-
Wana-Farasi Wanne Katika Mwendo!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na wakati yeye alipofungua kifungo cha tatu, mimi nikasikia kiumbe hai wa tatu akisema: ‘Njoo!’” (Ufunuo 6:5a, NW) Kwa furaha kerubi huyu wa tatu “ana uso kama wa binadamu,” kuonyesha sifa ya upendo. Upendo wenye kuongozwa na kanuni utakuwa mwingi sana katika ulimwengu mpya wa Mungu, hata kama vile sifa hiyo nzuri sana inavyoenea katika tengenezo lote la Yehova leo. (Ufunuo 4:7; 1 Yohana 4:16)
-
-
Wana-Farasi Wanne Katika Mwendo!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na wakati yeye alipofungua kifungo cha nne, mimi nikasikia sauti ya kiumbe hai wa nne ikisema: ‘Njoo!’” (Ufunuo 6:7, NW) Hii ni sauti ya kerubi anayeshabihi tai arukaye. Hekima yenye kuona mbali ndiyo inayoonyeshwa hapa, na kweli kweli Yohana, jamii ya Yohana, na wengine wote wa watumishi wa Mungu duniani wamehitaji kuona na kutenda kwa muono-ndani kwa sababu ya kinachoonyeshwa na picha hapa.
-