-
Vitu Ambavyo Lazima Vitukie KaribuniUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
4. (a) Kwa kuwa Yohana aliandika Ufunuo zaidi ya miaka 1,900 iliyopita, yeye angewezaje kusema juu ya “vitu ambavyo lazima vitukie karibuni”? (b) Ithibati inaonyesha nini sasa juu ya vitu vilivyotabiriwa?
4 Ingawa hivyo, Yohana angewezaje kusema, hawa “watumwa” wangeonyeshwa “vitu ambavyo lazima vitukie karibuni”? Je! maneno hayo hayakusemwa zaidi ya miaka 1,900 iliyopita? Kwa maoni ya Yehova, ambaye machoni pake miaka elfu moja ni “kama siku ya jana,” miaka 1,900 ni wakati mfupi unapolinganishwa na vipindi virefu vya wakati aliotumia katika kuumba na kutayarisha dunia ikaliwe na wanadamu. (Zaburi 90:4) Mtume Paulo aliandika juu ya “taraja na tumaini lenye hamu nyingi” lake mwenyewe, kwa kuwa pasipo shaka uhakika wa thawabu yake ulionekana kwake kuwa karibu sana. (Wafilipi 1:20, NW) Hata hivyo, leo, ithibati ni tele kwamba vile vitu vyote vilivyotabiriwa vitatukia kwa wakati ulioorodheshwa. Wokovu wenyewe wa aina ya binadamu haujapata kamwe kuhatarishwa kabla ya sasa katika historia. Ni Mungu tu aliye na ufumbuzi!—Isaya 45:21.
-
-
Vitu Ambavyo Lazima Vitukie KaribuniUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
11. (a) Ni kwa sababu gani ni jambo la muhimu sisi tuyashike maneno ya unabii huo? (b) Ni wakati gani ambao lazima uwe karibu sana sasa kihatari?
11 Ni jambo la muhimu sisi tuyashike maneno ya unabii huo, “kwa kuwa wakati uliowekwa u karibu.” Wakati uliwekewa nini? Utimizo wa unabii wa Ufunuo, kutia hukumu za Mungu. Wakati uko karibu kwa Mungu na Yesu Kristo kutekeleza hukumu ya kukata maneno juu ya mfumo wa ulimwengu wa Shetani. Wakati Yesu alipokuwa hapa duniani, yeye alitaarifu kwamba baba yake pekee ndiye alijua “siku hiyo au saa.” Akitazama mbele kwenye taabu ambazo zimeongezeka duniani katika nyakati zetu, Yesu alisema pia hivi: “Kizazi hiki hakitapitilia mbali kwa vyovyote mpaka mambo haya yote yatukie.” Kwa hiyo wakati uliowekwa wa kutekeleza uamuzi wa Mungu ni lazima uwe karibu sana kihatari. (Marko 13:8, 30-32, NW) Kama Habakuki 2:3 hutaarifu: “Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia.” Wokovu wetu kuipita ile dhiki kubwa unategemea kushika kwetu Neno la kiunabii la Mungu.—Mathayo 24:20-22.
-
-
Vitu Ambavyo Lazima Vitukie KaribuniUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Ufunuo kwa Yesu Kristo, ambao Mungu alimpa, aonyeshe watumwa wake vitu ambavyo lazima vitukie karibuni.” (Ufunuo 1:1a, NW)
-
-
Yesu Aja na Kitia-MoyoUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
1. Sasa Yohana anaandikia nani, na ni nani leo wanaopaswa kuona ujumbe wake ukiwa wenye upendezi wenye kuvuta fikira?
YALE yanayofuata yapasa yawe yenye upendezi wenye kuvuta fikira kwa kila mmoja anayeshirikiana na makundi ya watu wa Mungu leo. Hapa pana mfululizo wa jumbe. Hizo zina tumizi maalumu kadiri “ule wakati uliowekwa” uzidivyo kukaribia. (Ufunuo 1:3, NW)
-