Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uzuri Mwingi Mno wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha Kimbingu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 17. Ile “bahari ya kioo kama fuwele” inafananisha nini?

      17 Pia Yohana anaona “bahari ya kioo kama fuwele.” Hii ingefananisha nini kwa wale walioalikwa waingie ndani ya kitala cha kimbingu? Paulo alisema juu ya njia ambayo katika hiyo Yesu alitakasa kundi, “akilisafisha kwa mwosho wa maji kwa njia ya neno.” (Waefeso 5:26, NW) Kabla ya kifo chake, Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Nyinyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya neno ambalo mimi nimesema kwa nyinyi.” (Yohana 15:3, NW) Kwa sababu hiyo, hii bahari ya kioo kama fuwele lazima iwakilishe Neno la Mungu lenye kusafisha, lililorekodiwa. Wale wa ukuhani wa kifalme ambao wanakuja ndani ya kuwapo kwa Yehova lazima wawe wamekwisha safishwa kikamili kwa Neno lake.

  • Uzuri Mwingi Mno wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha Kimbingu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 25. Viumbe hai wanne na wale wazee 24 wanaunganaje katika kusujudia Yehova?

      25 Mbingu ya mbingu zote inavuma kwa sifa anazoimbiwa Yehova! Elezo la Yohana laendelea: “Na wakati wowote viumbe hai wanapotoa utukufu na heshima na utoaji-shukrani kwa yule Mmoja aketiye juu ya kiti cha ufalme, Mmoja ambaye huishi milele na milele, wazee ishirini na wanne huanguka chini mbele ya Mmoja aketiye juu ya kiti cha ufalme na huabudu Mmoja ambaye huishi milele na milele, nao hutupa mataji yao mbele ya kiti cha ufalme, kusema: ‘Wewe wastahiki, Yehova, hata Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu wewe uliumba vitu vyote, na kwa sababu ya penzi lako hivyo vilikuwako na vikaumbwa.’” (Ufunuo 4:9-11, NW) Katika Andiko lote, hili ndilo mojapo majulisho-wazi matukufu zaidi ya kumpa Yehova shikamoo, Mungu wetu na Bwana Mwenye Enzi Kuu!

      26. Ni kwa nini wazee 24 wanatupa mataji yao mbele ya Yehova?

      26 Wazee 24 wana mwelekeo wa akili ule ule ambao Yesu anaonyesha, hata wanatupa mataji yao chini mbele ya Yehova. Wazo la kujikweza wenyewe katika kuwapo kwa Mungu liko mbali zaidi sana na akili zao. Wao wanatambua kwa unyenyekevu kwamba kusudi pekee la umaliki wao ni kumletea yeye heshima na utukufu, kama afanyavyo Yesu sikuzote. (Wafilipi 2:5, 6, 9-11) Kwa unyenyekeo, wanakubali udhalili wao wenyewe na kukiri kwamba utawala wao unategemea enzi kuu ya Yehova. Hivyo, wako katika upatani wa moyo wote na wale makerubi na ule uumbaji mwingine wote wenye uaminifu katika kumpa sifa na utukufu Mungu ambaye aliumba vitu vyote.—Zaburi 150:1-6.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki