, kwa kuwa mwingine wa manabii wa Mungu anaieleza kwa maneno haya: “Tazama! Upepo-dhoruba wa Yehova, hasira kali yenyewe, imetoka ikaenda nje, tufani yenye kwenda mbele ikifagia. Juu ya kichwa cha waovu itazunguka vuruvuru. Kasirani yenye kuwaka ya Yehova haitarudi nyuma mpaka yeye awe ameua na mpaka yeye awe ametekeleza mawazo ya moyo wake.” (Yeremia 30:23, 24, NW) Ni jambo la uharaka kwamba sisi tuchukue hatua za kusalimika katika dhoruba hiyo!—Mithali 2:22; Isaya 55:6, 7; Sefania 2:2, 3.
Zile Pepo Nne
3. (a) Ni utumishi gani wa pekee unaofanywa na malaika anaouona Yohana? (b) Ni nini kinachofananishwa na “pepo nne”?
3 Kabla ya Yehova kuachilia kiruu hiki, malaika wa kimbingu wanafanya utumishi wa pekee. Sasa Yohana anaona hilo katika njozi: “Baada ya hili mimi niliona malaika wanne wakisimama juu ya kona nne za dunia, wakishika sana pepo nne za dunia, kwamba upepo wowote usipate kupuliza juu ya dunia au juu ya bahari au juu ya mti wowote.” (Ufunuo 7:1, NW) Hili linamaanisha nini kwa sisi leo? Hizi “pepo nne” ni ufananisho halisi wa hukumu yenye kuharibu inayokaribia kuachiliwa juu ya jamii mbovu ya kidunia, juu ya “bahari” yenye kusukasuka ya binadamu waasi-sheria, na juu ya watawala walioinuka mfano wa miti ambao wanapata uungaji-mkono na utegemezo kutoka kwa watu wa dunia.—Isaya 57:20; Zaburi 37:35, 36.
4. (a) Malaika wanne wanawakilisha nini? (b) Tokeo linakuwa nini juu ya tengenezo la kidunia la Shetani wakati pepo nne zinapoachiliwa?
4 Hapana shaka, hawa malaika wanne wanawakilisha vikundi vinne vya kimalaika, ambavyo Yehova anatumia kuzuia utekelezo wa hukumu yake mpaka wakati uliowekwa. Malaika hao waachiliapo pepo nne za hasira-kisasi zizunguke vuruvuru wakati ule ule mmoja kutoka kaskazini, kusini, mashariki, na magharibi, kumbo hilo litakuwa kubwa mno. Litafanana, lakini kwa kadiri kubwa mno, na utumiaji wa Yehova wa pepo nne kutawanya Waelamu, akiwavunjavunja na kuwaulia mbali kabisa. (Yeremia 49:36-38) Itakuwa dhoruba ya upepo mkubwa mno yenye kukumba zaidi ya ile “tufani” ambayo kwayo Yehova alifutilia mbali taifa la Amoni. (Amosi 1:13-15, NW) Hakuna sehemu ya tengenezo la Shetani duniani ambayo itaweza kusimama katika siku ya kiruu cha Yehova, wakati yeye anapotetea enzi kuu yake kwa umilele wote utakaokuja.—Zaburi 83:15, 18; Isaya 29:5, 6.
5. Unabii wa Yeremia unatusaidiaje kuelewa kwamba hukumu za Mungu zitaenea dunia yote nzima?
5 Je! sisi tunaweza kuwa na hakika kwamba hukumu za Yehova zitakumba dunia nzima? Sikiliza tena nabii wake Yeremia: “Tazama! Afa moja linaenda kutoka taifa moja kwenda kwenye jingine, na tufani kubwa yenyewe itaamshwa juu kutoka sehemu za mbali zaidi sana za dunia. Na wale wenye kuuawa na Yehova kwa hakika watakuja kuwa katika siku hiyo kutoka mwisho mmoja wa dunia hadi kufika mwisho mwingine kabisa wa dunia.” (Yeremia 25:32, 33, NW) Ni wakati wa dhoruba hii yenye tufani kwamba giza litagharikisha ulimwengu huu. Mawakili wao wenye kutawala watatikiswa waingie ndani ya utowesho. (Ufunuo 6:12-14) Lakini wakati ujao hautakuwa wenye giza kwa kila mmoja. Basi, ni kwa ajili ya nani zile pepo nne zinazuiwa?
Kuwatia Muhuri Watumwa wa Mungu
6. Ni nani anayeambia malaika wazuie pepo nne, na hilo linaruhusu wakati kwa ajili ya nini?
6 Yohana anaendelea kueleza jinsi baadhi ya watu wanavyotiwa alama kwa ajili ya kuokoka, akisema: “Na mimi nikaona malaika mwingine akipanda juu kutoka kwenye zukio la jua, akiwa na muhuri wa Mungu anayeishi; na yeye alilia kwa sauti kubwa kwa wale malaika wanne ambao kwao ruhusa ilipewa ya kudhuru dunia na bahari, akisema: ‘Msidhuru dunia au bahari au miti, mpaka baada ya sisi tuwe tumetia muhuri watumwa wa Mungu wetu katika vipaji vya nyuso zao.’”—Ufunuo 7:2, 3, NW.
7. Ni nani hasa aliye malaika wa tano, na ni ithibati gani inayotusaidia tuthibitishe utambulisho wake?
7 Ingawa huyu malaika wa tano hatajwi jina, ithibati yote inaonyesha kwamba lazima awe Bwana Yesu aliyetukuzwa. Kupatana na kuwa kwa Yesu Malaika Mkuu, yeye anaonyeshwa hapa akiwa na mamlaka juu ya wale malaika wengine. (1 Wathesalonike 4:16; Yuda 9) Yeye anapanda juu kutoka mashariki, kama “wafalme kutoka zukio la jua”—Yehova na Kristo wake—ambao wanakuja kutekeleza hukumu, kama walivyofanya wafalme Dario na Sairasi wakati waliponyenyekeza Babuloni wa kale. (Ufunuo 16:12; Isaya 45:1; Yeremia 51:11; Danieli 5:31, NW) Malaika huyu anashabihi Yesu katika njia ya kwamba yeye ameaminishwa kazi ya kutia muhuri Wakristo wapakwa-mafuta. (Waefeso 1:13, 14) Na zaidi, wakati pepo zinapoachiliwa, ni Yesu anayeongoza majeshi ya kimbingu katika kutekeleza hukumu juu ya mataifa. (Ufunuo 19:11-16) Basi, kimantiki, Yesu angekuwa ndiye wa kuamuru kwamba uharibifu kwa tengenezo la kidunia la Shetani uzuiwe mpaka watumwa wa Mungu wawe wametiwa muhuri.
8. Kutia muhuri ni nini, nako kulianza wakati gani?
8 Huku kutia muhuri ni nini, na hawa watumwa wa Mungu ni nani? Kutia muhuri huku kulianza katika Pentekoste 33 W.K. wakati Wakristo Wayahudi wa kwanza walipopakwa mafuta kwa roho takatifu. Baadaye, Mungu aliendelea kuita na kupaka mafuta “watu wa mataifa.” (Warumi 3:29; Matendo 2:1-4, 14, 32, 33; 15:14, NW) Mtume Paulo aliandika juu ya Wakristo wapakwa-mafuta wakiwa na uhakikisho wa kwamba wao ‘ni wa Kristo’ na akaongeza kwamba Mungu “pia ametia muhuri wake juu yetu na ametupa sisi dalili ya kitu ambacho kitakuja, yaani, roho, katika mioyo yetu.” (2 Wakorintho 1:21, 22; linga Ufunuo 14:1, NW.) Hivyo, wakati watumwa hawa wanapolelewa kuwa wana wa kiroho wa Mungu, wanapokea dalili yenye kutangulia urithi wao wa kimbingu—muhuri au rehani. (2 Wakorintho 5:1, 5; Waefeso 1:10, 11) Ndipo wanapoweza kusema: “Roho yenyewe hutoa ushuhuda pamoja na roho yetu kwamba sisi tu watoto wa Mungu. Ikiwa, basi, sisi ni watoto, sisi ni warithi pia: warithi kweli kweli wa Mungu, lakini warithi washirika pamoja na Kristo, iwapo sisi tunateswa pamoja ili kwamba sisi tuweze pia kutukuzwa pamoja.”—Waroma 8:15-17, NW.
9. (a) Ni uvumilivu gani unaotakwa upande wa mabaki ya wana wa Mungu waliozaliwa kwa roho? (b) Kutahiniwa kwa wale wapakwa-mafuta kutaendelea mpaka lini?
9 “Iwapo sisi tunateswa pamoja”—hiyo inamaanisha nini? Ili kupokea taji la uhai, Wakristo wapakwa-mafuta lazima wavumilie, wakiwa waaminifu mpaka kifo. (Ufunuo 2:10) Si shauri la ‘wakiisha okolewa, wanaokolewa daima.’ (Mathayo 10:22; Luka 13:24) Badala ya hivyo, wao wanapewa onyo hili la upole: “fanyeni yoteyote mwezayo mfanye kuitwa na kuchaguliwa kwa nyinyi kuwe hakika kwa ajili yenu wenyewe.” Kama vile mtume Paulo, mwishowe kabisa ni lazima wao waweze kusema: “Mimi nimepiga vita nzuri, mimi nimekimbia katika shindano mpaka mwisho, mimi nimeshika imani.” (2 Petro 1:10, 11; 2 Timotheo 4:7, 8, NW) Hivyo hapa duniani kule kutahiniwa na kupepetwa kwa yale mabaki ya wana wa Mungu waliozaliwa kwa roho lazima kuendelee mpaka Yesu na malaika wanaoandamana naye wawe wamekwisha kuutia kikiki muhuri ‘katika kipaji cha uso’ wa hawa wote, kuwatambulisha kabisa kabisa, bila kutanguka, kuwa “watumwa wa Mungu wetu” waliojaribiwa na waaminifu. Ndipo muhuri unapokuwa alama ya daima. Kwa wazi, wakati pepo nne za dhiki zinapoachiliwa, Waisraeli wote wa kiroho watakuwa wamekwisha tiwa muhuri kabisa kabisa, hata ingawa wachache watakuwa wangali wanaishi katika mnofu. (Mathayo 24:13; Ufunuo 19:7) Hesabu nzima ya washiriki itakuwa imekamilika!—Warumi 11:25, 26.
Ni Wangapi Wanatiwa Muhuri
10. (a) Ni maandiko gani yanaonyesha kwamba hesabu ya watiwa muhuri ina kikomo? (b) Ni nini jumla ya hesabu iliyotiwa muhuri, na wao wanaorodheshwaje?
10 Yesu aliambia wale waliokuwa katika mstari wa huku kutiwa muhuri: “Msiwe na hofu, kundi dogo, kwa sababu Baba yenu ametoa kibali cha kuwapa nyinyi ufalme.” (Luka 12:32, NW) Maandiko mengine, kama vile Ufunuo 6:11 na Warumi 11:25, huonyesha kwamba hesabu ya hili kundi dogo ina kikomo kweli kweli na, kwa hakika, ilikusudiwa kimbele. Maneno ya Yohana yanayofuata yanathibitisha hili: “Na mimi nikasikia hesabu ya wale ambao walitiwa muhuri, mia na arobaini na nne elfu, waliotiwa muhuri kutoka kila kabila la wana wa Israeli: Kutoka kabila la Yuda elfu kumi na mbili walitiwa muhuri; kutoka kabila la Reubeni elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Gadi elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Asheri elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Naftali elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Manase elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Simeoni elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Lawi elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Isakari elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Zebuloni elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Yosefu elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Benyamini elfu kumi na mbili walitiwa muhuri.”—Ufunuo 7:4-8, NW.
11. (a) Ni kwa nini lile rejezo kwa makabila 12 halingeweza kutumika kuhusu Israeli halisi, wa mnofu? (b) Ni kwa nini Ufunuo huorodhesha makabila 12? (c) Ni kwa nini hakuna kabila ambalo hilo pekee ndilo la kifalme au la kikuhani katika Israeli wa Mungu?
11 Je! hii haingeweza kuwa inarejeza kwa Israeli halisi, wa mnofu? La, kwa kuwa Ufunuo 7:4-8 hutofautiana na ile orodha ya kawaida ya kikabila. (Hesabu 1:17, 47) Kwa wazi, orodha hii hapa si kwa kusudi la kutambulisha Wayahudi wa mnofu kwa makabila yao bali ni kuonyesha muundo wa kitengenezo kama huo kwa Israeli wa kiroho. Hili linasawazika. Wanapaswa waweko washiriki 144,000 wa hili taifa jipya—12,000 kutoka kila mojapo makabila 12. Hakuna kabila katika huyu Israeli wa Mungu ambalo hilo pekee ndilo la kifalme au la kikuhani. Taifa lote kwa ujumla litatawala likiwa wafalme, na taifa lote kwa ujumla litatawala likiwa makuhani.—Wagalatia 6:16; Ufunuo 20:4, 6.
12. Ni kwa nini inafaa kwamba wale wazee 24 wanaimba mbele ya Mwana-Kondoo maneno ya ule wimbo wa Ufunuo 5:9, 10?
12 Ijapokuwa Wayahudi asilia na waongofu wa Kiyahudi walipewa fursa ya kwanza ili wachaguliwe kwa ajili ya kuwa Israeli wa kiroho, ni wachache tu wa taifa hilo walioitikia. Kwa hiyo Yehova aliwatolea mwaliko wale wasio Wayahudi. (Yohana 1:10-13; Matendo 2:4, 7-11; Warumi 11:7) Kama vile kwa habari ya Waefeso, ambao hapo kwanza walikuwa “wametenganishwa na dola la Israeli,” sasa watu wasio Wayahudi wangeweza kutiwa muhuri kwa roho ya Mungu na kuwa sehemu ya kundi la Wakristo wapakwa-mafuta. (Waefeso 2:11-13; 3:5, 6; Matendo 15:14) Basi, inafaa wazee 24 kuimba mbele za Mwana-Kondoo: “Kwa damu yako wewe ulinunua watu kwa ajili ya Mungu kutoka kila kabila na ulimi na kikundi cha watu na taifa, na wewe ulifanya wao kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, nao wanapaswa kutawala wakiwa wafalme juu ya dunia.”—Ufunuo 5:9, 10, NW.
13. Ni kwa nini ilifaa Yakobo ndugu-nusu ya Yesu aandike barua yake “kwa makabila kumi na mawili yaliyotawanyika kotekote”?
13 Kundi la Kikristo ni “jamii teule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu.” (1 Petro 2:9, NW) Likichukua mahali pa Israeli asilia likiwa taifa la Mungu, linakuwa Israeli mpya ambaye ni “‘Israeli’ kikweli.” (Warumi 9:6-8; Mathayo 21:43, NW)a Kwa sababu hii, ilifaa kabisa Yakobo ndugu-nusu ya Yesu aandike barua yake ya kiuchungaji “kwa makabila kumi na mawili yaliyotawanyika kotekote,” yaani, kwa kundi la ulimwenguni pote la Wakristo wapakwa-mafuta ambalo baadaye hesabu yalo ingekuwa 144,000.—Yakobo 1:1, NW.
Israeli wa Mungu Leo
14. Ni nini linaloonyesha kwamba bila ugeugeu Mashahidi wa Yehova wameshikilia kwamba 144,000 ni hesabu halisi ya wale wanaojumlika kuwa Israeli wa kiroho?
14 Kwa kupendeza, Charles T. Russell, alitambua 144,000 kuwa hesabu halisi ya watu mmoja mmoja wanaojumlika kuwa Israeli wa kiroho. Katika The New Creation, Buku 6 la mfululizo wake wa Studies in the Scriptures, kilichotangazwa 1904, yeye aliandika: “Sisi tuna kila sababu kuitikadi kwamba ile hesabu dhahiri, iliyo imara ya wateule [wapakwa-mafuta waliochaguliwa] ni ile ambayo imetaarifiwa mara kadhaa katika Ufunuo (7:4; 14:1); yaani, 144,000 ‘waliokombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu.’” Katika Light, Kitabu cha Kwanza, kilichotangazwa katika 1930 na Wanafunzi wa Biblia, ilitaarifiwa hali kadhalika hivi: “Hivyo washiriki 144,000 wa mwili wa Kristo wako katika kusanyiko wakionyeshwa kuwa wamechaguliwa na kupakwa mafuta, au kutiwa muhuri.” Bila ugeugeu Mashahidi wa Yehova wameshikilia oni la kwamba kihalisi Wakristo wapakwa-mafuta 144,000 wanajumlika kuwa Israeli wa kiroho.
15. Kabla tu ya siku ya Bwana, wanafunzi wa Biblia wenye mioyo myeupe walifikiri Wayahudi asilia wangefurahia nini baada ya Majira ya Mataifa kuisha?
15 Hata hivyo, je! Waisraeli asilia leo hawastahili kadiri fulani ya upendeleo wa pekee? Katika pindi iliyokuwa kabla tu ya siku ya Bwana, wakati wanafunzi wa Biblia wenye mioyo myeupe walipokuwa wakigundua tena nyingi za kweli za msingi za Neno la Mungu, ilidhaniwa kwamba Majira ya Mataifa yakiisha, Wayahudi wangefurahia tena msimamo wenye kibali mbele za Mungu. Hivyo, kitabu cha C. T. Russell The Time Is at Hand (Buku 2 la Studies in the Scriptures), kilichotangazwa 1889, kilitumia Yeremia 31:29-34 kuhusu Wayahudi asilia, na kueleza: “Ulimwengu ni shahidi wa uhakika wa kwamba adhabu ya Israeli chini ya utawala wa wasio Wayahudi imekuwa ikiendelea tangu K.K. [607], kwamba ingali inaendelea, na kwamba hakuna sababu ya kutazamia mtengenezo mpya wa kitaifa upesi zaidi ya M.B. 1914, kile kikomo cha ‘nyakati saba’ zao—miaka 2520.” Ilielekea kwamba wakati huo Wayahudi wangepata urudisho wa kitaifa, na kwa wazi tazamio hilo lilitiwa uangavu 1917, wakati Julisho-Wazi la Balfour lilipoahidi kuunga mkono Uingereza kwa kufanya Palestina kuwa kao la kitaifa kwa ajili ya Wayahudi.
16. Ni jitihada gani walizofanya Mashahidi wa Yehova kufikia Wayahudi asilia wakiwa na ule ujumbe wa Kikristo, na kukawa na tokeo gani?
16 Kufuata vita ya kwanza ya ulimwengu, Palestina ikawa eneo chini ya usimamizi wa Uingereza, na njia ikafunguka Wayahudi warudi kwenye bara hilo. Katika 1948 Dola la kisiasa la Israeli lilitokezwa. Je! hiyo haikuonyesha kwamba Wayahudi walikuwa katika mstari wa kupata baraka za kimungu? Kwa miaka mingi, Mashahidi wa Yehova waliitikadi kwamba ilikuwa hivyo. Hivyo, katika 1925 walitangaza kitabu chenye kurasa 128, Comfort for the Jews. Katika 1929 walitoa buku lenye kuvutia la kurasa 360, Life, ambalo lilikusudiwa livutie Wayahudi na pia lilishughulika na kitabu cha Biblia cha Ayubu. Jitihada kubwa zilifanywa, hasa katika Jiji la New York, kufikia Wayahudi kwa huu ujumbe wa Kimesiya. Kwa furaha, watu wachache mmoja mmoja waliitikia, lakini Wayahudi kwa ujumla, kama babu zao wa karne ya kwanza, waliikataa ithibati ya kuwapo kwa Mesiya.
17, 18. Watumwa wa Mungu walikuja kuelewa nini kuhusu agano jipya na unabii wa Biblia wa urudisho?
17 Ilikuwa wazi kwamba Wayahudi, wakiwa taifa, hawakuwa yule Israeli aliyeelezwa katika Ufunuo 7:4-8 au katika unabii mwingine wa Biblia unaohusu siku ya Bwana. Wakifuata pokeo, Wayahudi waliendelea kuepuka kutumia jina la kimungu. (Mathayo 15:1-3, 7-9) Kikizungumzia Yeremia 31:31-34, kitabu Jehovah, kilichotangazwa na Mashahidi wa Yehova katika 1934, kilitaarifu hivi kwa mkataa: “Lile agano jipya halihusiani kwa vyovyote na wazao asilia wa Israeli pamoja na aina ya binadamu kwa ujumla, bali . . . lina mpaka kwa Israeli wa kiroho tu.” Unabii wa Biblia juu ya urudisho hauhusu wala Wayahudi asilia wala Israeli ya kisiasa, ambayo ni mshiriki wa Umoja wa Mataifa na ni sehemu ya ulimwengu ambao Yesu alizungumzia kwenye Yohana 14:19, 30 na 18:36.
18 Katika 1931 watumwa wa Mungu duniani walikuwa wamepokea, kwa shangwe kubwa, jina Mashahidi wa Yehova. Wao waliweza kukubaliana kwa moyo wote na maneno ya Zaburi 97:11, NW: “Nuru yenyewe imemeta juu ya mwadilifu, na kushangilia hata kwa ajili ya wale walio wanyoofu katika moyo.” Wao wangeweza kufahamu kwamba Israeli wa kiroho pekee walikuwa wameletwa ndani ya agano jipya. (Waebrania 9:15; 12:22, 24) Waisraeli asilia wasioitikia hawakuwa na sehemu humo, wala aina ya binadamu kwa ujumla. Uelewevu huu ulifungulia njia mmeto mwangavu wa nuru ya kimungu, wenye kutokeza sana katika habari ya tarehe za historia ya kitheokrasi. Huo ungefunua jinsi Yehova atoavyo kwa wingi sana rehema, fadhili za upendo, na ukweli kwa wanadamu wote ambao wanamkaribia yeye. (Kutoka 34:6; Yakobo 4:8) Ndiyo, wengine mbali na Israeli wa Mungu wangenufaishwa na uzuifu wa malaika wa pepo nne za uharibifu. Hao wangekuwa nani? Je! wewe ungeweza kuwa mmoja wao? Acheni tuone sasa.
[Maelezo ya Chini]
a Kwa kufaa, jina Israeli humaanisha “Mungu Hushindana; Mwenye Kushindana (Mwendelevu) Pamoja na Mungu.”—Mwanzo 32:28, New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.
-
-
Kutia Muhuri Israeli wa MunguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha ya ukurasa mzima katika ukurasa wa 114]
[Picha katika ukurasa wa 116, 117]
Uteuzi wa ujumla wa Israeli wa kweli wa Mungu uliendelea kuanzia siku ya Pentekoste 33 W.K. kufika 1935 wakati, kwenye mkusanyiko wenye kufanyiza historia wa Mashahidi wa Yehova katika Washington, D.C., mkazo uligeuzwa ukaelekezwa kwenye kukusanywa kwa umati mkubwa wenye matazamio ya uhai wa kidunia (Ufunuo 7:9)
-
-
Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 20
Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi Sana
1. Baada ya kueleza habari ya kutiwa muhuri kwa wale 144,000, Yohana anaona kikundi gani kingine?
AKIISHA kueleza habari ya kutiwa muhuri kwa 144,000, Yohana anaendelea kuripoti mmojapo mafunuo yenye kutaharakisha zaidi sana katika Andiko lote. Lazima moyo wake uwe uliruka-ruka kwa shangwe alipokuwa akiuripoti, akisema: “Baada ya vitu hivi mimi nikaona, na, tazama! umati mkubwa ambao hakuna binadamu aliyeweza kuhesabu kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na ndimi, wakisimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo, wamevalia majoho meupe; na kulikuwa na matawi ya mitende katika mikono yao.” (Ufunuo 7:9, NW) Ndiyo, kuzuiliwa kwa zile pepo nne kunaruhusu wakati kwa ajili ya wokovu wa kikundi kingine mbali na washiriki 144,000 wa Israeli wa kiroho: umati mkubwa wa lugha nyingi, wa kimataifa.a—Ufunuo 7:1.
2. Waelezaji wa kilimwengu wameelezaje umati mkubwa, na hata Wanafunzi wa Biblia zamani walionaje kikundi hiki?
2 Waelezaji wa kilimwengu wamefasiri huu umati mkubwa kuwa watu wa mnofu wasio Wayahudi ambao wameongolewa kwenye Ukristo au kuwa Wakristo wafia-imani wanaoelekea mbinguni. Zamani, hata Wanafunzi wa Biblia waliwaona kuwa jamii ya pili ya kimbingu, kama ilivyotajwa katika 1886 katika Buku I la Studies in the Scriptures, The Divine Plan of the Ages: “Wao wanapoteza zawadi ya kiti cha ufalme, na ile asili ya kimungu, lakini mwishowe watafikia uzawa wakiwa viumbe wa roho wa hali ya chini zaidi ya asili ya kimungu. Ingawa hawa ni wakfu kikweli, wao wanashindwa na roho ya ulimwengu kwa kadiri ya kwamba wao wanakosa kutoa maisha yao kuwa dhabihu.” Hata karibuni zaidi kama 1930, hilo wazo lilitolewa katika Light, Kitabu cha Kwanza: “Wale wanaojumlika kuwa huu umati mkubwa wanashindwa kuitikia mwaliko wa kuwa mashahidi wenye bidii kwa ajili ya Bwana.” Ilielezwa kuwahusu kuwa kikundi cha wenye uadilifu wa kujifanyia wenyewe waliokuwa na maarifa ya ukweli lakini walifanya kidogo sana kuuhubiri. Walipaswa kwenda mbinguni wakiwa jamii ya pili ambayo haingeshiriki kutawala pamoja na Kristo.
3. (a) Ni tumaini gani walilotolewa wengine wa wale wenye mioyo inayofaa ambao baadaye walikuwa wenye bidii katika kazi ya kuhubiri? (b) Katika 1923 Mnara wa Mlinzi ulielezaje mfano wa kondoo na mbuzi?
3 Hata hivyo, kulikuwako wengine walioshirikiana na Wakristo wapakwa-mafuta ambao baadaye walikuwa wenye bidii zaidi sana katika kazi ya kuhubiri. Wao hawakuwa na tamaa za kwenda mbinguni. Kweli kweli, tumaini lao lilipatana na kichwa cha hotuba iliyotolewa na Mashahidi wa Yehova kuanzia 1918 kufika 1922. Mwanzoni kabisa, hiyo ilikuwa “Ulimwengu Umekoma—Mamilioni Wanaoishi Sasa Hawatakufa Kamwe.”b Upesi baada ya hapo gazeti Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15, 1923, lilieleza mfano wa Yesu wa kondoo na mbuzi (Mathayo 25:31-46), likataarifu: “Kondoo huwakilisha vikundi vyote vya mataifa, si vilivyozaliwa kwa roho lakini vyenye mwelekeo wa uadilifu, ambavyo kiakili hukiri Yesu Kristo kuwa Bwana na ambavyo hutazamia na kutumaini wakati ulio bora chini ya utawala wake.”
4. Nuru kuhusu jamii ya kidunia ilipataje kuwa nyangavu zaidi katika 1931? katika 1932? katika 1934?
4 Miaka kadhaa baadaye, katika 1931, Vindication, Kitabu cha Kwanza, kilizungumzia Ezekieli sura ya 9 kikitambulisha wale watu wenye kutiwa alama juu ya kipaji cha uso kwa ajili ya kuhifadhiwa kwenye mwisho wa ulimwengu kuwa kondoo wa huo mfano wa juu. Vindication, Kitabu cha Tatu, kilichotolewa 1932, kilieleza habari ya unyoofu wa mwelekeo wa moyoni wa mtu asiye Mwisraeli, Yehonadabu, aliyejiunga na Mfalme mpakwa-mafuta, Yehu Mwisraeli katika gari lake akaenda naye akaone bidii ya Yehu katika kufisha wanadini bandia. (2 Wafalme 10:15-17) Kitabu hicho kilitoa elezo hili: “Yehonadabu aliwakilisha au akatangulia kuweka kivuli cha jamii ya watu ambao wako duniani leo katika wakati ambao kazi ya Yehu [ya kujulisha wazi hukumu za Yehova] inaendelea, ambao ni wa nia njema, hawapatani na tengenezo la Shetani, ambao wanachukua msimamo wao katika upande wa uadilifu, na ndio ambao Bwana atahifadhi hai wakati wa Har–Magedoni awachukue kupitia taabu hiyo, na kuwapa uhai wa milele duniani. Hao wanajumlika kuwa ‘jamii ya kondoo.’ Katika 1934 Mnara wa Mlinzi ulieleza wazi kwamba Wakristo hawa walio na matumaini ya kidunia wapaswa wajiweke wakfu kwa Yehova na wabatizwe. Nuru kuhusu hii jamii ya kidunia ilikuwa iking’aa kwa uangavu zaidi na zaidi.—Mithali 4:18.
5. (a) Ni utambulisho gani wa umati mkubwa uliofanywa katika 1935? (b) Wakati J. F. Rutherford katika 1935 alipouliza wanamkusanyiko waliokuwa na tumaini la kuishi milele duniani wasimame, kulitukia nini?
5 Ule uelewevu wa Ufunuo 7:9-17 ulikuwa sasa unakaribia kububujika pamoja na uangavu wao wote wenye kumeremeta! (Zaburi 97:11) Kwa kurudiarudia gazeti Mnara wa Mlinzi lilikuwa limeonyesha tumaini la kwamba mkusanyiko mmoja uliokuwa umeratibiwa Mei 30 kufika Juni 3, 1935, katika Washington D.C., U.S.A., ungekuwa “faraja halisi na manufaa” kwa wale waliotolewa picha na Yehonadabu. Hivyo ndivyo ilivyokuwa! Katika hotuba yenye kusisimua juu ya “Mkutano Mkubwa” iliyotolewa kwa wanamkusanyiko wapatao 20,000, J. F. Rutherford, ambaye wakati huo alikuwa akielekeza kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote, alitoa uthibitisho wa Kimaandiko kwamba kondoo wengine wa ki-siku-hizi ni jamii ile ile ya umati mkubwa wa Ufunuo 7:9. Kwenye upeo wa hotuba hii, msemaji huyo aliuliza: “Wale wote ambao wana tumaini la kuishi milele juu ya dunia tafadhali mnaweza kusimama?” Sehemu kubwa ya hadhirina ilipokuwa ikisimama, msemaji alitangaza: “Tazameni! Mkutano mkubwa!” Kukawa na kimya, kikifuatwa na vigelegele vyenye mngurumo. Ilifurahi kama nini jamii ya Yohana—na pia kikundi cha Yehonadabu! Keshoye, Mashahidi wapya 840 walibatizwa, walio wengi zaidi wa hawa wakidai kuwa wa huo umati mkubwa.
Kuthibitisha Utambulisho wa Umati Mkubwa
6. (a) Ni kwa nini sisi tunaweza kuelewa waziwazi kwamba umati mkubwa ni kikundi cha ki-siku-hizi cha Wakristo walio wakfu ambao wanatumaini kuishi milele duniani? (b) Yale majoho meupe ya huo umati mkubwa yanafananisha nini?
6 Sisi tunaweza kutaarifuje tukiwa na uhakika sana hivyo kwamba ule umati mkubwa ni kikundi hiki cha ki-siku-hizi cha Wakristo waliojiweka wakfu ambao wanatumaini kuishi milele juu ya dunia ya Mungu? Wakati uliotangulia, Yohana alikuwa ameona katika njozi kikundi cha kimbingu ‘ambacho kilinunuliwa kwa ajili ya Mungu kutoka kila kabila na ulimi na vikundi vya watu na taifa.’ (Ufunuo 5:9, 10, NW) Umati mkubwa una chanzo kinachofanana na hicho lakini wanakoenda ni tofauti. Tofauti na Israeli wa Mungu, hesabu yao haikukusudiwa kimbele. Hakuna mtu anayeweza kusema mapema watakuwa wangapi. Majoho yao meupe yameoshwa kwa damu ya yule Mwana-Kondoo, kufananisha kwamba wao wana msimamo wenye uadilifu mbele za Yehova kwa sababu ya imani yao katika dhabihu ya Yesu. (Ufunuo 7:14) Nao wanapungapunga matawi ya mitende, wakimshangilia Mesiya kuwa Mfalme wao.
7, 8. (a) Kule kupungwapungwa kwa matawi ya mitende bila shaka kulimkumbusha mtume Yohana juu ya matukio gani? (b) Ni nini maana ya uhakika wa kwamba hao wa umati mkubwa wanapungapunga matawi ya mitende?
7 Anapotazama katika njozi hii, mawazo ya Yohana lazima yawe yanamrudisha nyuma zaidi ya miaka 60 kwenye juma la mwisho la Yesu duniani katika Nisani 9, 33 W.K., wakati umati ulipokuja makundi makundi ili kumkaribisha Yesu ndani ya Yerusalemu, wao “walichukua matawi ya mitende wakatoka nje kumlaki. Na wao wakaanza kupaaza sauti: ‘Okoa, sisi twaomba wewe! Mbarikiwa ni yeye ambaye anakuja katika jina la Yehova, hata mfalme wa Israeli!’” (Yohana 12:12, 13, NW) Hali moja na hiyo, kule kupungapunga matawi ya mitende na kupaaza sauti upande wa umati mkubwa huonyesha shangwe yao isiyozuilika katika kumkubali Yesu kuwa Mfalme wa Yehova aliyewekwa rasmi.
8 Pasipo shaka, hayo matawi ya mitende na vilio vya kuchachawa pia vinamkumbusha Yohana ile Sikukuu ya Vibanda ya kale ya Israeli. Kwa ajili ya sikukuu hii Yehova aliamuru: “Na ni lazima nyinyi mjichukulie kwa ajili yenu wenyewe katika siku ya kwanza tunda la miti mizuri sana, na matagaa ya mitende na matanzu ya miti yenye matawi na mipopla ya bonde la mvo, na ni lazima nyinyi mshangilie mbele za Yehova Mungu wenu siku saba.” Matawi ya mitende yalitumiwa kuwa alama ya kushangilia. Vibanda vya muda vilikuwa kikumbusha kwamba Yehova alikuwa amewaokoa watu wake kutoka Misri, waishi katika mahema katika jangwa. “Mkazi mgeni na mvulana asiye na baba na mjane” walishiriki hii sikukuu. Waisraeli wote walipaswa ‘wawe si kitu ila wenye kujawa na shangwe.’—Walawi 23:40; Kumbukumbu 16:13-15, NW.
9. Umati mkubwa unajiunga katika kilio gani cha shangwe?
9 Basi, inafaa kwamba, umati mkubwa, ingawa si sehemu ya Israeli wa kiroho, upungepunge matawi ya mitende kwa kuwa wanaonyesha kwa shangwe na asante kwamba ushindi na wokovu hutoka kwa Mungu na Mwana-Kondoo kama Yohana anavyoona hapa: “Nao hufuliza kulia kwa sauti kubwa, kusema: ‘Wokovu wetu ni kwa Mungu wetu, ambaye ameketi juu ya kiti cha ufalme, na kwa Mwana-Kondoo.’” (Ufunuo 7:10, NW) Ijapokuwa wao wametengwa kutoka vikundi vyote vya kikabila, huo umati mkubwa unalia kwa hiyo “sauti kubwa” moja tu. Wao wanawezaje kufanya hivi, wajapokuwa ni wa mataifa na lugha mbalimbali?
10. Umati mkubwa unaweza kuliaje kwa umoja kwa “sauti kubwa” moja ijapokuwa ni wa mataifa na lugha mbalimbali?
10 Huu umati mkubwa ni sehemu ya tengenezo la mataifa mengi ambalo ndilo pekee lina umoja kweli kweli duniani leo. Wao hawana viwango tofauti-tofauti kwa nchi tofauti-tofauti bali wanatumia kwa ajili ya upatani kanuni za Biblia zinazofaa kokote wanakoishi. Wao hawajiingizi katika harakati za kitaifa, zenye kutaka mapinduzi bali wao ‘wamefua panga zao zikawa majembe ya plau.’ (Isaya 2:4, NW) Wao hawana mgawanyiko wa mafarakano au vikundi vya kidini, hivi kwamba wanapaaza sauti zilizovurugika au jumbe za pamoja zenye kupingana-pingana kama zinavyofanya dini za Jumuiya ya Wakristo; wala wao hawaachii jamii ya viongozi wa kidini wenye kulipwa mshahara wafanye kusifu kwa ajili yao. Wao hawapaazi sauti kwamba wokovu wao hutoka kwa roho takatifu kwa kuwa wao si watumishi wa kamungu ka utatu. Katika maeneo ya kijiografia 200 kuzunguka dunia, wao wana umoja katika kuita juu ya jina la Yehova wanaposema lugha safi ya ukweli. (Sefania 3:9) Kwa kufaa, wao wanakiri peupe kwamba wokovu wao unakuja kutoka kwa Yehova Mungu wa wokovu, kupitia Yesu Kristo, Wakili Mkuu Wake wa wokovu.—Zaburi 3:8; Waebrania 2:10.
11. Tekinolojia ya ki-siku-hizi imesaidiaje wale wa umati mkubwa kufanya sauti yao kubwa iwe kubwa hata zaidi?
11 Tekinolojia ya ki-siku-hizi imesaidia kufanya sauti kubwa ya umati mkubwa wenye umoja ivume kwa ukubwa hata zaidi. Hakuna kikundi kinginecho cha kidini duniani ambacho kina uhitaji wa kuchapisha misaada ya kujifunza Biblia katika lugha zaidi ya 400, kwa maana hakuna kikundi kinginecho ambacho kinapendezwa na kufikia vikundi vyote vya watu wa dunia kwa ujumbe mmoja wenye umoja. Kama msaada zaidi katika jambo hili, chini ya uangalizi wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova lililopakwa mafuta mfumo uitwao, Multilanguage Electronic Phototypesetting System (MEPS) uliundwa. Kufikia wakati kitabu hiki kilipochapishwa, namna tofauti-tofauti za MEPS zinatumiwa katika maeneo zaidi ya 125 kuzunguka dunia, na jambo hili limesaidia kufanya iwezekane utangazaji sawia wa jarida la mara mbili kwa mwezi, Mnara wa Mlinzi, katika lugha zaidi ya 130. Pia watu wa Yehova wanatangaza kisawia, vitabu kama hiki, kwa lugha kadhaa. Hivyo, Mashahidi wa Yehova, ambao ule umati mkubwa ndio walio wengi sana, wanaweza kila mwaka kugawa mamia ya mamilioni ya vichapo katika lugha zote zinazojulikana vizuri zaidi, wakiwezesha misongamano mingi zaidi ya kutoka makabila yote na lugha wajifunze Neno la Mungu na kuunga sauti zao kwenye ile sauti kubwa ya umati mkubwa.—Isaya 42:10, 12.
Mbinguni au Duniani?
12, 13. Ni katika njia gani umati mkubwa ‘umesimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo’?
12 Sisi tunajuaje kwamba ‘kusimama mbele ya kiti cha ufalme’ hakumaanishi kwamba umati mkubwa umo mbinguni? Kuna ithibati nyingi iliyo wazi juu ya jambo hili. Mathalani, neno la Kigiriki linalotafsiriwa hapa “mbele” (e·noʹpi·on) humaanisha kihalisi “katika [mwono wa]” nalo linatumiwa mara kadhaa kuhusu wanadamu duniani ambao wako “mbele” au “katika mwono wa” Yehova. (1 Timotheo 5:21; 2 Timotheo 2:14; Warumi 14:22; Wagalatia 1:20, NW) Katika pindi moja wakati Waisraeli walipokuwa katika jangwa, Musa alimwambia Haruni hivi: “Sema kwa kusanyiko zima la wana wa Israeli, ‘Njooni karibu mbele za Yehova, kwa sababu yeye amesikia manung’uniko yenu.’” (Kutoka 16:9, NW) Waisraeli hao hawakulazimika kusafirishwa mpaka mbinguni ili wakasimame mbele za Yehova katika pindi hiyo. (Linga Walawi 24:8.) Badala ya hivyo, uko huko jangwani walisimama katika mtazamo wa Yehova, na uangalifu wake ukawa juu yao.
13 Kwa kuongezea, sisi tunasoma hivi: “Wakati Mwana wa binadamu anapowasili katika utukufu wake . . . mataifa yote yatakusanywa mbele ya yeye.”c Jamii ya kibinadamu kwa ujumla haitakuwamo katika mbingu wakati unabii huu unapotimizwa. Bila shaka, wale ambao ‘huondoka kwenda kuingia katika kukatiliwa mbali milele’ hawatakuwamo katika mbingu. (Mathayo 25:31-33, 41, 46, NW) Badala ya hivyo, aina ya binadamu husimama duniani katika mtazamo wa Yesu, naye hugeuza uangalifu wake awahukumu. Hali kadhalika, umati mkubwa uko “mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo” katika maana ya kwamba huo husimama katika mtazamo wa Yehova na Mfalme wake, Kristo Yesu, ambao kutoka kwao unapokea hukumu yenye kupendeleka.
14. (a) Ni nani wanaosimuliwa kuwa wako “kuzunguka kiti cha ufalme” na “juu ya Mlima Sayuni” wa kimbingu? (b) Ingawa umati mkubwa unatumikia Mungu “katika hekalu lake,” ni kwa sababu gani hilo haliwafanyi kuwa jamii ya kikuhani?
14 Wazee 24 na kikundi cha wapakwa-mafuta 144,000 wanasimuliwa kuwa wako ‘kuzunguka kiti cha ufalme cha Yehova pande zote’ na “juu ya Mlima Sayuni” wa kimbingu. (Ufunuo 4:4; 14:1, NW) Umati mkubwa si jamii ya kikuhani nao haufikii cheo hicho kilichokwezwa. Kweli, baadaye unasimuliwa katika Ufunuo 7:15 kuwa unatumikia Mungu “katika hekalu lake.” Lakini hekalu hili halirejezei patakatifu pa ndani zaidi, pale Patakatifu Zaidi Sana. Badala ya hivyo, ni ua wa kidunia wa hekalu la Mungu la kiroho. Neno la Kigiriki na·osʹ, linalotafsiriwa hapa “hekalu,” mara nyingi huwasilisha maana pana ya jengo zima lote lililojengwa kwa ajili ya ibada ya Yehova. Leo, hili ni jengo la kiroho ambalo hutia ndani mbingu na dunia pia.—Linga Mathayo 26:61; 27:5, 39, 40; Marko 15:29, 30; Yohana 2:19-21, New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.
Vigelegele vya Sifa vya Ulimwengu Wote Mzima
15, 16. (a) Kunakuwa na tendo-itikio gani katika mbingu kwa kuonekana kwa umati mkubwa? (b) Uumbaji wa roho wa Yehova unatendaje kwa kuitikia kila ufunuo mpya wa kusudi lake? (c) Sisi tuliopo duniani tunaweza kujiungaje kuimba wimbo wa sifa?
15 Umati mkubwa unamsifu Yehova, lakini wengine pia wanaimba sifa zake. Yohana anaripoti: “Na malaika wote walikuwa wakisimama kuzunguka kiti cha ufalme na wazee na viumbe hai wanne, na wao walianguka nyuso zao chini mbele ya kiti cha ufalme na wakaabudu Mungu, kusema: ‘Ameni! Baraka na utukufu na hekima na utoaji-shukrani na heshima na nguvu na imara ziwe kwa Mungu wetu milele na milele. Ameni.’”—Ufunuo 7:11, 12, NW.
16 Wakati Yehova alipoumba dunia, malaika zake wote watakatifu ‘walipiga kilio kikuu kwa shangwe pamoja, na wana wote wa Mungu wakaanza kupaaza sauti kwa vifijo.’ (Ayubu 38:7, NW) Kila ufunuo mpya wa kusudi la Yehova lazima uwe ulitokeza mipaazo ya sifa ya kimalaika jinsi iyo hiyo. Wakati wazee 24—144,000 katika utukufu wao wa kimbingu—wanapolia kwa sauti kubwa katika kumtambua Mwana-Kondoo, wengine wote wa viumbe wa kimbingu huitikia kwa kusifu Yesu na Yehova Mungu. (Ufunuo 5:9-14) Tayari, viumbe hawa wamekuwa na shangwe mno kuona utimizo wa kusudi la Yehova katika kufufua kwake wanadamu wapakwa-mafuta waaminifu kwenye mahali penye utukufu katika milki ya kiroho. Sasa, viumbe wote waaminifu wa Yehova wa kimbingu wanabubujika kwa sifa za kimelodia wakati umati mkubwa unapoonekana. Kwa kweli, kwa watumishi wote wa Yehova, siku ya Bwana ni wakati wenye kusisimua kuishi humo. (Ufunuo 1:10) Hapa duniani, sisi ni wenye pendeleo kama nini kushiriki kuimba wimbo wa sifa kwa kuutolea Ufalme wa Yehova ushuhuda!
Umati Mkubwa Wajionyesha
17. (a) Ni swali gani linalozushwa na mmoja wa wazee 24, na uhakika wa kwamba mzee angeweza kupata mahali pa jibu unadokeza nini? (b) Swali la mzee lilijibiwa lini?
17 Tangu wakati wa mtume Yohana na kundelea mpaka ndani ya siku ya Bwana, Wakristo wapakwa-mafuta walitatizika wakitaka kujua utambulisho wa umati mkubwa. Basi, inafaa kwamba, mmoja wa wazee 24, akiwakilisha wapakwa-mafuta ambao tayari wako katika mbingu, achochee kufikiri kwa Yohana kwa kuzusha swali hususa: “Na katika kuitikia mmoja wa wazee akasema kwangu mimi: ‘Hawa ambao wamevalia majoho meupe, wao ni akina nani na wao walitoka wapi?’ Kwa hiyo mara hiyo mimi nikasema kwa yeye: ‘Bwana yangu, wewe ndiwe mmoja ambaye anajua.’” (Ufunuo 7:13, 14a, NW) Ndiyo, huyo mzee angeweza kupata mahali pa jibu na kumpa Yohana. Hiyo inadokeza kwamba waliofufuliwa wa kikundi cha wazee 24 huenda wakawa wanahusika katika kuwasilisha kweli za kimungu leo. Kwa upande wao, wale wa jamii ya Yohana waliomo duniani walipata kujua utambulisho wa umati mkubwa kwa kutazama kwa ukaribu sana alichokuwa akifanya Yehova katikati yao. Wao walikuwa wenye uharaka wa kuthamini mmeto wenye kutia kiwi wa nuru ya kimungu ambao ulipamba anga la kitheokrasi katika 1935, wakati barabara wa Yehova.
18, 19. (a) Ni tumaini gani lililokaziwa na jamii ya Yohana wakati wa miaka ya 1920 na 1930, lakini ni nani walioitikia ujumbe kwa hesabu yenye kuongezeka? (b) Ule utambulisho wa umati mkubwa katika 1935 ulionyesha nini kwa habari ya 144,000? (c) Takwimu za Ukumbusho zinafunua nini?
18 Wakati wa miaka ya 1920 na 1930, jamii ya Yohana ilikuwa imekazia tumaini la kimbingu, katika vichapo na katika kazi ya kuhubiri pia. Kwa wazi hesabu kamili ya 144,000 ilikuwa bado kutimia. Lakini hesabu iliyokuwa ikiongezeka ya wale waliotii ujumbe na wakaonyesha bidii katika kazi ya kutoa ushuhuda wakaja kudhihirisha kuwa wanapendezwa na kuishi milele katika dunia Paradiso. Wao hawakuwa na tamaa ya kwenda mbinguni. Huo haukuwa mwito wao. Wao hawakuwa sehemu ya kundi dogo bali ya kondoo wengine. (Luka 12:32; Yohana 10:16) Kutambulishwa kwao katika 1935 kuwa umati mkubwa wa wale kondoo wengine kilikuwa kionyeshi cha kwamba wakati huo kuchaguliwa kwa 144,000 kulikuwa karibu kumekamilika.
19 Je! takwimu zinaunga mkono mkataa huu? Ndiyo. Katika 1938, ulimwenguni pote, Mashahidi wa Yehova 59,047 walishiriki katika huduma. Kati ya hao 36,732 walishiriki mifano kwenye mwadhimisho wa kila mwaka wa Ukumbusho wa kifo cha Yesu, hivyo wakionyesha kwamba walikuwa na mwito wa kimbingu. Katika miaka iliyofuata tangu hapo, hesabu ya washiriki hao imeendelea kupungua, hasa kwa sababu Mashahidi waaminifu wa Yehova walimaliza mwendo wa maisha yao ya kidunia katika kifo. Katika 2005 ni 8,524 pekee walioshiriki mifano ya Ukumbusho—asilimia 0.05 tu ya wale 16,390,116 waliohudhuria mwadhimisho huo wa pote katika tufe.
20. (a) Wakati wa Vita ya Ulimwengu 2, ni elezo gani alilotoa faraghani J. F. Rutherford kwa habari ya umati mkubwa? (b) Ni uhakika gani sasa unaoonyesha kwamba umati mkubwa ni mkubwa kweli kweli?
20 Wakati vita ya pili ya ulimwengu ilipofyatuka, Shetani alitia jitihada kali azuie kuvunwa kwa umati mkubwa. Kazi ya Yehova ilizuiwa katika nchi nyingi. Siku hizo zilizokuwa ngumu, na muda mfupi kabla ya kifo chake katika Januari 1942, J. F. Rutherford alisikiwa akisema: “Basi . . . inaonekana kama umati mkubwa hautakuwa mkubwa sana hata hivyo.” Lakini baraka za kimungu zilielekeza vingine! Kufikia 1946 hesabu ya Mashahidi waliokuwa wakitumikia ulimwenguni pote ilikuwa imeruka kufikia 176,456—walio wengi wa hao wakiwa wa umati mkubwa. Katika 2005 walikuwako Mashahidi 6,390,022 waliokuwa wakitumikia Yehova kiaminifu katika mabara mbalimbali 235—UMATI MKUBWA kweli kweli! Na hesabu inazidi kuongezeka.
21. (a) Kuvunwa kwa watu wa Mungu wakati wa siku ya Bwana kumekuwaje katika upatani kamili na njozi ya Yohana? (b) Unabii fulani wa maana ulianza kutimizwaje?
21 Hivyo kuvunwa kwa watu wa Mungu wakati wa siku ya Bwana kumekuwa katika upatani kamili na njozi ya Yohana: kwanza kazi ya kukusanya mabaki ya 144,000; kisha kukusanywa kwa umati mkubwa. Kama Isaya alivyotoa unabii, sasa “katika sehemu ya mwisho kabisa ya siku,” watu wa mataifa yote wanamiminika kushiriki ibada safi ya Yehova. Na, kweli kweli, sisi tunachachawa katika uthamini wa uumbaji wa Yehova wa “mbingu mpya na dunia mpya.” (Isaya 2:2-4; 65:17, 18, NW) Mungu anakusanya “tena vitu vyote pamoja katika Kristo, vitu katika mbingu na vitu juu ya dunia.” (Waefeso 1:10, NW) Warithi wapakwa-mafuta wa Ufalme wa kimbingu—waliochaguliwa katika muda wa karne zilizopita tangu siku ya Yesu—ndio “vitu katika mbingu.” Na sasa, umati mkubwa wa kondoo wengine wanatokea wakiwa wa kwanza wa “vitu juu ya dunia.” Kutumikia kwako kupatana na mpango huo kunaweza kumaanisha furaha ya milele kwa ajili ya wewe.
Baraka za Umati Mkubwa
22. Ni habari gani zaidi anayopokea Yohana kuhusu umati mkubwa?
22 Kupitia mfereji wa kimungu Yohana anapokea habari zaidi kuhusu huu umati mkubwa: “Na yeye [mzee] akasema kwangu mimi: ‘Hawa ndio wale ambao huja kutoka dhiki kubwa, na wamefua majoho yao na wameyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo. Hiyo ndiyo sababu wao wako mbele ya kiti cha ufalme cha Mungu; na wao wanatolea yeye utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake; na Mmoja anayeketi juu ya kiti cha ufalme atatanda hema yake juu yao.’”—Ufunuo 7:14b, 15, NW.
23. Ni nini iliyo dhiki kubwa ambayo umati mkubwa “huja kutoka” hiyo?
23 Katika pindi ya mapema zaidi, Yesu alikuwa amesema kwamba kuwapo kwake katika utukufu wa Ufalme kungefikia upeo katika “dhiki kubwa kama ambayo haijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka sasa, la, wala haitatukia tena.” (Mathayo 24:21, 22, NW) Katika utimizo wa unabii huo, wale malaika wataachilia pepo nne za dunia zikumbe mfumo wa ulimwengu wa Shetani. Cha kwanza kwenda kitakuwa ni Babuloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini bandia. Kisha, kwenye upeo wa dhiki hiyo, Yesu ataokoa mabaki duniani ya 144,000, pamoja na umati mkubwa wenye watu wengi sana.—Ufunuo 7:1; 18:2.
24. Watu mmoja mmoja wa umati mkubwa wanastahilije kwa ajili ya kuokoka?
24 Watu mmoja mmoja wa umati mkubwa wanastahilije kwa ajili ya kuokoka? Yule mzee anamwambia Yohana kwamba “wamefua majoho yao na wameyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” Kwa maneno mengine, wao wamezoea imani katika Yesu akiwa Mkombozi wao, wamejiweka wakfu kwa Yehova, nao wameonyesha wakfu wao kwa ubatizo wa maji, na ‘wanashika dhamiri njema’ kwa mwenendo wao mnyoofu. (1 Petro 3:16, 21; Mathayo 20:28, NW) Hivyo, wao ni safi na waadilifu katika macho ya Yehova. Na wanajiweka wenyewe “bila doa kutoka ulimwengu.”—Yakobo 1:27, NW.
25. (a) Umati mkubwa unamtoleaje Yehova “utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake”? (b) Yehova ‘anatandaje hema lake’ juu ya umati mkubwa?
25 Na zaidi, wao wamekuwa Mashahidi wenye bidii wa Yehova—“wanatolea yeye utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake.” Je! wewe ni mmoja wa huu umati mkubwa ulio wakfu? Ikiwa ndivyo, ni pendeleo lako kutumikia Yehova bila kuacha katika ua wake wa kidunia wa hekalu lake kubwa la kiroho. Leo, chini ya mwelekezo wa wapakwa-mafuta, umati mkubwa unafanya sehemu iliyo kubwa zaidi ya kazi ya kutoa ushuhuda. Wajapokuwa na madaraka ya kimwili, mamia ya maelfu wanautafutia nafasi ule utumishi wa wakati wote wakiwa mapainia. Lakini uwe wewe ni wa kikundi hicho au la, ukiwa mshiriki aliye wakfu wa umati mkubwa, wewe unaweza kushangilia ukiwa rafiki ya Mungu na mgeni anayekaribishwa katika hema yake. (Zaburi 15:1-5; Yakobo 2:21-26) Hivyo Yehova ‘anatanda hema yake’ juu ya wale ambao wanampenda yeye na, akiwa mkaribishaji-wageni mwema, anawapa himaya.—Mithali 18:10.
26. Ni baraka gani nyingine utakazofurahia umati mkubwa?
26 Yule mzee anaendelea: “Wao hawataona njaa tena wala kuona kiu tena, wala jua halitapiga juu yao tena wala joto lolote lenye kuunguza, kwa sababu Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha ufalme, atachunga wao, na ataelekeza wao kwenye vibubujiko vya maji ya uhai. Na Mungu atapangusa kabisa kila chozi kutoka macho yao.” (Ufunuo 7:16, 17, NW) Ndiyo, Yehova ni mkaribishaji-wageni kikweli! Lakini kuna maana gani yenye kina kirefu katika maneno haya?
27. (a) Isaya alitoaje unabii wa jambo linalofanana na maneno ya mzee? (b) Ni nini kinachoonyesha kwamba unabii wa Isaya ulianza kutimizwa juu ya kundi la Kikristo katika siku ya Paulo?
27 Acheni sisi tufikirie unabii ulio na maneno yanayofanana na hayo: “Hivi ndivyo Yehova amesema: ‘Katika wakati wa nia njema mimi nilijibu wewe, na katika siku ya wokovu mimi nimekusaidia wewe . . . Wao hawataenda njaa, wala hawataenda kiu, wala joto lenye kukausha au jua halitapiga wao. Kwa kuwa Mmoja ambaye ana sikitikio juu yao ataendesha wao, na kando ya chemchemi za maji yeye ataongoza wao.’” (Isaya 49:8, 10, NW; ona pia Zaburi 121:5, 6.) Mtume Paulo alinukuu sehemu ya unabii huu na akautumia kuhusu “siku ya wokovu” iliyoanza Pentekoste 33 W.K. Yeye aliandika: “Kwa maana yeye [Yehova] asema: ‘Katika wakati uliokubalika mimi nilisikia wewe, na katika siku ya wokovu mimi nilisaidia wewe.’ Tazama! Sasa ndio hasa wakati uliokubalika. Tazama! Sasa ndiyo siku ya wokovu.”—2 Wakorintho 6:2, NW.
28, 29. (a) Maneno ya Isaya yalitimizwaje katika karne ya kwanza? (b) Maneno ya Ufunuo 7:16 yanatimizwaje kwa habari ya umati mkubwa? (c) Ni nini litakalokuwa tokeo la kuelekezwa kwa umati mkubwa kwenye “vibubujiko vya maji ya uhai”? (d) Ni kwa nini umati mkubwa utakuwa usio na kifani miongoni mwa aina ya binadamu?
28 Ile ahadi ya kutoona njaa au kiu au kutaabishwa na joto lenye kukausha ilitumikaje wakati huo huko nyuma? Hakika, Wakristo katika karne ya kwanza walitaabishwa na njaa na kiu halisi nyakati nyingine. (2 Wakorintho 11:23-27) Ingawa hivyo, katika maana ya kiroho, wao walikuwa na chakula tele. Wao waliandaliwa kwa wingi hivi kwamba wao hawakwenda njaa au kiu kwa vitu vya kiroho. Zaidi ya hilo, Yehova hakuruhusu joto la kasirani yake liwake dhidi yao wakati yeye alipoharibu mfumo wa mambo wa Kiyahudi katika 70 W.K. Maneno ya Ufunuo 7:16 yana utimizo wa kiroho unaofanana na huo kwa ajili ya umati mkubwa leo. Pamoja na Wakristo wapakwa-mafuta, wao wanafurahia wingi wa maandalizi ya kiroho.—Isaya 65:13; Nahumu 1:6, 7.
29 Ikiwa wewe ni mmoja wa ule umati mkubwa, hali yako njema ya moyo itakufanya wewe “upige kilio kikuu kwa shangwe,” si kitu ulazimike kuvumilia nini kwa habari ya manyimo na mikazo wakati wa miaka hii ya gizagiza ya mfumo wa Shetani. (Isaya 65:14, NW) Katika maana hiyo, hata sasa, Yehova anaweza ‘kupangusa kabisa kila chozi kutoka macho yako.’ “Jua” lenye joto jingi la Mungu au hukumu mbaya halikutishi wewe tena, na pepo nne za uharibifu ziachiliwapo, huenda wewe ukakingwa na “joto lenye kuunguza” la kutopendezwa kwa Yehova. Baada ya uharibifu huo kwisha, yule Mwana-Kondoo atakuelekeza wewe unufaishwe kikamili na “vibubujiko vya maji ya uhai” vyenye kutia uhai mpya, hivyo vikiwa vinawakilisha maandalizi yote ambayo Yehova anakufanyia wewe upate uhai wa milele. Imani yako katika damu ya Mwana-Kondoo itatetewa katika maana ya kwamba wewe utainuliwa polepole ufikie ukamilifu wa kibinadamu. Nyinyi wa umati mkubwa mtakuwa bila kifani miongoni mwa aina ya binadamu mkiwa yale “mamilioni” ambayo hayakulazimika hata kufa! Katika maana iliyo kamili zaidi, kila chozi litakuwa limekwisha panguswa kabisa kutoka macho yenu.—Ufunuo 21:4.
Kufanya Ule Mwito Uwe Hakika
30. Ni mandhari gani nzuri mno inayofunguka kwetu katika njozi ya Yohana, na ni nani ambaye ataweza “kusimama”?
30 Lo! maneno haya yanatufungulia mandhari nzuri mno kama nini! Yehova mwenyewe yu katika kiti cha ufalme chake, na watumishi wake wote, wa kimbingu na wa kidunia, wanaungana katika kumsifu yeye. Watumishi wake wa kidunia wanathamini ni pendeleo lenye kutia hofu kama nini walilo nalo kushiriki katika hii korasi ya sifa inayoongezeka. Karibuni sana, Yehova na Kristo Yesu watatekeleza hukumu, nacho kilio hiki kitasikika: “Siku kubwa ya hasira-kisasi yao imekuja, na ni nani anaweza kusimama?” (Ufunuo 6:17, NW) Na jibu? Ni sehemu ndogo tu ya aina ya binadamu, kutia na wowote kati ya 144,000 waliotiwa muhuri ambao huenda wangali wanabaki katika mnofu na umati mkubwa wa kondoo wengine ndio ‘watasimama,’ yaani, wataokoka pamoja nao.—Yeremia 35:19; 1 Wakorintho 16:13.
31. Utimizo wa njozi ya Yohana wapasa uathirije Wakristo, wa wapakwa-mafuta na wa ule umati mkubwa pia?
31 Kwa sababu ya uhakika huu, Wakristo wapakwa-mafuta wa jamii ya Yohana hujipinda wenyewe kisulubu katika ‘kufuatilia kuteremka kuelekea mradi kwa ajili ya tuzo la mwito wa kuelekea juu wa Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.’ (Wafilipi 3:14, NW) Wao wanafahamu kabisa kwamba matukio wakati wa siku hizi hutaka uvumilivu wa pekee upande wao. (Ufunuo 13:10) Baada ya kutumikia Yehova kishikamanifu kwa miaka mingi, wao wanashikilia sana imani, wakishangilia kwamba majina yao “yamechorwa katika mbingu.” (Luka 10:20; Ufunuo 3:5, NW) Wale wa umati mkubwa vilevile wanajua kwamba ni “yeye ambaye amevumilia hadi mwisho ndiye ambaye ataokolewa.” (Mathayo 24:13, NW) Ingawa umati mkubwa ukiwa kikundi umetiwa alama utoke katika dhiki kubwa, watu mmoja mmoja wa huo lazima wajipinde wenyewe wabaki wakiwa safi na wenye kutenda.
32. Ni hali gani yenye umuhimu inayokaziwa na uhakika wa kwamba ni vikundi viwili tu ndivyo vitaweza “kusimama” katika siku ya hasira-kisasi ya Yehova?
32 Hakuna ithibati kwamba yeyote kando na hivi vikundi viwili ‘atasimama’ katika siku ya hasira-kisasi ya Yehova. Hii humaanisha nini kwa yale mamilioni ambayo kila mwaka huonyesha staha fulani kwa dhabihu ya Yesu kwa kuhudhuria mwadhimisho wa Ukumbusho wa kifo chake lakini ambao bado hawajajizoeza imani katika dhabihu ya Yesu kufikia hatua ya kuwa watumishi wa Yehova walio wakfu na waliobatizwa, wenye kutenda katika utumishi wake? Na zaidi, namna gani wale ambao hapo zamani walikuwa watendaji lakini ambao wameruhusu mioyo yao ‘ilemewe na mahangaikio ya maisha?’ Wote hao na waamke, na wakae wakiwa macho, ili ‘wafaulu katika kuponyoka mambo hayo yote ambayo yamekusudiwa yatukie na katika kusimama mbele ya Mwana wa binadamu’—Yesu Kristo. Wakati ni mfupi!—Luka 21:34-36, NW.
[Maelezo ya Chini]
a Ona New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.
b The Watch Tower, Aprili 1, 1918, ukurasa 98.
c Kihalisi, “katika mbele ya yeye,” The Kingdom Interlinear Translation of the Greek Scriptures.
-
-
Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha ya ukurasa mzima katika ukurasa wa 121]
-