-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na vita ikafyatuka katika mbingu: Mikaeli na malaika zake wakapigana na drakoni, na drakoni na malaika zake akapigana
-
-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Jina “Mikaeli” lamaanisha “Ni Nani Aliye Kama Mungu?” Kwa hiyo lazima Mikaeli awe anapendezwa na kutetea enzi kuu ya Yehova kwa kuthibitisha kwamba hakuna wa kulinganishwa na Yeye. Katika Yuda 9 yeye anaitwa “Mikaeli, malaika mkuu.” Kwa kupendeza, jina la cheo “malaika mkuu” limetumiwa mahali pengine katika Biblia kuhusiana na mtu mmoja tu: Yesu Kristo.b Paulo husema kwa habari yake hivi: “Bwana mwenyewe atashuka kutoka katika mbingu akiwa na mwito wenye kuamuru pamoja, na sauti ya malaika mkuu na pamoja na tarumbeta ya Mungu.” (1 Wathesalonike 4:16, NW) Jina la cheo “malaika mkuu” lamaanisha “mkuu wa malaika.” Kwa hiyo haishangazi kwamba Ufunuo husema juu ya “Mikaeli na malaika zake.” Mahali pengine ambapo Biblia hutaja malaika wakitii mtumishi mwadilifu wa Mungu hurejezea Yesu. Hivyo, Paulo husema juu ya “ufunuo wa Bwana Yesu Kristo kutoka katika mbingu pamoja na malaika zake wenye nguvu.”—2 Wathesalonike 1:7, NW; ona pia Mathayo 24:30, 31; 25:31.
16 Haya na maandiko mengine yanatuongoza kwenye mkataa usioepukika kwamba Mikaeli si mwingine ila Bwana Yesu Kristo katika cheo chake cha kimbingu.
-